Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Hakuna kitu kilichokuwa kikinishangaza - kama sio kuchefusha, kama kumsikia mwanasiasa, mwanaume au mwanamke mzima ambaye tunatumaini ana akili timamu na za kutosha, akitamka hadharani kwamba ameamua kutoka chama chake kwa kuwa eti amefurahishwa sana na Magufuli!
Hivi kweli hawa wanasiasa hawaoni aibu kutamka maneno kama haya mbele ya watu?
Wote siku zote tumeamini kwamba mwanasiasa anakuwa mwanachama wa chama fulani kwa kuamoni itikati au sera za chama hicho. Lakini mwanasiasa kuonyesha kwamba yeye suala la itikadi au sera za chama sio muhimu bali mtu fulani baki katika chama ndio anamvutia kiasi cha kuacha chama chake, huo ni ulevi na ujinga wa kisiasa ambao unatia hata aibu kuusema hdharani.
Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kwamba kuna watu katika siasa ni malaya wa kisiasa (political prostitution). Naamini kabisa alikuwa akiongelea watu kama hawa pia. Na baadae aliongelea kwamba kumpenda mtu na kutumia mapenzi hayo kwa mtu binafsi kama msingi wa kufanya uamuzi wa kisiasa haifai kabisa, kwa kuwa kupenda kwa namna hiyo kunapaswa kuhusianishwe na kutoleana posa! Alisema peleka posa tukacheka bila kuelewa aliwaza mbali sana.
Mimi nilitegemea kwamba wanasiasa hawa, hata kama ni kweli walihama vyama vyao kwa kufurahishwa na Magufuli, basi angalau wangekuwa na aibu ya kutuambia "nimehama chama changu kwa kuwa nimeipenda CCM na sera zake", sio "nimehama chama changu kwa kuwa nimempenda Magufuli". Huwezi kuwa mwanasiasa mwenye akili sawasawa ikiwa unahama chama chako kwenda CCM kwa kumfanya Magufuli ndio CCM.
Hebu fikiria, wewe unahama Chadema au CUF, na unajiunga na CCM kwa kuwa unafurahishwa na Magufuli. Sasa siku Magufuli akimaliza muda wake, au hata akishindwa uchaguzi wa 2020, utaenda aye Chato ukasaidiane kazi za nyumbani kwake na Mama Magufuli? Au tutarajie kwamba Magufuli akiondoka ikulu basi hawa wanasiasa itabidi watutangazie tena kurudi vyama walivyotoka kwa kuwa Magufuli sio raisi tena?
Kwa kweli akili ni nywele.
Hivi kweli hawa wanasiasa hawaoni aibu kutamka maneno kama haya mbele ya watu?
Wote siku zote tumeamini kwamba mwanasiasa anakuwa mwanachama wa chama fulani kwa kuamoni itikati au sera za chama hicho. Lakini mwanasiasa kuonyesha kwamba yeye suala la itikadi au sera za chama sio muhimu bali mtu fulani baki katika chama ndio anamvutia kiasi cha kuacha chama chake, huo ni ulevi na ujinga wa kisiasa ambao unatia hata aibu kuusema hdharani.
Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kwamba kuna watu katika siasa ni malaya wa kisiasa (political prostitution). Naamini kabisa alikuwa akiongelea watu kama hawa pia. Na baadae aliongelea kwamba kumpenda mtu na kutumia mapenzi hayo kwa mtu binafsi kama msingi wa kufanya uamuzi wa kisiasa haifai kabisa, kwa kuwa kupenda kwa namna hiyo kunapaswa kuhusianishwe na kutoleana posa! Alisema peleka posa tukacheka bila kuelewa aliwaza mbali sana.
Mimi nilitegemea kwamba wanasiasa hawa, hata kama ni kweli walihama vyama vyao kwa kufurahishwa na Magufuli, basi angalau wangekuwa na aibu ya kutuambia "nimehama chama changu kwa kuwa nimeipenda CCM na sera zake", sio "nimehama chama changu kwa kuwa nimempenda Magufuli". Huwezi kuwa mwanasiasa mwenye akili sawasawa ikiwa unahama chama chako kwenda CCM kwa kumfanya Magufuli ndio CCM.
Hebu fikiria, wewe unahama Chadema au CUF, na unajiunga na CCM kwa kuwa unafurahishwa na Magufuli. Sasa siku Magufuli akimaliza muda wake, au hata akishindwa uchaguzi wa 2020, utaenda aye Chato ukasaidiane kazi za nyumbani kwake na Mama Magufuli? Au tutarajie kwamba Magufuli akiondoka ikulu basi hawa wanasiasa itabidi watutangazie tena kurudi vyama walivyotoka kwa kuwa Magufuli sio raisi tena?
Kwa kweli akili ni nywele.