NAMTUMBA
JF-Expert Member
- Feb 20, 2014
- 1,939
- 600
Naomba kueleweshwa vizuri kuhusu watu wanaopinga Ushoga Nchini kwetu, hivi wanapinga nini haswa?
Kwamba Ushoga haupo au vipi?
Kwa maana maisha yangu yote tangu niko Mtoto najua kuna Mashoga wengi sana Dar akina Aunt Mudi (Marehemu) kulikuwa mpaka kuna Baa ya Macheni Magomeni, na karibu kila Mtu analijua hilo pamoja na Serikali yenyewe kwamba kwa macheni ilikuwa ni Baa ya Ushoga, sasa tatizo liko wapi hasa? Kwa nini leo hii ishu kubwa?
Nimesoma Shule na Watoto wengi tu walikuwa Mashoga na Shule nzima tulikuwa ^tunajua mpaka Walimu walikuwa wanajua, Sasa kwa nini kelele zote sasa hivi?
Tatizo ni liko wapi? Naomba kuelimishwa kwani hili swala linanichanganya Kidogo!
Mkuu hapo kwenye Blue ni typing error au? Nahisi ulitaka kuandika shule mzima tulkuwa mashoga.