Wanaopiga simu redioni kila siku wanatoa wapi fedha na muda?

Wanaopiga simu redioni kila siku wanatoa wapi fedha na muda?

Wajadi fundi wajadi(Binadam mashaka), Edward kabamba, Manyota top Manyota, Waziri dello, fundi hamis full migebuka, Daudi wakota, Hussein Laliga waziri mkuu wa dereva wa bajaji kutoka stendi kuu Lindi. Nk

Masumbuko shombe unamsahau vipi hapa
 
Miaka ya nyuma enzi za RTD Kulikuwa na watuma salamu maarufu kwa njia ya kadi na baadaye simu zilipoanza bado walikuwemo. Waliokuwa maarufu sana enzi hizo ni wajad fundi wajad wa mahuta shimon, Jumanne Sebarua Tingisha, Hawa Hassan Kilongo "super white orijino", Lusian Lems Ndambo wa Iringa, Mbago mhamed Mbago wa duka la mbolea pale Mbeya, wakulima wa ming'oko toka lindi nk. Sijui watu hawa kama wapo siku hizi
Wajad Fundi Wajad "binadamu mashaka"
Hahahaa umenikumbusha mbali sana.
Kuna mwingine alikuwa ajijiita ras Jah Gadi kutoka Trenchtown,mtoni mashine ya maji Dar.
 
Chaz Malaya Imara kama Simba,,,,,,,,,,,huyu jamaa alivuma sana miaka ya 90 mwishoni na 2000 mwanzoni.
Umenikumbusha huyu mtu. Ndo alikuwa wa Igoma kwa watu wazito?[emoji1] [emoji1]
 
Kuna wale ambao ujumbe wao BBC ndio uwa unasomwa tu pamoja na kwamba waliochangia kwenye habari husika ni wengi sana, sasa sijui uwa wanaselect ujumbe wao tu? Mmoja yuko Chunya, Kibaha, Muleba lazima uwasikie ujumbe wao unasomwa
 
Wananifurahishaga wale wa ushauri nasaha rfa daah pumba tupu na hamna msaada wowote. Wengine wanaamsha watu saa tisa usiku yaani daah tumetofautiana hatariii
 
Shangwe dereva bajaj wa Masasi [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Leo itabidi nikeshe na radio free usiku kucha niwasikie tena hawa jamaa,
kile kipindi kama sikosei kinaitwa the dance night show, kuanzia saa saba usiku hadi saa kumi na moja alfajiri

Mara ya mwisho wakati nasikiliza kilikuwa kinaongozwa na David Azaria au Coletha Makurwa. Nilikuwa nakesha nao.
 
Aseee daaaah!!! ata mim mekua najiulizaga ila kwq sasa kwa kuwa csikilz xn redio naon kidg imepungua,na huu utandawaz umekuja kupunguz kasi kdg khus upigaji simu...
 
Hahahaha, sasa afadhali huku, kuna ile radio ABOOD ya Morogoro, tena usiku kuanzia saaa saba wanapiga simu na kutuma salam kwa watu watano. Sasa kitu ambacho hunichekesha ni kwamba huwa wanatajana walewale mfano ally anapiga simu atatuma salam za kwa, rais wa sabuni, muuza bamia maarufu dumira, abdul machips, kakakuona, inshu inakuja kwamba mfano rais wa sabuni akipiga simu atarudia majina hayohayo niliyoyataja.
Kubwa kuliko wakishamaliza kutaja majina kuna kule kutuma ujumbe, sas hapo ndio kwenye kioja kikubwa ujumbe unakuwa wa ajabu sna, eg mtu atasema "UKILALA KWENYE MATANGA USIWE NA DESTURI YA KUJIKUNA SEHEMU ZA SIRI"
 
Back
Top Bottom