Wanaopiga simu redioni kila siku wanatoa wapi fedha na muda?

Wanaopiga simu redioni kila siku wanatoa wapi fedha na muda?

Jipe mwenyewe hiyo pole maana mm hata sijui kama kuna watu hupiga simu redioni kila siku
Ngoja nikusaidie. Natoka Nyumbani saa 6:30am na hufika ofisini saa 7:30 Kulingana na foleni kati ya Lugalo na Posta. Hapo nasikiliza radio.

Jioni kutoka posta kusukuma foleni lazima niwashe redio. Inatosha kabisa kusikiliza Power breakfast na Jahazi pamoja na BBC. Asante...
 
Ngoja nikusaidie. Natoka Nyumbani saa 6:30am na hufika ofisini saa 7:30 Kulingana na foleni kati ya Lugalo na Posta. Hapo nasikiliza radio.

Jioni kutoka posta kusukuma foleni lazima niwashe redio. Inatosha kabisa kusikiliza Power breakfast na Jahazi pamoja na BBC. Asante...
Muda huo huo unaoupata wa kusikiliza ukiwa kwenye jam,pia mwingine anaweza kuutumia kupiga simu kabisa wakati akiwa anafuatilia kipindi na kama ratiba zake zinafanana na zako kila siku anaweza kbs kupiga simu,na kwa swala la hela ya vocha huo ni ulevi kama ulevi mwingine,ndy maana kuna wavutaj sigara wasioweza kbs kukaa masaa mawili bila kuvuta.[emoji16]
 
Ngoja nikusaidie. Natoka Nyumbani saa 6:30am na hufika ofisini saa 7:30 Kulingana na foleni kati ya Lugalo na Posta. Hapo nasikiliza radio.

Jioni kutoka posta kusukuma foleni lazima niwashe redio. Inatosha kabisa kusikiliza Power breakfast na Jahazi pamoja na BBC. Asante...
Sasa wewe tangu umeweka uzi wako saa 2:16 asubuhi mpaka sasa hivi (saa 7:08 mchana) bado huko humu unajibizana na watu. Huo muda umeupata wapi? na bado unasikiliza redio kuwajua wote wanaopiga simu?!!!!!
 
Ostaadhi Saba Saba kutoka pale Sumbawanga, Lawena Nsonda,Yoram Mia Moja,Mwili Obare,Pagija wa Pagija,Akwino Msombe kutoka Uyole,Kituu Munishi,...orodha iendelee

Hawa ni maarufu hata jamii zao zinawatambua....huyo Akwino Msombe Mbeya pale anafahamika Sana japo ni fundi umeme Tu wa majumbani...harusi yake alipata jamii ya kutosha kumsapoti...plus Hilo hawa watuma salamu wana umoja wao husaidiana humo.....lakini pia suala Hilo si ushamba
° ni burudani baadhi Yao majina Tu unafurahia eg kina pagija wa pagija...

° ni sehemu ya 'ujamaa' ndio asili yetu mambo ya mageti na private lifestyle imekuja juzi...sie ni wajamaa tangu kabla ya sogesa

° ni fursa....Yule jamaa wa makongolosi anaeitika 'ee baba' lawena ni business man aliefanikiwa contributing factor ni umaarufu wake...I happened to meet him one time

° wanasaidia kutatua kero za jamii....sio kila mwanajamii anaweza kuzungumza...wao huzungumza on behalf...wakati wewe umejifungia kwenye gari yako na AC huku unalalamika matobo barabarani wao hupiga simu studios na kuwa-alert mamlaka waje wazibe hilo tobo.

° My very young brother ni journalist aliipenda hiyo kazi Kwa sababu mshua ni mtuma salamu wa DW na VOA Swahili miongo kadhaa iliyopita...so dogo alivutiwa na hilo...

Kwa hiyo usiwadharau watuma salamu
 
Muda huo huo unaoupata wa kusikiliza ukiwa kwenye jam,pia mwingine anaweza kuutumia kupiga simu kabisa wakati akiwa anafuatilia kipindi na kama ratiba zake zinafanana na zako kila siku anaweza kbs kupiga simu,na kwa swala la hela ya vocha huo ni ulevi kama ulevi mwingine,ndy maana kuna wavutaj sigara wasioweza kbs kukaa masaa mawili bila kuvuta.[emoji16]
Kupata line ni issue sana au MNA nafasi zenu.?
 
Kuna mitandao inatoa dakika 300 kwa mwezi kwa shilingi elfu 10, zinatosha sana kwa mtu anayependa kuongea na simu.
BTW wewe Archbishop uliyeleta hii hoja, mbona unashinda JF na mitandao mingine, unatoa wapi fedha na muda?

Vv
 
Ina maana vyuma vimebana sana huko eeehe!hadi vocha ni tatizo halafu mnasema turudi home!!
 
Kuna yule nani sijui wa Makongolisi Chunya, ni hobby kama hobbies nyingine.
"Naitwa Laweeena Nsonda wa Makoongorosi -Chunya,niambie baba mzazi"

Huyo jamaa ni mjasiriamali niliwahi kukutana nae yuko vizuri kiuchumi,ni mpambanaji ana fuso kama 4 na maduka.

Hata Rais JK alipokuwa katika ziara zake huko Chunya -Mbeya 2010,alipita makongorosi na msafara wake.Akaamuru msafara usimame akampigia simu hadharani Lawena Nsonda akaja na kumkabidhi Tsh.100,000 ikiwa ni mchango wa kuchangia kituo cha watoto yatima.Alimsikia Lawena redioni akiomba msaada wa kuwachangia watoto yatima na alimtaja mh.Rais.

HUYO NDIO Lawena Nsonda mzee wa makongorosi,Chunya.
 
Back
Top Bottom