Wanaoisaliti CHADEMA ni viongozi

Wanaoisaliti CHADEMA ni viongozi

Samawani wanaJF,
Kuna mdau mmoja amenitonya kuwa Mwali si mwanamke kama anavyojitambulisha na kuaminisha wengi hapa JF.
Kwamba the so called Mwali ni dume lililojivika kilemba. Naombeni msaada wa kutatua utata.

Btw, Selemani ni nani huko Bumbuli na ofisi ndogo ya ccm makao makuu lumumba?

Jibu hoja Mkuu!. mambo ya kusaka ID za watu humu JF mwachie Lema!
 
sasa mkuu hapo unajichosha kushaur!!nan kakuambia mbowe huwa anashauriw na wanachama?baba mkwe mzee mtei ndo mwenye final say na chadema!ukiona mbowe amefnya lolote kwny chama ujue hilo litakuw limetoka kwa baba yake na lilian

katiba ya chadema ndivyo inavyobainisha hivyo?

usiwe mtumwa wa fikra
 
TECH WIZ,

Lema kusema juu ya usaliti na kuonya ni kosa?Amekiuka ibara ya ngapi ya katiba ya CHADEMA?

Hilo la Mwigamba ikitangazwa hatua za kinidhamu zitafuata baada ya uchunguzi kukamilika ikiwa ataonekana kuwa na makosa
 
Last edited by a moderator:
Sio siri tena kwamba Chama sasa kinakabiliwa na dhoruba kali la kisiasa na Viongozi CHADEMA wasipokuwa makini huenda Chama kikafika 2015 kikiwa hoi bin taabani na binafsi nitaumia sana kama haya ndio yatakuwa matunda ambayo CHADEMA tutayavuna baada ya juhudi na bidii ya miaka mingi ya kujijenga Chama chini ya mateso na maumivu makali ya kimwili na kisaikolojia yaliyosababishwa na udhalimu wa vyombo vya dola kwa wakati wote ambao CHADEMA imekuwa katika harakati za kujijenga na kujiimarisha miongoni mwa Watanzania.Naweza kusema kuwa ng'ombe mzima tumeshakula bado mkia tu!Siamini!Mgogoro ulioibuka katika Chama baina ya makada kadhaa maarufu wa CHADEMA hauna afya kabisa kwa Chama na ukiachwa uendelee hivi huenda ukakiacha Chama kikiwa vipande vipande kabla hata ya mwaka 2015,Tusingependa hali hii iikumbe CHADEMA yetu kwa kweli.Ili kukata mzizi wa fitina na ili kuuzima huu mgogoro unaozidi kushika kasi ndani ya Chama ni muhimu basi kwa CHADEMA kuitisha Kikao kisha Lema na Mwigamba waitwe wakathibitishe hizo tuhuma

MKUU TECH WIZ kama unafuatilia kwa karibu mawazo ya wlio wengi utagundua nyimbo kama ZILPENDWA hazina mshiko tena na watu wamechoka nazo na ndiyo maana huu wimbo wako ni zilipendwa na watu wamechoka nao!!!!!!!!!!
 
Sio siri tena kwamba Chama sasa kinakabiliwa na dhoruba kali la kisiasa na Viongozi CHADEMA wasipokuwa makini huenda Chama kikafika 2015 kikiwa hoi bin taabani na binafsi nitaumia sana kama haya ndio yatakuwa matunda ambayo CHADEMA tutayavuna baada ya juhudi na bidii ya miaka mingi ya kujijenga Chama chini ya mateso na maumivu makali ya kimwili na kisaikolojia yaliyosababishwa na udhalimu wa vyombo vya dola kwa wakati wote ambao CHADEMA imekuwa katika harakati za kujijenga na kujiimarisha miongoni mwa Watanzania.Naweza kusema kuwa ng'ombe mzima tumeshakula bado mkia tu!Siamini!Mgogoro ulioibuka katika Chama baina ya makada kadhaa maarufu wa CHADEMA hauna afya kabisa kwa Chama na ukiachwa uendelee hivi huenda ukakiacha Chama kikiwa vipande vipande kabla hata ya mwaka 2015,Tusingependa hali hii iikumbe CHADEMA yetu kwa kweli.Ili kukata mzizi wa fitina na ili kuuzima huu mgogoro unaozidi kushika kasi ndani ya Chama ni muhimu basi kwa CHADEMA kuitisha Kikao kisha Lema na Mwigamba waitwe wakathibitishe hizo tuhuma

lumumba fc mnajitoa ufahamu na mwalimu wenu moyes
 
kuna vitu Tanzania ni unbelievable kabisa..

ndo maana hata wana JF wengi wanashinda MMU na CHIT CHAT sio sababu hawana uelewa
bali 'WANACHOSHWA NA KILA KITU'

CCM wako na kuibia wananchi na kuuza nchi
ulitegema CHADEMA watoe vision na hope nao ni even worse now

hata mtu kama Lema nae anaachiwa kuleta vurugu on top ya vurugu
shame...and sad
Mkuu The Boss, nimependa objectivity yako hapo kwenye bold!
Pasco
 
JF imekua sasa jukwaa la ndondi ambapo viongozi wa chadema wanagombana kwa maneno, kwa kuchafuana, wakidhani ku-convince opinion ya mashabiki wao jukwaa la siasa ndio tayari wananchi na taifa wamewakubali.
Viongozi wa Chadema wanatumia muda mwingi na resource za Chama kuchumia matumbo yao, then wanatumia resource zaidi kuficha uovu wao na kuwalipa mashabiki wao wakaeneze sumu mitandaoni dhidi ya wanachadema wenzao huku wakidai kua "wanasafisha chama", ndio maana hawawezi kudumisha demokrasia. Kusafisha kwenyewe hawasemi kutachukua muda gani na what are the criteria to this witch hunt!

Kwa mtindi huu (sorry, i meant kwa mtindo huu) sioni Chadema ikichukua uongozi in the next 100 years.

Anyway, najua walio na macho hawaambiwi tazama. Chadema has the potential to be an alternative to ccm ila kwa tunayo yaona siku baada ya siku tunakua na doubt. Na wanao wasaliti wanachama si wengine bali ni baadhi ya viongozi. Bahati mbaya hawawezi kuondolewa maana wamesha sitisha uchaguzi na wamebadilisha na katiba!

God protect Tanzania from such leaders!
Mkuu Mwali, nimekusoma kwa makini, huku nikitafakari na kujiuliza, hivi kweli viongozi wa Chadema huwa wanasoma mawazo kama haya?!.
Pasco.
 
you can't imagine eti mtu aitwe Msaliti kwa sababu tu anapinga Posho na eti kwa kuwa hachukui Posho!

Halafu wanajenga hoja eti oo hachukui Posho kwa sababu ana hela nyingi, Hivi Zitto na Mbowe nani ana hela nyingi, Mbona Mbowe anachukua posho kama kawaida?.

Chadema wanapinga Posho za wabunge kwenye vikao vya chama, lakini alas! Wabunge wake kina Lema wanataka kulia kisa kuna Mbunge mwenzao anaipinga kwa dhati!.

Viongozi wa Chadema should Walk the Talk, not Talk the Walk!!!!!
 
Samawani wanaJF,
Kuna mdau mmoja amenitonya kuwa Mwali si mwanamke kama anavyojitambulisha na kuaminisha wengi hapa JF.
Kwamba the so called Mwali ni dume lililojivika kilemba. Naombeni msaada wa kutatua utata.
Mkuu Mwita Maranya, kwenye hili, nimejitolea kusaidia kidogo, bila kumtaja jina, Mwali ni She!.

Nimetembelea first eleven yake humu jf ni hii hivyo ukiiangalia tuu utajua huyu ni she!.

Mahusiano, mapenzi, urafiki2,338

JF Chit-Chat1,972

Jukwaa la Siasa421

Jamii Photos335

Habari na Hoja mchanganyiko178

Mambo ya Kikubwa131

International Forum125

Complaints, Congrats, Advice102

Jukwaa la Lugha100

JF Doctor95

Love Connect88

Love Connect88
 
Nichukue tu hiyo mistari michache ya mwisho. Wewe ni nani mpaka uwaondoe HOFU wana-CDM? wenye chama huwa wanakuja na majina yao halisi humu. Tunawajua akina SLAA, BEN SAANAE, MWIGAMBA na weingine, iweje uje kututoa hofu na Id feki. Ukumbuke kuwa wengi kutofikiwa na CDM viijijini ni sababu mojawapo ya hao unaowaita wasaliti kutaka wafikiwe kwa hali mali na ndipo hubadilishiwa kibao na kuitwa wasaliti. Watafikiwaje wakati kuna watu wanataka kutengeneza mfumo wa fedha kwa tsh. mil 18 badala ya mil.2? watafikiwaje wakati machapisho ya kadi za chama yanafanywa na kampuni ya Mwenyekiti huko china, kwani kadi haziwezi kuchapishwa Tanzania? Kama mnataka CHADEMA isife ni lazima kwanza mtambue madai ya akina MWIGAMBA na wenzake kuwa ni ya msingi badala ya kuwaita wasaliti.

Aliyekuambia hilo jina ni fake ni nani? Mimi nimesema kama mwananchama wa chadema!
 
CDM inapoelekea kubaya sana. Huwezi kujustify ruzuku kwa njia yoyote ile ikiwa ni mwanamageuzi wa kweli. Hakuna Justification, uzi wa lema ya ruzuku na utu ni nothing but uroho wa wazi.

Kuna ethics gani kwa dharau kubwa kwaZito akiwa Naibu Katibu Mkuu wa CDM. Ikiwa yule kijana aliekuwa whistle blower amepewa kichapo, kuvunjiwa liberty yake na kusimamishwa kazi kwa visingizio vya usaliti hivi ni kweli hii ni promotion ya transparency? Ikiwa Lema ana haki ya kumjadili atakavyo Naibu Katibu Mkuu na kumuita mnafiki, huku akijustify kwamba hili halina mjadala na CDM ujue upeo wake wa fikra ni mdogo, akiwa unethical politician ndio leader wa chama hivi CDM haina interest ya kumuita na kumjadili badala ya kuwaacha wachache kumdharau na kumtusi hadharani?

Sijui huyu kijana anafikiri anayoyafanya yanaijenga CDM au kuibomoa, uongozi uliobomoka kimaadili utaendela kujadiliwa na JF badala ya vikao vya ndani vya kujisafisha na kusafisha chama. JF ndio itakayokuwa source ya machafuko na mgawanyiko wa CDM. Tunaitakia kila la kherilakini dalili za mvua mawingu.
 
Haya ndio yale nilikua nazungumzia:
Kwa vile chama tawala kina usaliti, basi chadema can be excuse. Haya ndio mawazo ya mashabiki wengi sababu viongozi wenu wanajitetea hivo na nyinyi mnaridhiana nao.
Kama chama tawala kina madudu lazima upinzani uwe msafi ili tuwaamini. Mkiingia kwa mtindo ule ule wa kukataa mawazo mbadala na kutumia vibaya pesa za uma sasa ni mbadala gani huo?

Sijawahi kuwa mshabiki yeyote ndani ya chama lakini najaribu kufuatilia mwenendo wa viongoz wetu ndani ya chama utabaini nini kinafanyika,sio dhambi kuwa na makundi japo itategemea ni kundi lipi lanaendana na mtazamo wako,ndani ya chadema kuna kundi linapigana kufa na kupona kuhakikisha chadema haifki popote pale kwa maslahi yao na chama tawara.
Kundi la pili ndilo lile linalopigana kufa na kupona kuhakikisha chama kinasimama imara na hatimaye kufkia malengo,na kundi la tatu ni lile linalokaa na kusubiria mivumo paspo kuijua chadema hawa kila mtu humwamini ni mwema ili mradi ana kadi ya cdm,zito ni mwanasiasa kijana nilimwamini sana kipindi cha nyuma lakini kufkia 2010 kwenye mkutano wake wa kampeni kwa wanakigoma kaskazini alitamka jambo ambalo nilishindwa kulielewa kwa mda huo,alitamka nataka mwaka 2015 nikija hapa sitawaombeni kura za ubunge tena ispokuwa za urais tu,hapo ni kwenye hadhara anatamka maneno hayo,nikajiuliza,atagombea urais kupitia chama kipi?na kama ni cdm anauhakika upi kuwa atapata fulsa ya kuwa mgombea?je asipopata fulsa hiyo je wanakigoma watamkubari mgombea mwingine?kama siyo yeye?kwanini atake yeye?tena kwa kulazimisha wakati ana jua ya kwamba jukumu la nani awe mgombea ni mchakato unaoanzia ndani ya chama,badala ya kusubiri watu wamwambie kuwa tunakuona unafaa kuwa rais yeye anasema anaweza.
Zito sku zote amekuwa akitafta sifa binafsi kwa masilahi yake badala ya kutata sifa kwa maslahi ya chama,kuendesha chama cha siasa na kipate mafanikio kwa siasa na sheria za nchi kama tz ni kazi ngumu sana ila kukibomoa ni kazi nyepesi mno,kwahyo lazima viongozi wawe makini sana watatumia njia za harali na hata za haramu kuhakikisha chama kinasimama bila kuyumba miaka yote.mfano cuf kilikua chama kikubwa cha upinzani walipokea ruzuka kubwa zaidi ya cdm ila hawakumdu gharama za kueneza chama chao kiwe na nguvu nchini sio kwamba walikua hawana mawazo ispokua dhamira ya kweli kwa kile wanachokisimamia hatimaye wapo kama hawapo,kama unazo akili timamu huwezi kulinganisha ccm na cdm,umesema viongoz wanaiba wanawekeza nje ya nchi na sio ndani ya nchi, je na wewe unauthibitisho?maovu ya ccm ndani ya nchi ni majanga kwa watz,chadema haijatenda kosa ambalo linagharimu maisha ya watz mwisho kwa ushauri wangu kama mnaona zito anaweza kuwa mtu mwenye nia njema na watanzani mumshauri atoke cdm na akaingie chama kingine awe mwenyekiti akisimamie hadi kifkie marengo ili na cdm waone mfano kwani gharama anazotumia kumiliki kundi ndani ya chama kulipia gharama za kuharibu chama ni rahisi akizitumia fedha hizo kujenga chama kingine kama kweli anayodhamila ya kweli.
 
Mwakalinga Y. R
===>Mimi binafsi simuamini ZZK hata siku moja maana yeye ndio muumini mkubwa wa hii mitandao ya kijamii,na anaitumia vizuri kuuumiza wenzake,kuuua CDM na kujijenga yeye mwenyewe,
Mathalani soma hapa uone jinsi ZZK alivyokuwa Ndumila kuwili:https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-zitto-kuhusu-lwakatare-maelezo-yangu-32.html
Jamaa ni zaidi ya tatizo ,ila uzuri kila anachokifanya against wapigania haki anaangukia pua . Tuachane na mabaya yake coz tumeshayajadili mpaka kero ,tusonge mbele tutafika .
 
TECH WIZ,

Lema kusema juu ya usaliti na kuonya ni kosa?Amekiuka ibara ya ngapi ya katiba ya CHADEMA?

Hilo la Mwigamba ikitangazwa hatua za kinidhamu zitafuata baada ya uchunguzi kukamilika ikiwa ataonekana kuwa na makosa

Hahahaha Ben, mbona unaji-contradict mwenywe, kigezo gani kwa Mwigamba kuwekewa uchunguzi na nidhamu baadae lakini ukawa tayari kumprotect Lema kwa kashfa kubwa against senior leader wa CDM. Hivi unadhani ikiwa ZZK ni unethical leader kama alivyomuonyesha Lema, huoni kama Ni best interest ya CDM kumjadili kwa uwazi, yeye Lema kupeleka hoja zake katika vikao vya ndani kama ilivyokuwa suggested kwa Mwigama, kuepusha kuichafua CDM kama Chama cha kubeba rogue leader?

Promotion ya transparency itawezekana vipi bila ya kuwaencourage whisle blowers? Alichokiandika Mwigama huhisi kwamba inawezekana ana genuine woga wa kutoweza kukisema mbele za watu na ingelikuwa vyema zaidi kwa uongozi CDM kujibu hoja zake badala ya kumsimamisha uongozi?

Tafauti gani hasa ya maelezo ya Lema against Zito na Mwigama against top wigs wa CDM hata iwe sawa kwa Lema lakini mbaya kwa Mwigamba?

Hivi hii tamthilia ya Lema unahisi hakukuwa na haja ya CDM kulijadili katika vikao vyake kwa kuhofia kuchafuwa taswira ya chama hasa kwa vile hizi bado ni allegation ambazo Zito anatakiwa kuzijibu, ikiwa Zito atakuja kuwa right na Lema yuko wrong jee image ya chama itakuwa katika naasi gani? Hivi kuna uzito mkubwa wa Lema kuwalk the talk kwa kuliwasilisha jalada la Zito mbele ya chama ili kumpa nafasi ya kujitetea na pia kuhakikisha chama kinamchukulia hatua ipasavyo if atanaonekana amekosea badala ya kuwaacha wanaJF wakawa ndio majaji wa kesi inayomkabili mmoja wa viongozi wakuu wa CDM..

Binafsi sijaona tafauti kubwa kati ya Lema na Mwigamba, kuficha ID yake sio kosa hasa ikiwa cdm inajali promotion za transparency katika chama, hoja hujibiwa na hoja sio mafukuzano na magumi, wanachokikosea jeshi la polisi ndio exact wanachokifanya sasa CDM, ukosefu wa hekima.. Kama Mwigamba anakosa, Lema nae amekosea kwa kuuchafua uongozi wa CDM hadharani..ZZK bado ni Naibu Katibu Mkuu wa CDM, na heshima ya cheo chake ingelifikiriwa zaidi na hizi hujuma ambazo zinaichafua CDM zaidi kuliko Zito.
 
Tatizo Mtei ameshikilia madaraka kwenye mkoba wake na anagawa kinyume cha Katiba.

Mtu kama Lema from no where anaibuka na kupewa ujumbe wa kamati kuu na kuanza dharau kwa waliokijenga chama, kisa tu kaongea vizuri na Mtei!!!
lema huwezi kumlinganisha na mwigamba weye; mlipeni ataenda nccr au cccm
 
dada wewe ni mwandishi mzuri sana, lakini linapofika jambo la Chadema sijuhi fahamu huwa inakutoka ama nini?
sasa kama huu uzi, sijuhi unaishauri Chadema, au unaionya? au unaicheka?, hebu jaribu kutuliza mihemko ya matukio yanayotokea , chukua muda wako na uandike kitu cheme maana na chenye kueleweka
​kitu imetulia wewe tu!
 
Mkuu Mwali, nimekusoma kwa makini, huku nikitafakari na kujiuliza, hivi kweli viongozi wa Chadema huwa wanasoma mawazo kama haya?!.
Pasco.

Nina hakika wanayasoma sana, lakini kwa vile yako against wao hawatayafanyia kazi.

Cdm supporters wanadhani bila umoja na mshikamano wa viongozi pale juu wataing’oa ccm madarakani. Uwingi wa watu kwenye mikutano kamwe haiwezi kuwa turufu ya ushindi.

Mambo mengine yanahitaji hekima na busara siyo kushabikia tu kwa sababu tumejawa na mahaba.
 
What made people believe in Chadema was the genuine reapect of democratic rules they set up from the begining. I really admired them when they went on primary elections.
Unfortunately as time goes, democratic values are progressively replaced by selfishness. Chadema is so intrinsically tangled into undemocratic scandals at this point that the mere mention of a democratical process threatens its leaders. Financial accountability, democratical elections, representing the people's agenda etc. Even pointing out these dark spots is in itself an anti-Chadema behavior.
Uchaguzi ni mwaka 2014 kikatiba. Kiherehere cha uchaguzi sasa hivi wa nini? Ni wana CDM watakaoamua kama ni muafaka kwa chama chao kufanya uchaguzi mwaka huu, 2014 au la. Wataamua kinachofaa kwa chama na mustakabali wa taifa.
Huku kote kutaka uchaguzi kwa njama hizi kunaonyesha kuwa wana CDM hawapaswi kufanya uchaguzi sasa hivi. Uchaguzi si kigezo cha kuimarisha chama. Unaweza kuibomoa vilevile. Na kwa vile CCM wameshaonyesha wazi kuwa wanataka kutumia huo uchaguzi kuvuruga CDM kabla ya uchaguzi wa 2015 ni busara kuacha kufanya uchaguzi. Uchaguzi ufanyike tu kama CDM wamemua kuwa bora wasubiri kuchukua dola lakini wawaondoe wasaliti kwanza. Vinginevo waachwe wajiondokee wenyewe bila kusingizia uchaguzi. Wakiondoka wenyewe watajionyesha wazi kuwa ni wapinga mabadiliko. Wanasubiri uchaguzi waanze mizengwe ya kuonewa ili waonekane wema mbele ya umma. Kamwe CDM isifanye kosa hilo. Vinginevo kama imewadhibiti ifanye uchaguzi.
Mimi kama mwananchi ninayetaka mabadiliko na maendeleo uchaguzi unanihusu nini? Haunihusu. watu kupigana kumbo kutaka kushika nafasi ya kula pesa hata kama wanaharibu chama ndicho kinachonihusu. Kama chama kiko imara sina sioni tatizo. Wasaliti wataumbuliwa na wale wanaotumia nafasi zao vibaya chamani wataondolewa.
 
Back
Top Bottom