Wote tunajua kuwa mapambano yoyote ya kujikomboa huwa hayakosi vikwazo, au wapinzani wa Mapambano hayo wawe wa kutoka ndani au nje ya kundi linalopambana! Wakitoka ndani ya kundi ndo wanaitwa wasaliti. Lakini katika Historia wasaliti hawajawahi kuzuia dhamira ya mapambano isitimie kwa wakati! Chadema ilipofikia na mapambano yalipofikia haina haja ya kuhofia wasaliti, inayo nguvu na uwezo wa absorb shock zitakazoletwa na msaliti wa aina yoyote! Ziko namna za kudeal na wasaliti kwa calculations ili kupunguza risk na impact yake kwenye Chama, lazima ujue hao unaowaita wasaliti nimwatumishi wa kambi nyingine iliyokinyume na Chadema either kwa kujua au kwa kutokujua, kwahiyo Chama lazima kiwe na busara ya kudeal nao. Lazima ujue msaliti huwa anasura mbili sura inayoonekana nje siyo ya kisaliti anaonesha sura malaika lakini ndani ni umbwa mwitu, na hivyo baadhi ya watu hao huwa ni watu wenye ushawishi kwenye jamii lakini ndani yao ni wasaliti wakubwa, kwahiyo lazima chama kiwe na busara namna ya kudeal na wasaliti, wasaliti hawataisha kwenye taasisi yoyote, na pengine siyo wote watakaondolewa au hata kugundulika na wasaliti wengine hawatakiwi kuondolewa kwenye chama kabisa kwasababu kuwabakiza na kuwanyima mazingira ya kuondoka ni mkakati pia wa ushindi kwa dhamira ya ukombozi. Na Hapa nitaomba with all due respect nitofautiane na Kiongozi wangu Mh. Godbless Lema, Chadema haiwezi kuacha ku-pursue cause ya mabadiliko na ikaazisha vita ya wenyewe kwa wenyewe eti ya kupambana na wasaliti, hatuna sababu ya kufanya hivyo wala si busara kufanya hivyo! Wasaliti hawajaizui Chadema kujenga Chama na kuendelea kujiimarisha vijijini na mijini, katika kipindi chote baada ya uchaguzi mkuu 2010 Chadema imepiga hatua kubwa na imejenga imani kubwa sana kwa wananchi siyo kwamba wasaliti hawakuwepo, wasaliti wanapaswa kuwepo washuhudie dhamira ya ukombozi ikitimie mbele yao, hatuna sababu ya kuanzisha vita na wasaliti, wakati nguvu hiyo tunaweza kuitumia kuingiza maelefu ya wanachama wapya wanaoisubiri chadema vijijini na hawajafikiwa! Mimi naamini Godbless Lema ni mtu ambaye ni positive thinker sana ila kwa hili la wasaliti approach yake ni destructive kwa mustakabali wa Chama na itatuchelewesha kutimiza dhamira yetu ya Ukombozi. Na yeye kama mjumbe wa kamati kuu amepotoka kuongelea maswala nyeti ya Chama kwenye mitandao! Nashauri atumie vikao husika ambavyo yeye ni mjumbe kutoa maoni yake. Mwisho nitoe wito kwa wapenzi na wanachama wa Chadema na wapenda mabadiliko wote kuwa Chadema iko imara, Chadema haina hofu na wasaliti, Chadema imejipanga kuchukua dola 2014/2015!
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Chadema.