Wanandoa na extended family

huyo alizidi sasa khaaa! yaani mumlee yeye pamoja na familia yake! hata mie siwezi.

my dear yakikufika utafanya tuu if it is meant to be so.
haya mambo hayana kanuni manake kila ajae kwako ipo riziki yake kwako, mtu haji kwako hivi hivi, muda mwingine unaweza kupata wagen hadi ukajiuliza ivi sasa humu ndani tutaishije?? utashangaa unapata riziki mnakula hadi wanapofikia kuondoka.

naelewa kwamba ni gharama sana lakin mara zote niwazapo kwamba maisha hayana kanuni maalum huwa nasema iwe kama ilivyo, ingawa ninasheria kwangu nikikaa na wewe nikakupeleka shule once ukipata kazi/kibarua utaanza kujitegemea
 
Ndugu yangu, ukitaka kuelewana na mtu yoyote epuka chakula chake.....take my Words....

Kim nana, Hilo nimejifunza tangu utoto, hata maza alinifundisha kutokula kwa watu. Lakini nimeshindwa kuwaelewa wanawake katika hili...!!
 
Last edited by a moderator:

Kama ulichoandika ndicho unachoishi, then wewe ni mama na mke bora. Kizazi chetu kimekuwa na uchoyo, ubinafsi na umimi. Hata watoto wetu tunawafundisha vibaya.
 
Kuishi na extended family ni changamoto sana. Inabidi wakati mnaoana muweke house rules kuhusu kuishi na ndugu.
 

kuna jambo ambalo watu hawalielewi, mara nyingi sana wanawake huwa hawapatani hasa wakaapo chini ya dari moja. yashindikana mama na bintiye huwa kila mara ni kugombana sembuse mwanamke mwingine??

mke amekaa kuyaona makosa ya ndg wa mume, ndg wa mume wamekaa kuona makosa ya mke wa kaka yao so wanaviziana na kila mmoja anataka aonyeshe ubabe wake hapo.

to me wala sina haja ya kushindana na wewe manake kama unaweza ingia rum ulale na kaka yako lakin kama mpera naufaidi mie basi kwangu wewe ni banadamu unayestahili heshima tu na wala siwez kupoteza muda kugombana na wewe milele.

i have a friend of me dada wa mumewe alimtafutia mumewe mke, kazi na nyumba ya kuish, akimwambia achana na mkeo wa ndoa njoo nyumban huku kuna mke mzuri tumekutafutia na kazi nzuri ambayo mume alishatumiwa hadi employment contract ajaze arejeshe na pia wamempangia nyumba.

mke siku kama Mungu kamuonyesha hana hili wala lile kazikuta sms kenye wassap ya mumewe akaangalia sms zote wifi alizomtumia mumewe ila hakuona za mume.

bidada kumbe nae aliwahigi kutongozwa na mume wa wifi yake na mbaya zaid wakati anamtongoza alimshirikisha mumewe na kuna siku yule bwana alimtumia bidada ela kwa western union na akamuonyesha mumewe. lakin wakafanya siri ili wsivunje ndoa ya wifi mtu.

sasa mchezo ulikuja kunoga yalipotokea haya ya mume kupatiwa mke mwingine bidada alifunguka kaa bomba kuu la gesi linapolipuka, alaiwasha moto na kuforward sms zote ambazo alitongozewa na yule mume wa wifi kisha akamalizia na matus yasiyona kipimo. yaani mpaka sasa ile familia ya wifi mtu inahaha manake ni aibu iliyojee??
 
chokochoko hizi mara nyingi husababishwa na ugumu wa maisha (unaweza ita umaskini katika familia) hivyo huyo mmoja mwenye ka-uwezo kila mtu anataka amegewe japo chochote na wakati mwingine huvuka hata mstari wa nini amegewe, mke akisimama kwenye principles za familia ndo anaonekana mmbaya. Hata hivyo, ndo hali halisi ya familia zetu kikubwa ni nini kifanyike? ni wenye dhamana hasa baba kusimamia usawa haki na uhalisia. Ndugu akiruka mstari anarekebishwa instant, mke akivuka mstari anarekebishwa instant. Kama ndugu wapo wengi wote wanafate principles sawa, hakuna kubaguliwa wala kupendelewa. Mkiishi hivi hakuna mikwaruzo na hata ikitokea itakuwa ile ya kawaida.
 
Kama ulichoandika ndicho unachoishi, then wewe ni mama na mke bora. Kizazi chetu kimekuwa na uchoyo, ubinafsi na umimi. Hata watoto wetu tunawafundisha vibaya.
kiukweli mie kwangu ukija ndugu wala sijiulizi mara mbili mbili, na hata kama utakuwa mgonjwa nitakutibia ukipona utaondoka kwa amani na hata kama utanilipa baya sitawaza manake najua majaribu yapo na mtu hujaribiwa kwa akipendacho.

iko hivi mara nyingi sana akina mama/wake mioyo yetu huwa kwenye ndoa zetu na ndicho kitu tukipendacho zaid na shetan naye kwa kulijua hilo huwa anatujaribu kupitia ndoa zetu. ujue pale moyo wako ulipo ndipo hazina yako ilipo na wengi badala ya kumfanya Mungu kuwa hazina zetu na mioyo yetu kuwa kwake siye tumefanya hazina zetu kuwa ndoa zetu na mioyo yetu kuwa hapo. kinachotokea NI iBILISI kukujaribu kupitia ndoa iyo iyo.

chunguza kwa wanawake wote wanaopitia magumu kwenye ndoa wengi watakuambia ndoa zao wanazipenda na ndo mana zikileta shida wanakonda na kuchoka kabisa yaani ata kama akitafuta mchepuko ataenda tuu kwa tabia za kimwili lkn moyoni hilo linamuuma kuliko jambo lolote lile.

Tumtangulize Mungu zaid kwenye maisha yetu na yeye atahangaika na yale yaliyo ya haki yetu
 

Asante kwa ushauri mzuri dada mkubwa gfsonwin...

Be blessed!
 
Last edited by a moderator:

Well said wakwetu... Nimepata kitu hapa.

Wakondya....
 
Kuishi na watu wasio na kazi ni kazi.
Kuishi na mtu mzima mwenzako ni kazi kubwa. Baba yangu aliwahi mwambia Mama kuwa hawa watoto wakioa waache wakae wao wenyewe na wake zao, tusije tukapata taabu. Na mzee aliwahi sema hatakuja lala kwa mtoto wake yoyote.
Wanajiweza zaidi yetu.
 
Kwa vile familia zetu za kiafrika extended family for some reasons imekua kama part of family hatuna option, lakini honestly isingekua umaskini wetu ishi na mkeo/mumeo na watoto, mtu baki awe house girl/boy kwisha. Mtoto wa kaka, dada, shangazi, mamdogo, mdogo etc.. wasiwe na nafasi kwenye familia yako. Kama ni msaada wasaidie huko waliko. Usipokua mwangalifu watoto wako mwenyewe watakosa haki za msingi kutoka kwenu only kwa sababu mnategemewa na ndugu. Mimi nilikua katika mazingira ya extended family, ndugu zaidi ya watano hadi kumi ndani ya nyumba. Hakuna shukrani hata moja, hata uwafanyie nini. Tulipokua na maisha yetu, baba yangu alikua mkali sana akisikia unaishi na ndugu wa mume au mke. hakutaka yale yaliyomkuta yeye ya kusaidia ndugu wasiokua na shukrani yatukute na sisi. Mimi kwangu mtu baki ni house girl/boy sina zaidi. Na mume wangu nilimpa darasa akaelewa hivyo. Tunasaidia ndugu lakini kwa remote control.
 

Asante.


Aamen!
 

Si mpaka umpate mwanaume muelewa... Sio wanaume wote utakaowaambia tuwasaidie ndugu wakiwa mbali.

Ukute hao ndugu ndio walikuwa wanaishi na mumeo tangu awali, utawezaje kuwaachanisha??

Cha muhimu ukikuta kuna ndugu kwa mumeo ni kujifunza kuchukuliana nao tu la sivyo wewe ndio utaonekana mbaya.

Kuwa busy na kazi zako, fanya majukumu yako na pia watafutieni kazi / shule wawe busy sio kukaa nao pasi na chochote wafanyacho!

Ni mtazamo wangu CL...
 

unapotoa msaada usiufanye deni wala usingoje shukrani!
 


Na hicho ndicho ninachomaanisha..

Jaribu kuangalia kwenye kamusi ya kiswahili maana ya neno "kufuga". Na kama bado lina utata tunaweza kuendelea na mjadala wa hilo neno.

Na kama umekuwa ukifuatilia michango yangu, ni kwamba nilishachoka na mambo ya ndugu. Na kwa kweli nakosa neno zuri zaidi la kutumia. Sorry, kama nimekukwaza!
 

Baba akifika kuwatembelea halali kwenu?...duh!
 
Baba akifika kuwatembelea halali kwenu?...duh!

Tunaishi Mkoa mmoja ,Wilaya moja umbali ni kilometer 20 tu.
Hivi kama ananizidi pesa anauwezo gani kulala kwangu
 
Hii maada ningumu musiichukulie poa kila mtu inanulenga kwa namuna moja au nyingine hivyo wataaram wa maswaara haya wajitokeze watufafanulie.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…