Kamanda Asiyechoka
JF-Expert Member
- Sep 13, 2020
- 3,166
- 4,581
HABARI Wananchi wa Kitongoji cha Ihula kilichopo Kata ya Gibishi Halmashauri ya wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu wameamua kujenga nyumba za tope ili kuwawezesha Walimu kuishi jirani na shule.
Wananchi hao wamesema walimu wakiwa karibu na mazingira ya shule wanao uhakikia wa kuwahi hususani vipindi vya asubuhi hivyo kuwawezesha watoto wao kuanza kufundishwa mapema.
"Tumeamua tujenge nyumba ili watoto wetu wapate huduma ya kufundishwa, hatuna nguvu ya kuwajengea nyumba ya block ndio maana tukaamua tujenge nyumba ya tope ili wasogee huku," amesema Loli Machama ambaye ni mwananchi