Wanamuziki wa extra musica

Wanamuziki wa extra musica

STEPHEN JIBE

Member
Joined
Jan 23, 2013
Posts
61
Reaction score
9
Habari wanajamii,napenda kuuliza maswali yafuatayo; Kila Mbongo wa Extra Musica yu wapi sasa bend hyo maendeleo yake yakoje na huyu Ramatoulay ndio yule aliyeimba ule wimbo wa alaj maana majina yao na saut vinanichanganya sana.
Naomba msaada wenu wadau
 
Habari wanajamii,napenda kuulzg maswal yafuatayo; kila mbongo wa extra musica yu wapi sasa bend hyo maendeleo yake yakoje na huyu ramatoulay ndo yule aliyeimba ule wimbo wa alaj maana majina yao na saut vinanichanganya sana.
Naomba msaada wenu wadau

mkuu hao c kitu uliza Wenge musica bcbg 4*4,hao walikuwa noma
 
Kila mbongo hayupo tena kimuziki.kuna uwezekano kabisa kazamia mamtoni.extra musica inaendelea ikiongozwa na baba lao roga roga.wale wakali wa zamani ktk bendi hiyo wengi hawapo.bendi ipo na sebene linagongwa kisasa zaidi
 
Kila mbongo hayupo tena kimuziki.kuna uwezekano kabisa kazamia mamtoni.extra musica inaendelea ikiongozwa na baba lao roga roga.wale wakali wa zamani ktk bendi hiyo wengi hawapo.bendi ipo na sebene linagongwa kisasa zaidi

kila mbongo ni habari nyingine.
 
Kila mbongo hayupo tena kimuziki.kuna uwezekano kabisa kazamia mamtoni.extra musica inaendelea ikiongozwa na baba lao roga roga.wale wakali wa zamani ktk bendi hiyo wengi hawapo.bendi ipo na sebene linagongwa kisasa zaidi

kila mbongo ni habari nyingine.

kila mbongo si ndo yule jamaa mrefu?kama ni huyo hayupo tena kimziki tetesi ni kuwa yupo ubelgiji kwa shughuli zake nyingine,ila kumbuka mtu alikuwa anaitwa Roberto Enkokota huyu alikuwa Wenge bcbg hakuna repa aliekuwa anamfikia
 
kila mbongo si ndo yule jamaa mrefu?kama ni huyo hayupo tena kimziki tetesi ni kuwa yupo ubelgiji kwa shughuli zake nyingine,ila kumbuka mtu alikuwa anaitwa Roberto Enkokota huyu alikuwa Wenge bcbg hakuna repa aliekuwa anamfikia


Anaitwa Roberto Wuunda Ekokota...
Haya sahihisha hilo jina lako kabla sijarudi
 
kila mbongo si ndo yule jamaa mrefu?kama ni huyo hayupo tena kimziki tetesi ni kuwa yupo ubelgiji kwa shughuli zake nyingine,ila kumbuka mtu alikuwa anaitwa Roberto Enkokota huyu alikuwa Wenge bcbg hakuna repa aliekuwa anamfikia


Lamatoulay alikuwa anapiga Drums...
Kila Mbongo mazikoya ana rap...
King Rogaroga anacharaza Solo...
espa Bass anacharaza Bass...

Dah bendi hii ilidumu mpaka albam ya pili ya Confirmation kisha ikaanza kumong'onyoka huku ikibaki ngangali.

Kuna watu wawili ama watatu muhimu kabisa katika bendi hii walijitoa na kwenda kuanzisha Extra Musica International.
Lakini Extra waliobaki walitoa albam yao ya 3 ya Losambo na kitu kikabamba.
Kisha wakaenda toa albam yao ya 4 ya Etat Major nayo ikabamba ile mbaaaya.
Kisha ikaTolewa Obrigator nayo ikabamba mbaaya.

Na hapo ndipo ulikuwa mwisho wa mimi kuifuatilia bendi hii niliopata kuipenda sana.
Hakika kama wangeweza kudumu basi wangeurudisha mtindo wangu boora wa Soukous japo wao hawakutokea Congo hii ya Kabila...
 
Congo nzima hakutakuja kuwa na bendi kama Wenge BCBG ile ya Jp Mpiana na Werrasson Ngiama. Wengine wanaruka ruka 2

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
angalia wmbo wa shalai mwshon kuna sehem jamaa kama wanaita hv"shalaaaaaai!" na kelele nyng huku bit lime2lzwa na kuna jamaa anaongea kwa saut kubwa huk pcha zake zikiwa slow motion kavaa shat dak bluu,tai ya kaki na kot jeupe.
yule jamaa ndo nani
 
Lamatoulay alikuwa anapiga Drums...Kila Mbongo mazikoya ana rap...King Rogaroga anacharaza Solo...espa Bass anacharaza Bass...Dah bendi hii ilidumu mpaka albam ya pili ya Confirmation kisha ikaanza kumong'onyoka huku ikibaki ngangali.Kuna watu wawili ama watatu muhimu kabisa katika bendi hii walijitoa na kwenda kuanzisha Extra Musica International.Lakini Extra waliobaki walitoa albam yao ya 3 ya Losambo na kitu kikabamba.Kisha wakaenda toa albam yao ya 4 ya Etat Major nayo ikabamba ile mbaaaya.Kisha ikaTolewa Obrigator nayo ikabamba mbaaya.Na hapo ndipo ulikuwa mwisho wa mimi kuifuatilia bendi hii niliopata kuipenda sana.Hakika kama wangeweza kudumu basi wangeurudisha mtindo wangu boora wa Soukous japo wao hawakutokea Congo hii ya Kabila...
Solo la Rogaroga kwenye Shalai ni moto
 
Kabla ya ujio wa extra musica, wenge musica lilionekana kundi bora tena lenye damu changa. Lakini kuibuka kwa extra musica 95 na wimbo wao wa freddy nelson kuliishtua dunia na kufanya kila mpenda bolingo aulize ni wakinani hawa jamaa. Bendi hii imepata mafanikio sana nakuchukua tuzo mbalimbali kama za Kora Africa na best band of africa ya muongo. Leo niishie hapa nitakuja na full history ya hawa jamaa kuanzia walipotokea,wanamuziki wa kwanza wa bendi,albamu zao zote, walipo sasa na shughuri wafanyazo stay tuned. More info. Check me via bislisk@yahoo.com
 
Sikuwa mshabiki sana wa dansi lakini Extra Musica walimikamata...

Ni mpenzi sana wa ufundi na mautundu ya upigaji solo na drums na nikubali hawa jamaa walikuwa ni mafundi
 
Hapa Extra Musica ilikuwa imekamilika. Kibao ni Amie Reviens kutoka albamu yao ya kwanza inayojulikana kama Les Nouveaux Missiles ya mwaka 1995.

 
Last edited by a moderator:
Extra Musica ni bendi kutoka Congo Brazzaville, sio DRC kama watu wengi wanavyodhani. Nchi hizi ni majirani na miji yao mikuu Brazzaville na Kinshasha imetenganishwa na Mto Congo. Kilingala kinazungumzwa katika nchi zote mbili.
 
nawakubali sana kuliko bendi yoyote ile duniani mpaka sasa,ya pili ni wenge mesomere ya werason ngiama makanda
 
Back
Top Bottom