kila mbongo si ndo yule jamaa mrefu?kama ni huyo hayupo tena kimziki tetesi ni kuwa yupo ubelgiji kwa shughuli zake nyingine,ila kumbuka mtu alikuwa anaitwa Roberto Enkokota huyu alikuwa Wenge bcbg hakuna repa aliekuwa anamfikia
Lamatoulay alikuwa anapiga Drums...
Kila Mbongo mazikoya ana rap...
King Rogaroga anacharaza Solo...
espa Bass anacharaza Bass...
Dah bendi hii ilidumu mpaka albam ya pili ya Confirmation kisha ikaanza kumong'onyoka huku ikibaki ngangali.
Kuna watu wawili ama watatu muhimu kabisa katika bendi hii walijitoa na kwenda kuanzisha Extra Musica International.
Lakini Extra waliobaki walitoa albam yao ya 3 ya Losambo na kitu kikabamba.
Kisha wakaenda toa albam yao ya 4 ya Etat Major nayo ikabamba ile mbaaaya.
Kisha ikaTolewa Obrigator nayo ikabamba mbaaya.
Na hapo ndipo ulikuwa mwisho wa mimi kuifuatilia bendi hii niliopata kuipenda sana.
Hakika kama wangeweza kudumu basi wangeurudisha mtindo wangu boora wa Soukous japo wao hawakutokea Congo hii ya Kabila...