Wanamuziki wa extra musica

Wanamuziki wa extra musica

Extra Musica ni kundi la muziki linalotoka katika nchi ya Congo Brazzaville. kundi hili lilianzishwa mwaka 1993 na wanamziki walioanzisha kundi hili ni Roga Roga na Espe Bass. Pamoja nakuanzishwa mwaka huo 1993, walifanikiwa kutoa albamu yao ya kwanza mwaka 1995 iliyoitwa Les Nouveaux Missiles. Albamu zingine ni Confirmation (1996), Ouragan 1997(Champions d’ Afrique), Etat-Major (1998) , Shalai (1999), Trop C’est trop(2001), Obligatoire(2004), La main noire(2006), Sorcellerie (Kindoki)-2011. Wanamziki waliokuwepo tangu albamu ya kwanza ni
Ø Waimbaji ; Guy Guy Fall, Quentin Moyascko, Oxygene (Mbon Sylvain), Dou dou copa (Elenga Laka Bienvenu Dominique), Christian na Herman Ngassaki (Don Mfumu).
Ø Atalaku ; Kila Mbongo
Ø Gitaa la solo; Roga Roga (Ibambi Okambi Rogatien)
Ø Gitaa la base; Espe Base
Ø Gitaa la Rhymes ; Durell Loemba
Ø Drummer; Ramatoulaye (Ngolali G)
Ø Keyboard & Horns; Christian Kingstall

Wanamziki wengine wa kundi hilo wa mwanzo walikuwa Pinochet Thierry, Regis Touba, Cyrille Malonga na Arnaud Laguna. Albamu ya kwanza Herman Ngassaki na Dou dou Copa hawakupata nafasi kubwa sana ya kuimba kutokana na uwepo wa mtu kama Guy Guy Fall, Oxygene, Christian na Quentin Moyascko katika safu ya waimbaji.

Baada ya kufanya vizuri sana albamu yao ya kwanza Mwanamziki Abilissi (Samba Brice) alijiunga na Extra Musica hivyo naye kuwemo katika safu ya waimbaji ya Extra Musica walipotoa albamu yao ya pili ya Confirmation. Ujio wake ulifanya jumla ya wanamziki saba kuwa katika safu ya uimbaji wa Extra Musica ambao ni Guy Guy Fall, Dou Dou Copa, Christian, Oxygene, Herman Ngassacky, Abilissi na Quentin Moyascko. Safu hii ilifanya albamu yao ya pili kuwa moto kuliko ya awali na hivyo kuteka hisia toka sehemu mbalimbali Afrika na duniani kote huku ikichombezwa na atalaku za Kila Mbongo na gitaa la Roga Roga.

Baada ya kufanya vizuri sana albamu yao ya pili, mgogoro wa kimaslahi na kiuongozi ulilikumba kundi hili na kupelekea wanamziki kama Christian na Guy Guy Fall kujitoa na kutokuwepo kwenye albamu ya tatu ya kundi hili. Nafasi zao zilijazwa vyema na Herman Ngassaki aliyechukua nafasi ya Guy Guy Fall na Abilissi aliyechukua nafasi ya Christian na huwezi sikia kutajwa kwa Guy Guy Fall na Christian albamu ya Oargun. Herman Ngassaki alifanikiwa sana kuitumia sauti ya Guy Guy Fall katika album zote ambazo Guy Guy Fall na ukitaka ujue jinsi wanavyofanana kisauti sikiliza wimbo wa Success Extra anavyoanza Guy Guy Fall na usikilize wimbo wa Lolango katika album ya Oaragan namna anavyoanza Herman Ngassaki, usipokuwa makini unaweza jua ni mtu mmoja kumbe sio.


Pamoja na kukimbiwa na waimbaji hao wawili bado kundi lilbaki imara sana na kufanikwa kutoa albamu yao ya tatu huku Guy Guy Fall akienda kufanya kazi kama mwanamziki wa kujitegemea(solo Artist) na mpaka leo yupo kivyake na habari za Christian kimziki kuishia hapo.

Lakini pamoja na kutoa albamu hii ya tatu, kundi liliingia tena kwenye mgogoro mkubwa na kusababisha wanamziki wapatao sita kuondoka na kwenda kuunda kundi la Extra Musica International. Wanamziki hao ni Pinochet Thierry, Regis Touba, Cyrille Malonga, Durell Loemba ,Quentin Moyascko na Arnaud Laguna. Huko nako baadae Extra Musica International iligawanyika na kundi la ZI International kuundwa chini ya uongozi wa
Durell Loemba, Pinochet Thierry, Regis Touba na Cyrille Malonga, huku Extra Musica International ikibakiwa na Quentin Moyascko na Arnaud Laguna.

Baada ya kukimbiwa na wanamziki hawa Extra musica chini ya uongozi wa Roga Roga walijipanga na Ku-recruit wanamziki wapya kama Sonor aliyechukua nafasi ya Durell Loemba katika gitaa, Gildas Pozzi na Emery Mbona wakisimama katika Tumbas. Safu ya uimbaji ikabakiwa na wanamziki wanne tu ambao ni Oxygene, Herman Ngassaki, Dou Dou Copa na Abilissi. Atalaku ikiongozwa na Kila Mbongo huku kwenye drummer akisimama Ramatoulaye, keyboard kama kawaida ni Christian Kingstall, Gitaa la base Espe Bass na la Solo ni Roga Roga na kufanikiwa kutoa albamu ya nne iitwayo Etat-Major ambayo inaaminika kuwa ni albamu bora ya kundi hili. Albamu hii sio tu ilivunja rekodi ya mauzo ya kundi hili bali pia iliwafanya kupata mialiko mbalimbali ya kimataifa ikiwepo Tanzania. Pia album hii iliwafanya kuchukua tuzo nyingi Afrika ikiwepo tuzo ya Kora kama kundi bora la mziki kwa Afrika.

Baadae walitoa albamu yao ya tano iliyokuja kujulikana kama Shalai na ndiyo ilikuwa albamu ya mwisho kwa Rapa wa muda mrefu wa kundi hili Kila Mbongo baada ya kujiengua na kundi hili na kuchana na mziki. Pia ilikuwa ni albamu ya mwisho kwa Abilissi. Pia katika albamu hii wanamziki kama Papy Batin Maboulango na Boudouin Massipi walishiriki baada ya kujiunga na kundi hili kwa mara ya kwanza.

Kimya kidogo kilipita kabla ya kutoa albamu ya sita ya kundi hili iitwayo Trop c’est trop huku rapa akiwa ni mpya baada ya Kila Mbongo kuacha muziki. Rapa huyu mpya aliitwa Arafat.
Baada ya albamu hii ya sita ya, kundi hili lilibadili jina na kuwa Extra Musica Zangul.

Mwaka 2004 wakafanikiwa kutoa albamu yao ya saba iitwayo Obligatoire. Mwaka huohuo baada ya kutoka albamu hii Dou Dou Copa Alijitoa na kuwa mwanmziki anayejitegemea (solo Artist) na Oxygene alijitoa mwaka 2005 na kuunda kundi lake la Universal Zangul huku akiondoka na baadhi ya wanamziki ambao walikuwa hawapati nafasi ya kuimba katika Extra Musica Zangul.
Pamoja na kuondoka Oxygene na Dou Dou Copa bado kundi hili lilitoa albamu yao ya nane mwaka 2006 iitwayo La Main Noire na albamu ya tisa ambayo nikama ya Roga Roga iitwayo Sorcellirie(Kindoki) na imetoka mwaka 2011.

Kwasasa kundi lipo kisasa zaidi na linapiga Rhumba ya kisasa zaidi huku rapa wake ni Zaparo. Wanamziki wa awali waliopo mpaka leo ni Roga Roga,Espe Bass, Ramatoulaye na Herman Ngassaki. Pia kwa habari zisizoaminika ni kuwa Rapa wao wa zaman Kila Mbongo naye amerudi kundini. Mwaka jana 2013 HermanNgassaki alitoa nyimbo kadhaa kama solo artist lakini bado yupo na kundi hili. Wasiomjua Herman Ngassaki waangalie wimbo Etat-Major mwishoni anavyokata mauno.

Zifuatazo ni Albamu za Extra Musica na nyimbo katika albamu hizo tukianza na albamu ya kwanza mpaka ya mwisho.

v 1995 Album Les Nouveaux Missiles
- Amie reviens (Duller Loemba)
- Chagrin plus plus (Pinochet Thierry)
- Detresse
- Dieu L'eternel (Roga Roga)
- Freddy nelson (Quentin Moyasko)
- Na Ko Bala Yo Na Ko
View attachment 136084
v 1996 Album Confirmation
- Success Extra
- Inondation
- Angela
- Ziya
- Denide
- Etape
- Kende
- Love in love
View attachment 136085

v 1997 Album Ouragan
- Losambo
- Melenge (Roga Roga)
- M'ere S (Duller Loemba
- Panique totale (Quintin Moyascko)
- Reconnaissance (Espe Bass)
- Lolango (Duller Loemba)
- Hommage (Roga roga)
- Generation Mechante (Oxygene)
View attachment 136086

v 1998 Album Etat-Major
- Etat-major
- Raccine (Roga Roga)
- Patience (Kila mbongo)
- Vertige D'amour (Ramatoulaye)
- Villegiature
- Plus tard(Abillisi)
- La plule (Roga Roga)
- Ecart (Dou Dou)
- Cri Du Coeur (Oxygene)
View attachment 136087

v 1999 Album Shalai
- Aministe Shalai
- Matongi
- A vous de voir
- Complainte
- Horizon 2000
- Laissez passer
- Ndzima
- Sissi limperatrice
- Solitude
- Tu me manques(Abillisi)
- Zineba
View attachment 136088
v 2001 Album Trop C’est Trop
- Trop c’est trop
- Gambala
- Zangul Zangul
- Moselekete
- N’julie
- Guivano
- Papato
- Polemique generale
- Probleme sur problem
- 12 Balles
- Zongi Sanga
- Bikisa Nga’ (chez Ntenda)
- Kared Amour
View attachment 136108
v 2004 Album Obligaitore
- Obligaitore
- Honorablement
- Epaka
- Racini II
- Gyrophare
- Aigle Impérial
- Rufin Bouka (Oxygene)
- Radoutable
- Boss chez Trimba
- Foundation Muller
- L’oublier
- Honorablement
View attachment 136109
v 2006 La Main noire
- La main noire
- Racine III
- Rosalain
- 72 minutes de silence
- Mban-Antoine
- Eternite d,amour (Espe Bass)
- Magomboro
- Noces de bois(Roga roga)
- Parfum mondial
- Petit mais costaud
- Mack Serge
View attachment 136110
v 2011 Sorcellerie (Kindoki )
- Sorcellerie
- Kindoki
- La sape
- Le meilleur
- Marriage
- Les gouts et les couleurs
- Congo United
- Brice Anga Golo
- Flo Miokono(Roga roga)
- Jules Maswa
- Gael Bitoma
- Racine IV
- Gaetan Kodia
- Supreme
- Musicien
- Vrai PDG
- Rosalin
View attachment 136111



View attachment 136113View attachment 136114View attachment 136115View attachment 136116View attachment 136117View attachment 136123View attachment 136124View attachment 136125View attachment 136126View attachment 136127View attachment 136128View attachment 136129View attachment 136130View attachment 136132



View attachment 136083
Sehemu ya pili itahusu nini wanafanya Extra Musica International, ZI International, Universal Zangul, Dou Dou Copa na Guy Guy Fall.
More information & Contacts ................Bislisk@yahoo.com
Mkuu inatajwa kuwa kundi la G7(Impressions Des As) lilianzishwa ili kupambana na hawa jamaa, lakini lilishindwa, je madai haya yana ukweli wowote?
Kama utausikiliza wimbo wa G7 uitwao Flueve Du Mal(Impressions Des As Album) utasikia sauti za moja wa watu kama kutoka Extra Musica.
 
Mkuu inatajwa kuwa kundi la G7(Impressions Des As) lilianzishwa ili kupambana na hawa jamaa, lakini lilishindwa, je madai haya yana ukweli wowote?
Kama utausikiliza wimbo wa G7 uitwao Flueve Du Mal(Impressions Des As Album) utasikia sauti za moja wa watu kama kutoka Extra Musica.
G7 hawajawahi kuwa na muimbaji toka Extra Musica, G7 (Impressions Des As) album yao iliitwa Prenez vite !!! yenye nyimbo kama Ca va aller na Fleuve du mall. Ili wapate umaarufu, G7 walitumia muda mwingi kuwashambulia extra musica kwa maneno japo extra walikuwa kimya, hali hii ilifanya kundi hili kupoteza mvuto na kufanya album yao ya pili iitwayo A qui la faute na yatatu kutofanya vizuri sokoni na kupelekea kundi la G7 kupotea. Kumbuka Congo-Brazaville kuna makundi na wanamuziki wengi sana kama Mbuta Likassu, Arlus Mabelee, Alain Konkou, nk
 
G7 hawajawahi kuwa na muimbaji toka Extra Musica, G7 (Impressions Des As) album yao iliitwa Prenez vite !!! yenye nyimbo kama Ca va aller na Fleuve du mall. Ili wapate umaarufu, G7 walitumia muda mwingi kuwashambulia extra musica kwa maneno japo extra walikuwa kimya, hali hii ilifanya kundi hili kupoteza mvuto na kufanya album yao ya pili iitwayo A qui la faute na yatatu kutofanya vizuri sokoni na kupelekea kundi la G7 kupotea. Kumbuka Congo-Brazaville kuna makundi na wanamuziki wengi sana kama Mbuta Likassu, Arlus Mabelee, Alain Konkou, nk
Rogaroga kwema ? kule penye uzi wa tafsiri naona pamepwaya .
 
G7 hawajawahi kuwa na muimbaji toka Extra Musica, G7 (Impressions Des As) album yao iliitwa Prenez vite !!! yenye nyimbo kama Ca va aller na Fleuve du mall. Ili wapate umaarufu, G7 walitumia muda mwingi kuwashambulia extra musica kwa maneno japo extra walikuwa kimya, hali hii ilifanya kundi hili kupoteza mvuto na kufanya album yao ya pili iitwayo A qui la faute na yatatu kutofanya vizuri sokoni na kupelekea kundi la G7 kupotea. Kumbuka Congo-Brazaville kuna makundi na wanamuziki wengi sana kama Mbuta Likassu, Arlus Mabelee, Alain Konkou, nk
Mkuu Rogaroga nakushukuru sana kwa ufafanuzi. Ila G7 album hiyo walijitahidi sana. Fleuve du Mall naupenda sana.

Leo umenitoa matongotongo sikuwa na ufahamu kuwa Alain Konkou, Aurlus Mabele(I hope ni yule wa Loketo Group) Mbuta Likasu ni kutoka Congo Brazzavile! Hivi Tchico Tchikaya,Marehemu Jean Baron wanatoka Congo Kinshasa au Congo Brazzaville?
Taarifa nilizo nazo ni kuwa Aurlus Mabele(Groupe Loketo) alipata stroke, sijui kwa sasa afya yake ikoje maana ni muda mrefu kidogo tangu nisikie hivyo!

Ubarikiwe sana Roga roga.
 
Mkuu Rogaroga nakushukuru sana kwa ufafanuzi. Ila G7 album hiyo walijitahidi sana. Fleuve du Mall naupenda sana.

Leo umenitoa matongotongo sikuwa na ufahamu kuwa Alain Konkou, Aurlus Mabele(I hope ni yule wa Loketo Group) Mbuta Likasu ni kutoka Congo Brazzavile! Hivi Tchico Tchikaya,Marehemu Jean Baron wanatoka Congo Kinshasa au Congo Brazzaville?
Taarifa nilizo nazo ni kuwa Aurlus Mabele(Groupe Loketo) alipata stroke, sijui kwa sasa afya yake ikoje maana ni muda mrefu kidogo tangu nisikie hivyo!

Ubarikiwe sana Roga roga.
Tchico Tchicaya, Ballu Canta, Zitani Nell, Pierre Belcos, Lucien Bokilo hawa wanatoka Brazaville. Kuhusu Arlus Mabelee nalifanyia kazi swala lako.

Ona mfanano huu wa Congo Brazzaville na Congo Kinshasa

Congo Brazaville
Official language: French
Recognised languages: Kikongo, Lingala
Main ethnic groups: Kongo, Sangha, M'Bochi, Teke


Congo Kinshasa

Official language: French
National languages: Kikongo, Lingala, Kingwana (Swahili), Tshiluba
Main ethnic groups: Kongo,Mongo, Luba, Mangbetu-Azande


The two closest capital cities between two sovereign countries are Kinshasa, Democratic Republic of the Congo, and Brazzaville, Republic of the Congo, which are about 1.6 km (0.99 mi) apart, one upstream from the other on different banks of the Congo River (the distance between the middle points is about 10 km)
 
Tchico Tchicaya, Ballu Canta, Zitani Nell, Pierre Belcos, Lucien Bokilo hawa wanatoka Brazaville. Kuhusu Arlus Mabelee nalifanyia kazi swala lako.

Ona mfanano huu wa Congo Brazzaville na Congo Kinshasa

Congo Brazaville
Official language: French
Recognised languages: Kikongo, Lingala
Main ethnic groups: Kongo, Sangha, M'Bochi, Teke


Congo Kinshasa

Official language: French
National languages: Kikongo, Lingala, Kingwana (Swahili), Tshiluba
Main ethnic groups: Kongo,Mongo, Luba, Mangbetu-Azande


The two closest capital cities between two sovereign countries are Kinshasa, Democratic Republic of the Congo, and Brazzaville, Republic of the Congo, which are about 1.6 km (0.99 mi) apart, one upstream from the other on different banks of the Congo River (the distance between the middle points is about 10 km)
Mkuu ahsante sana. Kuna uzi unazungumzia wanamuziki wa Congo, karibu watu wanashusha nondo kule balaa. Tunategemea mchango wako. Watu wamezungumzia Amida Shatur kumsaliti mumewe na kuolewa na Didi Kinuani, na baadae JB mpiana kukubalina kurudiana nae, hadi picha ya mtoto wa Amida aliyezaa na Kinuani ipo tena mtoto kamshika Mpiana
 
Mkuu ahsante sana. Kuna uzi unazungumzia wanamuziki wa Congo, karibu watu wanashusha nondo kule balaa. Tunategemea mchango wako. Watu wamezungumzia Amida Shatur kumsaliti mumewe na kuolewa na Didi Kinuani, na baadae JB mpiana kukubalina kurudiana nae, hadi picha ya mtoto wa Amida aliyezaa na Kinuani ipo tena mtoto kamshika Mpiana
Ngoja niutafute nije na nondo huko
 
Kwa
Kila Mbongo Aliamua Kuacha Muziki na Kujikita Zaidi na Biashara na Kutengeneza Matangazo Nchini Ufaransa na Ubelgiji baada Ya Kundi Zima La Extra Musica BPBL ( Bon Pied Bon Look ) ikimaanisha Wajuao Kuvaa na Wenye Mwonekano Mzuri Lilipogawanyika baada Ya Mvurugano Kati Ya Manguli Wawili Ibambi Ikombi au Wengi Mnamjua Kama Roga Roga La Liberateur na Abilisi ambapo Wakagawanyika na Pakawa na Extra Musica Zangul chini Yake Roga Roga na Extra Musica Internationale chini Yake Abilisi ila hadi Sasa Extra Musica Ya Roga Roga ndiyo Inatamba Sana Kwani Ilibaki na Watu Muhimu Sana ktk Bendi Kama Mpiga Drums Maarufu na Anayetisha Aitwae Ramatoulaye Diabate na Mpiga Solo Akiwa Mwenyewe Gwiji Roga Roga na ktk Mpini wa Bass Akiwa Mwenyewe Espa Bass na Kwa Mliokuwa Mkidhani Kuwa Labda Kuondoka Kwa Kila Mbongo au ( Mazikou Ghislain ) ktk Upande wa Kughani au Kurepu Mlikosea Mno Kwani Alikuja Mtu Mwingine Hatari Kwa Kurepu Aitwae ARAFATE WANYA na Ukitaka Usikie Shughuli Yake Fuatilia Albam Yao Ya Trose Trop Utaijua Habari Yake na Sasa hivi Kimeongezeka Kingine ktk Kurepu Kinaitwa ZAPARRO DEGAIRE ni Hatari Tupu na Wana Album Yao Mpya Iitwayo KINDOKI Ikiimanisha UCHAWI au NDUMBA. Kila la Kheri!
Kwa hiyo mkuu huyu kindoki wa yanga ni ndumba?
 
Nipo naanda story kuhusu Loketo group, keep wait
Ok mkuu,tunasubiri kwa hamu.
Hivi JB Mpiana yuko wapi? Mbona hana nyimbo zinazobamba kama zile za zamani mfano wa zile Album kali za
Titanic,Toujours Humble,Internet. Alipotoa Ant-Terror haikufanya vizuri sana na tangu hapo sijasikia Album nyingine kuzizid hizo 3
 
Ok mkuu,tunasubiri kwa hamu.
Hivi JB Mpiana yuko wapi? Mbona hana nyimbo zinazobamba kama zile za zamani mfano wa zile Album kali za
Titanic,Toujours Humble,Internet. Alipotoa Ant-Terror haikufanya vizuri sana na tangu hapo sijasikia Album nyingine kuzizid hizo 3
Yupo, ana albamu nyingi tu mfano ni Kipé Ya Yo (2007), Quel Est Ton Probleme n.k Tatizo albu hizi kizazi kikubwa cha wenge kama wakina Titina, Aimelia, Alain mpella walikuwa wameshajitoa kwa JB Mpiana na JB kwa kiasi fulani anaangushwa na Serguin Mignon ambaye ndiye drummer wake
 
Nipo naanda story kuhusu Loketo group, keep wait
Mkuu ile nyimbo ya Extra Musica niliokuwa naisema Oxygene ni Cri du coeur (oxygene) ambayo ipo kwenye album ya etat major
Tafazal nitupie kiongozi
Pia hizi zifuatazo
[emoji673] Chagrin plus plus
[emoji673] Amie ravens
[emoji673] Losambo
[emoji673] Na ko bala
 
Back
Top Bottom