Wanajeshi wamenipiga mbele ya mke wangu

Wanajeshi wamenipiga mbele ya mke wangu

bro mwambie wife ulikuwa unawatafutia timing sema boss wao aliwahi kuwatoa! Ila nimecheka sn pole lkn!
 
Ilikuwa juzi kwenye heka heka za kusheherekea pasaka mimi na demu wangu.

Maeneo ya barabara ya chuo kikuu (UDSM) inayoelekea changanyikeni nikawa nimepaki gari pembeni kidogo na barabara siku ipaki pembeni kabisa kiukweli kwa namna fulani nikamuacha demu wangu mi nikaingia sehem (hillpark) kununua vocha pamoja kumtumia mtu hela, nilipo maliza nikawa natoka nje nikakuta lile gari kubwa kabisa la jeshi limesimama nyuma ya gari yangu halafu kuna wanajeshi wawili wapo kwenye gari yangu wanaongea na wife wakimuuliza mwenye gari yupo wapi namimi nikawa natokea akasema huyo hapo... mamamamaaaaaaaa............... kabla hawajaniuliza kitu walinipokea kwa makofi na vibao, walinipiga sana kwa kweli, sikuweza kupigana nao hata kidogo kwasababu kuna wengine walikuwa wametulia tu kwenye gari lao. Mke wangu alishuka kuamulia waniache hawakumpiga lakn walimsukuma akadondokea mkono wa kushoka umeteguka.

Namshukuru sana Mungu, akashuka mwanajeshi mwingine sijui ni boss wao akawaambia waniache ndipo wakaondoka.

Mke wangu amewekewa muhogo mkononi huku mimi naugulia tu maumivu, nimeaibika sana mbele ya mke wangu japo naona aibu lakni najifanya uso mkavu kama ndimu.

kuna mtu humu aliwasifia wanajeshi kwa kumpiga traffic police,nikamwambia subiri siku moja wakupige kisa umewapita au kusimama ghafla mbele yao. ndio haya sasa.

mimi siwafagilii kabisa hawa jamaa wana ubabe wa kijinga sana, sasa hapo ulipopaki siwangekupita tu waendelee na safari yao??au hio ni high way??
 
Pole kwa kipigo swahiba, Kwa hiyo kwenye gari mlikuwa watatu ,wewe,mkeo na demu wako kama sijakosea ???
 
Mkuu ulitaka apewe hii angeweza?
Bado swali litabaki kuwa hiyo ni sahihi kwa kuvunja sheria za barabarani? Makofi kwa mtu mzima yanadhalilisha jamani... Hata hao watoto tumeacha 'kuwazibua' makofi kwa hofu ya kuwatia uziwi...
 
Hahahaaa l do hate them soooooooooooo much... ila samahanini wanajeshi wa humu kwa kutokua mnafiki.

kwa ujinga wao wanachukiwa na wengi. hata mimi nawachukia naona kama hawana kazi ndio wanamalizia hasira za mazoezi yao kwa wananchi. hebu angalia wamemtengua mkono mke wa jamaa sasa amevaa P.OP ni haki hii.....halafu kuna watu humu wanasapoti huu ujinga!
 
au walidhani na ww ni mshabiki wa S2 labda wanata S 3, ndy maana wana hasira,
 
Sometimes uwa najiuliza watu wengine wanafanya makosa au kwa kukusudia au ngoja nifanye kwani watanifanyaje? Mimi kama mimi sioni mtu kama huyo utamsaidiaje ili ajue kuvunja sheria kwa makusudi ni kosa kubwa sana, na kwa ufahamu wangu na niko sahihi asilimia 100 hatakaa tena arudie ilo kosa la kupark barabarani. Kila mara atakapokumbuka kipigo hicho atatafuta wapi panaruhusiwa kupark. Kwa hiyo sometimes nchi hii inahitaji watu kama wanajeshi wawatie adabu watu wote wanaofanya vitu vya hovyo hovyo bila kujua wanaleta madhara kwa wengine

Bado swali litabaki kuwa hiyo ni sahihi kwa kuvunja sheria za barabarani? Makofi kwa mtu mzima yanadhalilisha jamani... Hata hao watoto tumeacha 'kuwazibua' makofi kwa hofu ya kuwatia uziwi...
 
Join Date : 20th April 2014
Posts : 7
Rep Power : 302
Likes Received 2

Likes Given 0



Mkuu naona umetumia busara kuifungulia hii habari id mpya. Hivi ile id yako ya siku zote ndio nani vile????
 
Ilikuwa juzi kwenye heka heka za kusheherekea pasaka mimi na demu wangu.

Maeneo ya barabara ya chuo kikuu (UDSM) inayoelekea changanyikeni nikawa nimepaki gari pembeni kidogo na barabara siku ipaki pembeni kabisa kiukweli kwa namna fulani nikamuacha demu wangu mi nikaingia sehem (hillpark) kununua vocha pamoja kumtumia mtu hela, nilipo maliza nikawa natoka nje nikakuta lile gari kubwa kabisa la jeshi limesimama nyuma ya gari yangu halafu kuna wanajeshi wawili wapo kwenye gari yangu wanaongea na wife wakimuuliza mwenye gari yupo wapi namimi nikawa natokea akasema huyo hapo... mamamamaaaaaaaa............... kabla hawajaniuliza kitu walinipokea kwa makofi na vibao, walinipiga sana kwa kweli, sikuweza kupigana nao hata kidogo kwasababu kuna wengine walikuwa wametulia tu kwenye gari lao. Mke wangu alishuka kuamulia waniache hawakumpiga lakn walimsukuma akadondokea mkono wa kushoka umeteguka.

Namshukuru sana Mungu, akashuka mwanajeshi mwingine sijui ni boss wao akawaambia waniache ndipo wakaondoka.

Mke wangu amewekewa muhogo mkononi huku mimi naugulia tu maumivu, nimeaibika sana mbele ya mke wangu japo naona aibu lakni najifanya uso mkavu kama ndimu.

Umeanza vizuri mistari umekuja kuharibu mwishoni hivi nicheke au nisicheke
 
Hadi hapa wengi wa watoa maoni wamekuwa wakiwaunga mkono wanajeshi kwa kumpiga huyo ndugu. Mi naona kwa hali hii jamii jjetu ina matatizo katika kufahamu taratibu na sheria mbalimbali. hali hii imeenea katika nyanja mbalimbali.

Kingine nikuwa inaonesha wazi jamii yetu inawaogopa sana wanajeshi nakuwaona kama waabudiwa. Sababu tumewapa silaha.

Kuna nchi ambazo silaha ni kitu cha kawaida, huko mwanajeshi akionea raia basi ajue raia watamtandika risasi tu hata kama sio yeye basi watalipiza kwa mjeshi yeyote yule siku ya siku.
 
kichapo ulichopewa hakitoshi...we uliza waliofumwa wakiendekeza michepuko kwa wake za wajeshiiiiiiiii
 
hapo nimeshindwa kidogo kukuelewa, ulikuwa na DEMU wako ama ulikuwa na MKE WAKO. kwa mtazamo wangu demu wako na mke wako na vitu viwili tofauti.

Huyu jamaa apigwe tu! Inawezekana huyo demu anachukuliwa na mmoja wa wajeda hao ndo maana wamempiga!! Mke na Demu haviwezi kuwa sawa hata siku moja!
 
Mara demu wako mara mke wako!
Hebu mwite kwa namna anavyopaswa kuitwa.
 
Sometimes uwa najiuliza watu wengine wanafanya makosa au kwa kukusudia au ngoja nifanye kwani watanifanyaje? Mimi kama mimi sioni mtu kama huyo utamsaidiaje ili ajue kuvunja sheria kwa makusudi ni kosa kubwa sana, na kwa ufahamu wangu na niko sahihi asilimia 100 hatakaa tena arudie ilo kosa la kupark barabarani. Kila mara atakapokumbuka kipigo hicho atatafuta wapi panaruhusiwa kupark. Kwa hiyo sometimes nchi hii inahitaji watu kama wanajeshi wawatie adabu watu wote wanaofanya vitu vya hovyo hovyo bila kujua wanaleta madhara kwa wengine

How would you feel ukiwa umefanyiwa ivi wewe?
How would you feel kitendo hichi akafanyiwa mtoto wako tena kipigo hicho kikampelekea kupata madhara makubwa ya mwili?
 
kaka we ni Dereva wa daladala? wenye tabia za kupaki ovyo huwa ni madereva wa daladala! Hao jamaa wamefanya safi kabisa, wananikera sana watu wanaopaki vibaya.
 
Huyu jamaa apigwe tu! Inawezekana huyo demu anachukuliwa na mmoja wa wajeda hao ndo maana wamempiga!! Mke na Demu haviwezi kuwa sawa hata siku moja!

huo ni ukweli mtupu kiongozi!
 
Back
Top Bottom