Wanajeshi, polisi watwangana risasi

Wanajeshi, polisi watwangana risasi

anachosema Mantombazane kina logic ni mara nyingi TPDF imehusika na ukiukwaji wa sheria na hasa haki za binadam kwa kupigapiga raia bila sababu na kuwashambulia polisi(polisi wa usalama barabarani) rejea tukio la ubungo si mara moja,kwani sisi raia hatuna haraka??walishamtwanga traffic pale,ila kuvamia mitaani na kupiga raia si mara moja mdau lutamyo ni mara nyingi sana,wiki 2 zilizopita hapahapa jamvini iliripotiwa kuwa JWTZ wanajesh wake wamewapiga vijana keko ambao walikuwa wakihisiwa kuiba simu ya sh 25,000/= ajabu sasa huyo aloibiwa wala si mwanajeshi,hawakuishia hapo wanajesh wale waliwanywesha maji machafu wale vijana,uhasama kati ya raia na wanajesh upo sana kama ulivyo kati ya askari wa wanyama pori na wakaz wanaokaa pembezon wa hifadh za taifa.
Wanajesh si malaika usiwasifie kiasi hiko wapo micharuko,wapo wengi sana Mwamunyange alivalie njuga hili,
ila mwisho nasapot POLISI KULAMBISHWA KICHAPO maana nadhan wanajesh wanatimiza kauli ya 'WAPIGWE TU' sikumbuk aloitamka hii kaul

hakuna uhasama wowote kati ya wajeda na raia nimetoka ktk kikos cha jeshi kule arusha nimeona watoto wa kimasai walikuwa wanakuja kula msosi wa jion wala hawaguswi pia 2kitoka nje ya kambi raia wanakuja kuuza vitu tofaut bila hata hofu yoyote ila uhasama mkubwa upo kati ya polisi na wajeda hadi nyimbo zao wanawaponda kinoma polis
 
Last edited by a moderator:
Massai mm nakushauri ni bora ukae kimya...hii mitandao itakupeni shida...hili jina fake lickufanye udhani uko safe xana...records are taken,itc all urs

umemaliza homework?
 
hakuna uhasama wowote kati ya wajeda na raia nimetoka ktk kikos cha jeshi kule arusha nimeona watoto wa kimasai walikuwa wanakuja kula msosi wa jion wala hawaguswi pia 2kitoka nje ya kambi raia wanakuja kuuza vitu tofaut bila hata hofu yoyote ila uhasama mkubwa upo kati ya polisi na wajeda hadi nyimbo zao wanawaponda kinoma polis

Hapa ata mimi nakubali hakuna uhasama kati ya askari jeshi na raia labda kama uhasama basi ni suala la binafsi kati ya mwanajeshi na raia fulani au kuna tatizo limetokea labda ndio ichukuliwe kama uhasama ila ata mimi ninachofahamu kati ya askari jesh na askari polisi dah hapa ni mbinde uhasama nje nje
 
Polisi hawana chochote wanachochangia kwenye utulivu wa nchi hii!! Acha ujinga wewe poilccm.
 
Jameni kazi ya polisi ngumu sana, unakumbana na wabakaji, wezi, wauaji n.k. afu unakutana na wengine wanajifanya wao wapo juu ya sheria, sababu eti mwanajeshi na hawashikiki bila kuzua fujo. Polisi kwetu Kenya huwa wanawashika hata wabunge kwenye madanguro halafu inabidi ipigwe kimya maana afande atapoteza kazi.
 
Askari jeshi c wakolofi kama haujawachokoza tatizo police ni watu ambao kila sheria wanayo wao.
 

Attachments

  • 1412358473592.jpg
    1412358473592.jpg
    9 KB · Views: 573
VURUGU MARA: Wanajeshi 6 JWTZ jioni hii wavamia kituo cha polisi cha Tarime na kuwapiga polisi baada ya mwenzao kukamatwa, RPC Lazaro Mambosasa athibitisha.



CHANZO: Mwananchi

Ni aibu sana kwa jeshi letu la JW…shabaha hawajui ??? risasi zote zile zimeshindwa kumpata hata mmoja
 
Jameni kazi ya polisi ngumu sana, unakumbana na wabakaji, wezi, wauaji n.k. afu unakutana na wengine wanajifanya wao wapo juu ya sheria, sababu eti mwanajeshi na hawashikiki bila kuzua fujo. Polisi kwetu Kenya huwa wanawashika hata wabunge kwenye madanguro halafu inabidi ipigwe kimya maana afande atapoteza kazi.

Mkuu POLISI Wa Tz hawafai, wametunyanyasa sana! Naunga mkono hoja ya jomba anayesema wapigwe tu, tumechoka sisi! Tena sijui kwa nini waliwaacha wanatembea? Walistahili watenguliwe viuno hawa wajinga na madivision 5 yao! Wanabahati wamekutana na vikuruta!!
 
Hahaa makamanda walishindwa kukwepa risasi maana wana mafunzo ya hali ya juu kuliko polisi.???.
 
hakuna uhasama wowote kati ya wajeda na raia nimetoka ktk kikos cha jeshi kule arusha nimeona watoto wa kimasai walikuwa wanakuja kula msosi wa jion wala hawaguswi pia 2kitoka nje ya kambi raia wanakuja kuuza vitu tofaut bila hata hofu yoyote ila uhasama mkubwa upo kati ya polisi na wajeda hadi nyimbo zao wanawaponda kinoma polis
Kwa kua ni kambi hiyo ume-conclude,haya
 
ha ha umeeleza vizuri mwanzoni, ulivyomalizia umenichekesha bure
Mr.Reliable unacheka ila huo ndo ukweli,ingawa Mr. Mangi anapinga,sasa wanajesh wanaenda kupiga raia kweli wapo sawa upstairs hao,au tuambiwe sheria ipi inamruhusu mwanajeshi kuvunja sheria za barabarani,maana mtoa mada amesema walikuwa wame vaa kiraia hawakua na Helmet
 
hakuna uhasama wowote kati ya wajeda na raia nimetoka ktk kikos cha jeshi kule arusha nimeona watoto wa kimasai walikuwa wanakuja kula msosi wa jion wala hawaguswi pia 2kitoka nje ya kambi raia wanakuja kuuza vitu tofaut bila hata hofu yoyote ila uhasama mkubwa upo kati ya polisi na wajeda hadi nyimbo zao wanawaponda kinoma polis

wanajeshi walishawahi kuchoma moto kijiji cha DUKA BOVU Arusha baada ya mwanajeshi mmoja kuporwa mwanamke na raia ..
 
Hivi wewe unakijua unacho kiongea au unashabikia tu, nikuulize swali moja mwanajeshi utampa rushwa katika mazingira yepi, kuna huduma gani ambayo anaitoa kwa mwananchi mmoja mmoja, ambako anaweza kupewa rushwa.swali la pili nitajie nnchi moja hapa duniani amboyo polisi wanapendwa na wananchi wake.
Ulishawahi kwenda jeshi au kumjua mwanajeshi? Unakijua unacho ongea au ushabiki tu? Nikujibu swali lako, hakuna mazingira ya kumpa mwanajeshi hela kwa sababu kwa sasa hakuna huduma anayotoa moja kwa moja kwa mwananchi. Lakini nina imani kutokana na mafunzo na mazingira ya wanajeshi wa chini wakimwagwa katika sekta zote za serikali kusimamia utendaji kazi zitafanyika kwa ufansis maana, hawana ruhusa ya kuwa na benki account binafsi, kiwanja binafsi nakadhalika mpaka baada ya miaka flani kupita. Hivyo chances za wao kuchukua rushwa ni ndogo sana maana watapeleka wapi hio hela wakati kila kitu hupewa na hawana ruhusa ya kuwa na private possessions? Ulishawahi kwenda hospitali za mission? Je ilibidi utoe rushwa kwa ma sister wakusaidie? Unafikiri ni kwanini ukiachana na sababu ya imani?
Sijui una maana gani na swali lako la pili? Nikutajia ncho moja ambayo polisi wanapendwa na wananchi wao? Hehehehe. Kwani hata hapa Tanzania hakuna wananchi wanaopenda polisi? Vipi mkuu uko poa upstairs? Au una maana gani embu fafanua? Kila nchi kuna wananchi wanapenda polisi, asilimia ya hao wananchi wanaopenda polisi ndio hutofautiana. Nchi kama New Zealand, Switzerland, Netherlands e.t.c. hata miji kadhaa nchini Australia polisi huwapa lift watu waliolewa bar ili wasije endesha na kusababisha ajali. Sasa kwa nini wachukiwe.

Natumaini nimekufunua kidogo.
 
JWTZ maranyingi huwa wanapigwa na Police ila maripota wanageuza habari teh teh

Uliangalia habari ya jana ucku ITV?kuna FFU mmoja ana mwili hv alipewa mkono akapepesuka kurudi nyuma akakimbilia kwny gari!Jeshi litabaki kuwa jeshi tu nchi yoyote ile!sema JWTZ cku hz imeingiliwa na siasa na diplomasia imekua nyingi mno!Enzi za kina Gen Musuguri na makamanda wengine wa cku za nyuma icho kituo cha police wangehama!!
 
Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limelaani kitendo cha askari wake wa kikosi cha Nyandoto 27 KJ Makoko ambaye inadaiwa alishindwa kutii maelekezo ya askari polisi wa Usalama Barabarani wilayani Tarime, Mara na kusabisha mapigano baina ya wanajeshi na polisi.

Katika tukio hilo ambalo lilitokea Oktoba Mosi, mwaka huu jioni katika kituo cha mabasi mjini Tarime, raia mmoja na askari kadhaa wa Jeshi la Polisi wakiongozwa na Mkuu wa Upelekezi wa Makosa ya Jinai (RCO) Kanda maalum ya Tarime /Rorya na askari wawili wa JWTZ walijeruhiwa kwa risasi.

Mkuu wa Brigedi 202 kundi la vikosi kanda ya Magharibi, Brigedia Jenerali Mathew Mayela Sukambi, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi, alisema kitendo hicho cha aibu kimefanywa na askari binafsi na siyo JWTZ.

Alisema askari huyo amekiuka kiapo chake, hivyo hastahili kuendelea kuitwa mwanajeshi wa jeshi hilo na kwamba ameagiza sheria na taratibu zichukuliwe dhidi yake pamoja na wote walioshiriki katika tukio hilo.

"Kitendo hicho kimefanywa na askari binafsi na siyo jeshi, taratibu za jeshi zinafundisha na kueleza afisa na askari kuwa mtiifu na mwenye nidhamu na kutakiwa kutii mamlaka na kufuata sheria za nchi kwa mujibu wa katiba," ilieleza sehemu ya tamko hilo la JWTZ.

Alisema kuwa chanzo cha fujo na vurugu hizo zilisabishwa na askari wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani kumkamata askari wa JWTZ kwa kosa la kuendesha pikipiki bila kuvaa kofia ngumu (Helment) na baada ya majibishano askari huyo aliita wenzake walikuwa jirani kwa ajili ya msaada ndipo polisi waliitana kwa wingi na kuanza kutumia nguvu kwa kutumia risasi za moto kuzima vurugu hizo.

Aliwataka maofisa na askari wa jeshi hilo kuzingatia viapo vyao, kutii sheria na taratibu za nchi, mamlaka ya kiraia kwa mujibu wa katiba ya Tanzania huku akiwaonya raia kuacha kushabikia matukio mabaya pindi yanapotokea.
 
Back
Top Bottom