Wanajeshi 88 Washindwa Kumaliza Kozi TMA

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Wanafunzi 88 waliojiunga na Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli (TMA) mkoani Arusha, wameshindwa kumaliza mafunzo kwa sababu mbalimbali ambapo kati yao, 14 wadaiwa kuyakimbia ambapo mhitimu hutunukiwa “Shahada ya Kijeshi.”

Hayo yamebainishwa katika mahafali ya leo Jumamosi Novemba 18, 2023 ambapo maofisa wanafunzi 575, wametunukiwa Kamisheni na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Samia Suluhu Hassan na hivyo kuvishwa vyeo vya Luteni Usu.

Akitoa taarifa ya mafunzo hayo, Mkuu wa chuo hicho, Brigedia Jenerali Jackson Mwaseba amesema kulikuwa na makundi mawili wa wanafunzi ambapo katika kundi la 04/20 la maofisa wa wanafunzi wa shahada ya Sayansi ya Kijeshi, waliojiunga na chuo walikuwa 73 huku 62 ndiyo walifanikiwa kuhitimu.

Chanzo Mwananchi
 
Wanafunzi 88 waliojiunga na Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli (TMA) mkoani Arusha, wameshindwa kumaliza mafunzo kwa sababu mbalimbali ambapo kati yao, 14 wadaiwa kuyakimbia ambapo mhitimu hutunukiwa “Shahada ya Kijeshi...
Vigezo n masharti kuzingatia, wateule wa Mungu huwa ni wachache, hao ndo wateule waliochaguliwa na MUNGU
 
Wanafunzi 88 waliojiunga na Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli (TMA) mkoani Arusha, wameshindwa kumaliza mafunzo kwa sababu mbalimbali ambapo kati yao, 14 wadaiwa kuyakimbia ambapo mhitimu hutunukiwa “Shahada ya Kijeshi.”

Hayo yamebainishwa katika mahafali ya leo Jumamosi Novemba 18, 2023 ambapo maofisa wanafunzi 575, wametunukiwa Kamisheni na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Samia Suluhu Hassan na hivyo kuvishwa vyeo vya Luteni Usu.

Akitoa taarifa ya mafunzo hayo, Mkuu wa chuo hicho, Brigedia Jenerali Jackson Mwaseba amesema kulikuwa na makundi mawili wa wanafunzi ambapo katika kundi la 04/20 la maofisa wa wanafunzi wa shahada ya Sayansi ya Kijeshi, waliojiunga na chuo walikuwa 73 huku 62 ndiyo walifanikiwa kuhitimu.

Chanzo Mwananchi
Wanakimbia maana yake wanaacha kazi au wanatoroka mafunzo wanarudi kazini kwake au inakuwaje hapa?
 
Hao hawakuwa KURUTA,tayari walikuwa ni Waajiriwa wa Jeshi hivyo walichaguliwa kwenda TMA Mafunzoni kutoka MAKAMBINI kwao wanakofanyia kazi kusomea Course Maalum ili Cheo kipande. Sababu ya kutoroka unakuta wengine tayari wanaumwa mfano gauti,wengine mishono,wengine umri umeenda nk,hivyo kukurukakara na mchakamchaka tena wa Mafunzoni inakuwa ngumu kumudu. Wakitoroka maana yake wanarudi kwenye vituo vyao vya kazi na kuendelea kuchapa kazi,kama ni Cheo wanakuwa wamekosa maana wameshindwa kumaliza Mafunzo
 
Hao hawakuwa KURUTA,tayari walikuwa ni Waajiriwa wa Jeshi hivyo walichaguliwa kwenda TMA Mafunzoni kutoka MAKAMBINI kwao wanakofanyia kazi kusomea Course Maalum ili Cheo kipande. Sababu ya kutoroka unakuta wengine tayari wanaumwa mfano gauti,wengine mishono,wengine umri umeenda nk,hivyo kukurukakara na mchakamchaka tena wa Mafunzoni inakuwa ngumu kumudu. Wakitoroka maana yake wanarudi kwenye vituo vyao vya kazi na kuendelea kuchapa kazi,kama ni Cheo wanakuwa wamekosa maana wameshindwa kumaliza Mafunzo
Hahahah makamanda wamechomoa betri😂😂
Halafu wanasema tuna jeshi imara🤣
 
Hahahah makamanda wamechomoa betri
Halafu wanasema tuna jeshi imara
Unakuta Kamanda ameshakuwa na Kitambi chake cha Bia karidhika na Cheo chake,leo umtoe Ngara huko au Mtwara Kituo chake cha Kazi umpeleke Monduli Arusha kwenye baridi uanze kumkimbizakimbiza mchakamchaka ni kutaka kufukua tu maradhi yake kama gauti,kifua nk,lazima asepe zake maana hana cha kupoteza zaidi ya kukosa hiko Cheo tu
 
Back
Top Bottom