Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,997
Badala ya kuandamana kudai ng'ombe atoe maziwa zaidi kwanini wasiandamane kutaka ng'ombe alishwe zaidi ili atoe maziwa zaidi? Au kwanini wasiandamane kupinga maziwa ya ng'ombe kupewa watu wachache zaidi huku wengi wakijitahidi kumlisha ng'ombe huyo?
Wanafunzi wa Vyuo vikuu na wananchi wengine wana haki ya kupinga malipo ya kifisadi ambayo yanafanyika kwa jina la "ubunge"; kwanza siyo tu wakatwe posho na mishahara ya wabunge wote isitishwe kuongezeka kwa miaka miwili ijayo. n.k n.k n.k Au wanafikiri hizo posho na malipo ya wabunge zinatoka wapi kama siyo katika kodi za watoka jasho wa Tanzania?
Wanafunzi wa Vyuo vikuu na wananchi wengine wana haki ya kupinga malipo ya kifisadi ambayo yanafanyika kwa jina la "ubunge"; kwanza siyo tu wakatwe posho na mishahara ya wabunge wote isitishwe kuongezeka kwa miaka miwili ijayo. n.k n.k n.k Au wanafikiri hizo posho na malipo ya wabunge zinatoka wapi kama siyo katika kodi za watoka jasho wa Tanzania?