waliofeli kwani bado wanaendelea kwenda shule?.hao wazomeaji nao hawana akili
Yani.Hapo ndo wanaposhangaa hata hao wanafunzi.
Wanazomewa wakati waliofeli wapo kimyaaa wanakunywa Tangawizi.
(But point yako inanikumbusha mbali sana.
Enzi hizo nasoma(siku hizi nimezeka Si unajua Kigagula)
Basi,
Nilikuwa Na Rafiki angu aitwae Grace(kama jina fake langu hapo juu?
Mimi Na yeye ni marafiki.Lakini kichwani tofauti.
Ilikuwa shule ya kufaulu but Si unajua kuna wale wanaofaulu mpaka wao wanashangaa wamef aulujefaauluje...!
Basi sasa ndo alikuwa huyo Rafiki angu Giresii.
Yeye kuwa wa mwisho sijui wa Pili kwa umwisho ilikuwa kwake kawaida Na hajari kitu.
Baba ake alikuwa tajiri mchimba madini,Binti mrembo.Pesa ipo sasa ajishuhulishe Na masomo ili iweje.
Basi.Shule yetu ilikuwa Na utaratibu siku ya kutangazwa matokeo kwa shule nzima
Nakusanyika wooote.
Wa kwanza mpaka wa 5,Wanatajwa Na Zawadi.
Wa Mwisho karudi nyuma nayo watano.
Cha ajabu jina la rafiki angu lilipotajwa kawa wa mwisho kasoro watu wawili watu walinigeukia mimi Na Kunizomea
Sio keba walikosea hapana(kwa kuwa nilikuwa kiongozi Na najulikana sana sana)
Nilijua wanazomea kama ujumbe why naongozana Na MTU anayefeli ka siku.
But urafiki wetu ulitokea kinature tu.(Automatically)
Sasa nilitegemea baada ha Mimi kuzomewa huyo Grace angenitafuta Na kuniomba msamaha kwa niaba but aliponiona naye Alianza kucheka kucheka sana.
Nikamuuliza kwa nini sasa naye anacheka nikidhania angepata huzuni kama binadamu yeye alicheka tu..
Mpaka Leo huwa najiuliza kama Rafiki angu huyu alijua anachofanya.
Though tunakaa mikoa tofauti sasa but Urafiki wetu haujawai kuisha.
That was Grace !!
Sasa yumkini wanaozomewa wana maana Taarifa zitawafikia Dada zao but in Wrong way.