Wanafunzi Jangwani wanavyozomewa sio sawa

Wanafunzi Jangwani wanavyozomewa sio sawa

Shule hizo za Manzese ujuaji.mwingi,wanafunzi wanajiona wanajua Kila kitu.
Halafu sijui kwanini wanafunzi waliopo kwenye Elimu bure ndo wakorofi mno wakati wale waliopo kwenye shule za bei Mbaya wapo very disciplined kutoka Nyumbani Kwao.Watoto wa Kayumba ni kama wamesuswa tu.
Kwa kweli mwenye nacho ataongezewa
Umaskini wakati mwingine ni kama Dhambi.
 
Sasa Mzazi mpaka mtoto anafeli alikuwa hajui? Ujue mtoto wa kufeli Huwa anaonekana kabisa mwenendo wake.We maksi anakuletea hazieleweki halafu upo kimya.Wanategemea mwisho ndo atafaulu.
Kuna hizi shule za Kata tukienda kwenye vikao vya wazazi shule ina wanafunzi elfu moja kwenye kikao wazazi hata Mia hawafiki
Kweli kuna cha Kufanya kunusuru Elimu Yetu.
Kumbuka Taifa bila Elimu.Haliwezi Endelea
Hata viwanda hivi itakuwa Ndoto
 
Wazazi huwa hawafatilii hayo usemayo.
Kama wazaz wa DSM hujifanya wapo BUSY sana
Yaani Eti wao wazae tu Walimu Ndo wahanfaike Nao.Walimu wenyewe Nao ni wazazi kwa watoto wao..
Muhimu kusaidiana. Ulezi.Wazazi Na walimu
 
Siku zote ufaulu wa mwanafunzi hutegemea jitihada zake mwenyewe, walimu pamoja na jitihada za mzazi, kama mwanafunzi hajawa tayari kufanya vizuri hizo jitihada za mwl.+ wazazi zinakuwa ni kazi bure katika kuleta matokeo chanya.

Kwa level hii (A' level) wazazi wengi wamekuwa wakijisahau kukakazania na kufuatilia maendeleo ya watoto wao wawapo shuleni na hata baada ya kurudi nyumbani, wanawaamini kupitiliza na kuwachukulia wameshakuwa na ufahamu wa kujiongoza na kujiassess wenyewe katika taaluma yao. Mwisho wa siku inafika siku ya mtihani wa mwisho mzazi hajui mwanafunzi amejiandaa vipi katika mitihani yake, matokeo yake ndio haya.

Na kuna wanafunzi wengine hawajitambui pia, pasipo purukushani purukushani za walimu mambo hayaendi, lakini hii pia inawaletea matatizo baadhi ya walimu wa kiume wanaofundisha shule za kike, mwl.akifuatilia sana maendeleo ya mwanafunzi mwisho wa siku wanafunzi huwageuzia kibao kwamba wanawataka kimapenzi (wanafunzi wasiojielewa)...Hivyo walimu pia wanaamua kuacha kuwabugudhi..

Sidhani pia kama kuwahamisha walimu hao ndio suluhisho,...kwamba walimu wote takribani 39 wamechangia ufaulu mbovu wa wanafunzi hao?? Sio kweli.

Wanaowazomea ni kutokujielewa tu, waliofeli wamefeli hivyo wasiwafanye hawa waliobaki hapo jangwani kujiona hawafai na kwamba hawapo sehemu sahihi...Wasiwafanye kutokujiamini.
 
Siku zote ufaulu wa mwanafunzi hutegemea jitihada zake mwenyewe, walimu pamoja na jitihada za mzazi, kama mwanafunzi hajawa tayari kufanya vizuri hizo jitihada za mwl.+ wazazi zinakuwa ni kazi bure katika kuleta matokeo chanya.

Kwa level hii (A' level) wazazi wengi wamekuwa wakijisahau kukakazania na kufuatilia maendeleo ya watoto wao wawapo shuleni na hata baada ya kurudi nyumbani, wanawaamini kupitiliza na kuwachukulia wameshakuwa na ufahamu wa kujiongoza na kujiassess wenyewe katika taaluma yao. Mwisho wa siku inafika siku ya mtihani wa mwisho mzazi hajui mwanafunzi amejiandaa vipi katika mitihani yake, matokeo yake ndio haya.

Na kuna wanafunzi wengine hawajitambui pia, pasipo purukushani purukushani za walimu mambo hayaendi, lakini hii pia inawaletea matatizo baadhi ya walimu wa kiume wanaofundisha shule za kike, mwl.akifuatilia sana maendeleo ya mwanafunzi mwisho wa siku wanafunzi huwageuzia kibao kwamba wanawataka kimapenzi (wanafunzi wasiojielewa)...Hivyo walimu pia wanaamua kuacha kuwabugudhi..

Sidhani pia kama kuwahamisha walimu hao ndio suluhisho,...kwamba walimu wote takribani 39 wamechangia ufaulu mbovu wa wanafunzi hao?? Sio kweli.

Wanaowazomea ni kutokujielewa tu, waliofeli wamefeli hivyo wasiwafanye hawa waliobaki hapo jangwani kujiona hawafai na kwamba hawapo sehemu sahihi...Wasiwafanye kutokujiamini.
Well said my .
 
Back
Top Bottom