Wanafunzi Jangwani wanavyozomewa sio sawa

Wanafunzi Jangwani wanavyozomewa sio sawa

Zamani nilikuwa na tabia kama za Magufuli za kuita/ kuona watu wanaofeli mitihani vilaza.

Lakini Tanzania - not necessarily Jangwani- kuna sababu nyingi sana watu wanafeli.

Kuna watu hawana miwani tu, na hata hawajui kwamba wana matatizo ya macho wanahitaji miwani, wanaona kawaida, kwa sababu vijijini kwao huko watu hawavai miwani sana.

Na hawa (victims wa jamii ambayo kuvaa miwani ni anasa) wakifeli watasemwa vilaza.

Halafu mimi nahoji dhana nzima ya kwamba wanafunzi wa maswekeni huko wakiwa wa mwisho ni poa tu, hakuna anayelalamika, lakini siku wananfunzi wa maswekeni wakilipiza kisasi na kuchukua "nafasi ya Jangwani" ya juu, licha ya kukosa miwani na taa, halafu wanafunzi wa Jangwani wakachukua nafasi ambayo tulitegemea na kutarajia kwamba iwe ni nafasi ya wanafunzi wa maswekeni, hilo liwe ni tatizo la kitaifa linalotakiwa kutungiwa muswada pekee wa kupelekwa Bungeni kwa jina la "Saidia Jangwani Isishuke Daraja la Msimbazi"


Eti isishuke daraja la Msimbazi! 😀

Ingekuwa bora kama hili lingechukuliwa kitaifa na kufikia kwa hao watunga miswaada na kuwekewa kipaumbele badala ya watu kujadili wale watu walioshika nembo ya Taifa.
 
Eti isishuke daraja la Msimbazi! 😀

Ingekuwa bora kama hili lingechukuliwa kitaifa na kufikia kwa hao watunga miswaada na kuwekewa kipaumbele badala ya watu kujadili wale watu walioshika nembo ya Taifa.
Mbona Kantalamba na huko Ntogwimandegegamasangu shule zikishika mkia na watu wakiharibu watu wanaona kawaida tu?

I have nothing against Jangwani. My mom went there back in the days. But still...
 
Aiseee.We Nalendwa.But according to my experience no Teacher can allow such thing.This is false accusation

Lakini pia ni muhimu tatizo liangaliwe kwa kina pande zote mbili na sio kuchukua sheria mikononi na kuwanyanyasa wanafunzi.

Shule za Dar kiuhalisia zitaendelea kufelisha,zikifaulisha Basi itakuwa ni mbinu tu


Teh!, Aiseeh. Inasikitisha.
 
Mbona Kantalamba na huko Ntogwimandegegamasangu shule zikishika mkia na watu wakiharibu watu wanaona kawaida tu?

I have nothing against Jangwani. My mom went there back in the days. But still...


True, kwa kweli. Hizo Kantalamba na Togwi..something you can tell hazipewi umuhimu wowote?!, as if they're not part of Tanzania.

It's Not Fair.
 
Zama hizi siyo zama kama za zamani siku hizi Kila mtu ataubeba msalaba wake mwenyewe.Kama hutaki kusoma unasubiri mwalimu akufosi wakati naye anahangaika na wanawe utafeli tu
Ndo shida ya wanafunzi wa kileo,hawataj kusoma,wanapenda kuvaa uniforms,wanapenda kuitwa wanafunzi.Wanapenda posho wanazopewa nyumbani.
Nna mifano ya watoto wanaoishia mitaani kubeti na kufanya uhuni mwingine.Lakini mwalimu wa leo hawez kuhangaika na mtoto.
Mtoto wa kumuhangaikia ni wa Primary.
 
Nalendwa suala la watoto wa shule kutomiliki simu si kwamba shule haliruhusiwi bali hata wizara hairuhusu.
Hao watoto wakat wana join waliambiwa "Lazima ilikuwa hivyo" kwamba simu haziruhusiwi.
Siamini kama hawajui.
Umemwambia,umemwambia na kumwambia lakini hajali.
Unajua mwalimu anachokifanya?
"Anawapotezea" sasa wao watajiona WAJANJA kumbr ndo wanaangamia.
Ni sawa na mgonjwa wa kisukari,dokta atampa miongozo na masharti lakini mgonjwa mbishi,kila siku anamwambia bado hafati masharti,
Kitakachofata ni athari kwa mgonjwa sio DOKTA.
 
Shule za Dar kiuhalisia zitaendelea kufelisha,zikifaulisha Basi itakuwa ni mbinu tu
Dar shule zinafaulisha.
Ila zinazofaulisha ni za Binafsi.
Rate ya watoto kufeli imekuwa kubwa sana kwa sasa.
Na ni public schools ndiko wanakofeli.
Hata kuwe na mbinu watoto watafeli kwa sababu moja tu HAWASOMI.
Na life styles zao zinawaangamiza.
 
Unaona eeeh??
Janafunzi linamtishia mwalimu Bisibisi.Atafaulia wapi Yarabiii
Nimemsikia mratibu wa elimu kata analalamika amepita maporini amekuta watoto wana sufuria huko maporini wanapika.
Mabegi yanekutwa na BISIBISI,kondomz na lundo la nguo za nyumbani.
Hao ni watoto wa DAR
 
Dar kwani zamani walikuwa hawafundishi,walimu walikuwa wanafundisha tena nadhani Kwa kiwango kinachotakiwa.Shida ni kuwa wanatishwa walimu tu na wanafunzi plus wazazi wanachekelea tu.Ndio maana nimesema Dar wakifaulu itakuwa ni mbinu tu za ufundi zinatumika lakini hii Zima moto haiwezi faulisha .
Huwez fanya mbinu za ufundi kwa mwanafunzi asiyesoma.
Impossible.
 
Shule za Dar watoto wana changamoto nyingi ikiwepo Usafiri.Kuna shule watoto Kila siku wanafika shule saa tatu na wanafika makwao saa kumi na mbili.
Kosa la wale wanaowapangia shule kwenda form I.
Lakini kuna shule kama Manzese,Mugabe na Mburahati watoto wanaosoma hizo shule hawatoki mbali sana na wanapoishi.
Ila ni shule ambazo zina watoto "Vichaa sana" sasa nakushauri fatilia matokeo yao mwakani.

Kingine ni kwamba hizo shule wanafunzi wapo wengi sana.Kuna mwalimu anafundisha wanafunzi 500.
Hivi nwl mwenye load hiyo ataweza toa assignment?
 
Back
Top Bottom