Wanadamu wana mengi ya kujifunza kutoka kwa Mbwa Mwitu!

Wanadamu wana mengi ya kujifunza kutoka kwa Mbwa Mwitu!

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,869
Reaction score
828,403
Wakati wa vita, Mbwa Mwitu wa kike hukaa karibu chini ya wa kiume, kwa utulivu mkuu na usio na hofu.
Anamwamini kabisa na anajua nguvu zake zitawalinda wote wawili.

LAKINI...!
Mbwa mwitu wa kiume wana sheria moja wanayoiheshimu sana ...!
Hawadhuru wanawake kamwe; hivyo mbweha jike yuko salama kando yake.

Hata hivyo hayupo chini ya dume kwa ajili ya kujificha tuu ... Anasaidia pia!

Shingoni ni sehemu dhaifu ya mbwa mwitu, mahali ambapo adui angelenga. Jike anajua hili, na anajifunga shingoni mwake, akimkinga na mwili wake.
Kwa kufanya hivyo, anamlinda kutoka kwa adui na hii ni ishara kwamba hata katikati ya vita, uaminifu na upendo hupewa kipaumbele zaidi kuliko hofu.


FB_IMG_1756634099452.jpg
 
Wakati wa vita, mbwa mwitu wa kike hukaa karibu chini ya wa kiume, kwa utulivu mkuu na usio na hofu.
Anamwamini kabisa na anajua nguvu zake zitawalinda wote wawili.

LAKINI...!
Mbwa mwitu wa kiume wana sheria moja wanayoiheshimu sana ...!
Hawadhuru wanawake kamwe; hivyo mbweha jike yuko salama kando yake.

Hata hivyo hayupo chini ya dume kwa ajili ya kujificha tuu ... Anasaidia pia!

Shingoni ni sehemu dhaifu ya mbwa mwitu, mahali ambapo adui angelenga. Jike anajua hili, na anajifunga shingoni mwake, akimkinga na mwili wake.
Kwa kufanya hivyo, anamlinda kutoka kwa adui na hii ni ishara kwamba hata katikati ya vita, uaminifu na upendo hupewa kipaumbele zaidi kuliko hofu.


View attachment 3460061
Ukuwa unataka Amani ya moyo never be a sympathiser to hide woman....one day ata kutenda utaumia mara mbili.
 
Ni vile tu wanadamu wameamua kuacha kufuata asili ndio maana mambo mengi yanatusumbua.

Ila nawakubali sana mbwa mwitu wa Afrika, wale wanyama wana focus ya hali ya juu wakiwa kwenye harakati zao, na hawana papara wao ukikimbia mbio wao wanakufuata kwa mchaka mchaka hadi utadata mwenyewe. 😂
 
Mawili matatu ya kutia shaka kuhusu hili
1. Ina maana shingo ya jike sio dhaifu? Kwa nini amkinge dume kisha ajiexpose yeye na shingo yame?
2. Kwa muktadha huo, ni nani anayepata kinga hapo? Maana naona dume katulizwa kwa chini huku jike akikenyua meno

Kadhalika mbwa mwitu wako aina tofauti. Kuna wale wa tropical kama fisi. Hao nao wana tabia sawa na hao wa kizungu?
 
Ni vile tu wanadamu wameamua kuacha kufuata asili ndio maana mambo mengi yanatusumbua.

Ila nawakubali sana mbwa mwitu wa Afrika, wale wanyama wana fovus ya hali ya juu wakiwa kwenye harakati zao, na hawana papara wao ukikimbia mbio wao wanakufuata kwa mchaka mchaka hadi utadata mwenyewe. 😂
Na Wako Kundi Hakuna Kuchoka Hiyo.....Ni Mchakaa.. Mchakaaa...Chinjaa...
 
Mawili matatu ya kutia shaka kuhusu hili
1. Ina maana shingo ya jike sio dhaifu? Kwa nini amkinge dume kisha ajiexpose yeye na shingo yame?
2. Kwa muktadha huo, ni nani anayepata kinga hapo? Maana naona dume katulizwa kwa chini huku jike akikenyua meno

Kadhalika mbwa mwitu wako aina tofauti. Kuna wale wa tropical kama fisi. Hao nao wana tabia sawa na hao wa kizungu?
LAKINI...!
Mbwa mwitu wa kiume wana sheria moja wanayoiheshimu sana ...!
Hawadhuru wanawake kamwe; hivyo mbweha jike yuko salama kando yake.

Hata hivyo hayupo chini ya dume kwa ajili ya kujificha tuu ... Anasaidia pia!
 
Ni vile tu wanadamu wameamua kuacha kufuata asili ndio maana mambo mengi yanatusumbua.

Ila nawakubali sana mbwa mwitu wa Afrika, wale wanyama wana fovus ya hali ya juu wakiwa kwenye harakati zao, na hawana papara wao ukikimbia mbio wao wanakufuata kwa mchaka mchaka hadi utadata mwenyewe. 😂
Napenda sana kusikia hadithi za wanyama , mchango wako nimeufurahia na umenifunza kitu kipya bwashee
 
LAKINI...!
Mbwa mwitu wa kiume wana sheria moja wanayoiheshimu sana ...!
Hawadhuru wanawake kamwe; hivyo mbweha jike yuko salama kando yake.

Hata hivyo hayupo chini ya dume kwa ajili ya kujificha tuu ... Anasaidia pia!
Huoni kwamba ni kutokana na silika (insinct) inawaongoza na kama wangekuwa na akili wangewacharaza makucha "wake" zao? Silika iko genetically wired to perform according to rules and NOT otherwise. It is absolute absence of consciousness
 
Na Wako Kundi Hakuna Kuchoka Hiyo.....Ni Mchakaa.. Mchakaaa...Chinjaa...
Na mbaya zaidi wanaenda kwa formation kabisa. Unakuta wapo mbwa hata 9 kwenye kundi ila wanajigawa makundi mawili hapo hapo.

Unakuta waliopo mbele ni kama 5 alafu wengine wanakuja mdogo mdogo zaidi wale wa mbele wakichoka unaona waliokuwa nyuma wanasogea mbele.

Hapo hakuna kuchoka.

Wale mbwa mwitu wa Afrika hawana kiongozi rasmi kwenye kundi ila wana nidhamu na focus ya hali ya juu.
 
Na mbaya zaidi wanaenda kwa formation kabisa. Unakuta wapo mbwa hata 9 kwenye kundi ila wanajigawa makundi mawili hapo hapo.

Unakuta waliopo mbele ni kama 5 alafu wengine wanakuja mdogo mdogo zaidi wale wa mbele wakichoka unaona waliokuwa nyuma wanasogea mbele.

Hapo hakuna kuchoka.

Wale mbwa mwitu wa Afrika hawana kiongozi rasmi kwenye kundi ila wana nidhamu na focus ya hali ya juu.
Na kama kuna wagonjwa huwekwa nyuma
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom