Wana jf nisaidieni elimu ya tanzania imeingia kirusi gani!

kifaransa wanakipata barabara lakini kingereza ni mambumbu ile mbaya.
Sasa huyu muanzisha thread anaona kingereza ndio ishu,angewauliza hao jamaa wako fluent kwa kiswahili au la.
Cha muhimu angalia uwezo wa mtu kufanya kazi,kwani alikuwa anaajiri walimu wa kingereza?

sasa waulize darasani walifundishwa kifaransa na wanaweza kuelezea wanayoyajua kifaransa au wanjing'atang'ata kama hawa wetu apa!
 
Mwalimu hajui kiingereza, anafundisha shule ya kata, chuo cha kata, kiingereza lazima kiwe tatizo. Babu yangu alikua mjeshi wakati wa ukoloni - KARs lakini anapeleka kiingereza hadi nashangaaga....... Anyway, hata hizo shule za akina St. Mary's wanajua kiingereza lkn kichwani hamna kitu.... Acha Tanzania tuendelee kupika bomu litakalolipuka siku yoyote...... Mfumo wetu wa elimu ni uchafu mzima, too politicized......

wewe ni mzalendo mkuu na unaujua ukweli! safi sana
 
kwa nini hujui swahili is becoming the world language.
Angalia Media mbalimbali zinatangaza kiswahili nadhani hata software za computer zimeanza kuwa za kiswahili.wanyarwanda na warundi wanajifunza kiswahili
SHTUKIA!

Safi kabisa mkuu, ila wewe chuoni umefunzwa kwa kiingereza, unataka interview ya kazi ujibu kwa kimatumbi!??
 
Sasa tuchukulie unahokiongelea ni sahihi ok, umeitwa ktk interview na nimekuuliza swali nielezee kitu unachokipenda na unachokifahamu vizuri kabisa ktk waledi wako. Ukashindwa kueleza, sasa mimi nitajua je wewe unazifahamu principles? naomba unielimishe hapo.

Nafahamu hilo swali hata nikikuuliza kwa kiswahili sanifu pia utashindwa kulieza maana utakosa terms za kuunganisha.

kinacholalamikiwa ni kushindwa kujielezea kwa kingereza na sio kuelezea utaalamu walionao.kama wasahiliwa walishindwa kuongea kingereza angewapa wajieleze kwa lugha wanayoiweza ilimradi atambue weledi waliokua nao wangeshindwa hapa ndio tungehitimisha kwamba hawajui kazi.
Kama anataka waongeaji wazuri wa kingereza nadhani tunafahamu pa kuwapata -aende england sio Tz wala Ke.
 
Naanza na wewe kwanza, kanuni za HR nikutunza siri, kwa sababu hr ni kudili na watu wa aina mbalimbali wakiwemo na hao pia. Ndio maana si kila mtu anaweza ku muintavyu mtu, iweje wewe ufanyie watu usaili then utoke uanze kutangazia watu. HR hayuko hivyo wewe mwenyewe uchunguzwe kwanza umepewaje kazi hiyo, Kitu kingine ndio maana ikawekwa intavyuu ili kupima uwezo wa watu na uelewa wao, kwa kitu kile kile ili upate ambae anaelewa zaidi na kutenda pia, wangekua wote wanalingana uelewa na kufam basi kusingekua na haja ya kuwa fanyia usaili, hata waswahili wanasema kwenye safari ya mamba hata kenge wapo, sasa ungejuaje yupi ni bora kama hao wasingekuwepo? acha kua unatoa siri za watu na za ofisi sio poa ili na wewe uwe bora:blabla::blabla:.
 
Ndugu zangu tusiwalaumu waitimu,mfumo wetu wa elimu ndo umetufikisha hapa tulipo

Na hili ndo linalolifanya taifa letu liendelee kuwa na maskini wengi wasio na kazi,wenzetu wachina,warusi n.k wameweza kutumia lugha zao na kuwapima vijana wao kwa kutumia lugha zao,vijana wanajieleza na wanapewa kazi ili kufaidi stadi zao,

sasa kwa vile sisi hatuwezi kujitegemea ndo maana hata lugha yetu haina mchango katika kuonyesha mtu anaelewa nini na anaweza kufanya nini mwishowe wanaachwa wanaendelea kuwa maskini,siamini kama mtu anamaliza chuo akiwa hajuhi kitu,mie nafikiri tungepima yote katka njia tofauti,apewe kazi ademonstrate na pili apimwa uwezo wa kuwasiliana

kazi za kijamii asilimia kubwa iwe kuwasiliana alafu zile physical wapime matendo zaidi kuliko mawasiliano,lakini hata vyuoni kwenyewe fields zimekuwa ni sehemu ya kutengeneza pesa na kufifisha maana halisi ya field,

lakini kuna sehemu ya uzoefu nayo ni lazima izingatiwe,ni wachache wanaokuwa na uwezo wa kumaster yote mwanzoni,ila kadri mda unavyoenda uweza kumshape mhusika,tusiwaache watanzania wenzetu hawa ndo kwanza wanapata exposure,baadae anaweza kumaster na akapafomu wonders
 
Ndugu zangu tusiwalaumu waitimu,mfumo wetu wa elimu ndo umetufikisha hapa tulipo

Na hili ndo linalolifanya taifa letu liendelee kuwa na maskini wengi wasio na kazi,wenzetu wachina,warusi n.k wameweza kutumia lugha zao na kuwapima vijana wao kwa kutumia lugha zao,vijana wanajieleza na wanapewa kazi ili kufaidi stadi zao,

sasa kwa vile sisi hatuwezi kujitegemea ndo maana hata lugha yetu haina mchango katika kuonyesha mtu anaelewa nini na anaweza kufanya nini mwishowe wanaachwa wanaendelea kuwa maskini na kuwa hasara kwa taifa,siamini kama mtu anamaliza chuo akiwa hajuhi kitu,mie nafikiri tungepima yote katka njia tofauti,apewe kazi ademonstrate na pili apimwa uwezo wa kuwasiliana

kazi za kijamii asilimia kubwa iwe kuwasiliana alafu zile physical wapime matendo zaidi kuliko mawasiliano,lakini hata vyuoni kwenyewe fields zimekuwa ni sehemu ya kutengeneza pesa na kufifisha maana halisi ya field,

lakini kuna sehemu ya uzoefu nayo ni lazima izingatiwe,ni wachache wanaokuwa na uwezo wa kumaster yote mwanzoni,ila kadri mda unavyoenda uweza kumshape mhusika,tusiwaache watanzania wenzetu hawa ndo kwanza wanapata exposure,baadae anaweza kumaster na akapafomu wonders
 
Naanza na wewe kwanza, kanuni za HR nikutunza siri, kwa sababu hr ni kudili na watu wa aina mbalimbali wakiwemo na hao pia. Ndio maana si kila mtu anaweza ku muintavyu mtu, iweje wewe ufanyie watu usaili then utoke uanze kutangazia watu. HR hayuko hivyo wewe mwenyewe uchunguzwe kwanza umepewaje kazi hiyo, Kitu kingine ndio maana ikawekwa intavyuu ili kupima uwezo wa watu na uelewa wao, kwa kitu kile kile ili upate ambae anaelewa zaidi na kutenda pia, wangekua wote wanalingana uelewa na kufam basi kusingekua na haja ya kuwa fanyia usaili, hata waswahili wanasema kwenye safari ya mamba hata kenge wapo, sasa ungejuaje yupi ni bora kama hao wasingekuwepo? acha kua unatoa siri za watu na za ofisi sio poa ili na wewe uwe bora:blabla::blabla:.

mkuu sikutaja jina la mtu! au na kama mtu haelewi mada ischangie mimi kwenye original post sikuwalaumu hawa vijana ila nilitoa options kama tatu ili nipate chacho halisi cha haya.
 
kinacholalamikiwa ni kushindwa kujielezea kwa kingereza na sio kuelezea utaalamu walionao.kama wasahiliwa walishindwa kuongea kingereza angewapa wajieleze kwa lugha wanayoiweza ilimradi atambue weledi waliokua nao wangeshindwa hapa ndio tungehitimisha kwamba hawajui kazi.
Kama anataka waongeaji wazuri wa kingereza nadhani tunafahamu pa kuwapata -aende england sio Tz wala Ke.


kaka wenzetu wa kenya hawana ile knowledge tuliyo nayo sisi ila wanajua kujieleza na kama huamini mimi najua kampuni zaidi ya kumi kati ya chache tulizo nazo ma c.e.o wake ni wakenya na mwanzoni anajieleza vizuri akipewa kazi anaanza kusema naomba training nipate japo kauzoef ka mazingira ya kazi kwani sisi tunashindwa ua ni uvivu!
 
mlichokuwa mnaangalia ni uelewa wa hao uliowainterview wa kazi wanayoiombea au ni kiingereza chao na je kiingereza kilikuwa ni moja ya qualification za kuomba kazi katika kampuni yako na je wanaenda kufanya kazi ya kuongea kiingerez aau taaluma yao

Ukweli unabaki pale pale kwamba sisi wa-TZ Kiingereza chetu ni cha kubahatisha. Ila tusiwahukumu huko chuo kikuu, tatizo liko huku kwenye msingi yaani Primary, Sekondari (yaani O-Level na A-Level). Kwa wenzetu kitoto cha primary kinaweza kukutoa jasho, hebu angalia Kenya, Rwanda na Burundi (hawa wawili kwa Kifaransa) wako vizuri.

Kwenye kampuni nyingi Kiingereza ni lazima bwana huwezi kuwekwa pale hata kama una taaluma ya kitu fulani lakini eti Kiingereza huwezi! Sasa ukitembelewa na wageni kutoka nje tuende kuazima tena makarimani? Wewe vipi wewe!!! Hivyo vijana wetu kazi bado wanayo, hata kama kichwani ni wazuri lazima wafanye jitihada na mikakati ya ziada kuweza kujua Kiingereza cha kuongea, vingeinevyo watabaki wasindikizaji na walalamikaji tu, ngoja shirikisho lije bila lugha ya wenzetu mtabaki na vyeti vyenu bila kazi!!

Hata kama una shahada yako kama hakipandi ni veyma ukaenda english course mkuu!! Shauri yenu!!!
 
Kuna njia mbili tu za kuweza kujua kama mtu anaweza fanya kazi fulani; 1. Kumuuliza aeleze ataifanya vipi na 2. Kumpa kazi aifanye. Mara nyingi kwenye usaili tunatumia njia ya kwanza yaani "mtu ajieleze/auze skills zake". Mara zote kwa wahitimu wa elimu ya juu kiingereza hutumika kama lugha ya usaili. Kuna sababu mbalimbali zilizochangia kutumika kwa hii lugha katika usaili.

Kwa kweli ni kama mtu hawezi kujieleza inakuwa ngumu kufanhamu anajua kiasi gani. Bila kujieleza utajuaje kuwa mtu anajua anachokiomba? Mtu amaomba kazi ya ualimu, uhasibu, uhakimu, n.k lazima aeleze kwa maneno jinzi atakavyofanya kazi. Tukumbuke pia kuwa hawa watu wataongea na watu tena toka sehemu mbalimbali duniani. Je akishapata ajira itakuweje? Itakuwa kama yule jamaa yetu moja ambae kamaliza shule na kupata ajira lakini akiona mzungu anakuja ofisini anaaga.

Hii ni "changamoto". Binafsi sioni sababu za kukataa ukweli.Tukubali; kuukubali udhaifu ni kitu muhimu sana katika kutatua tatizo. Tukishaukubali udhaifu wetu tujadili/tuamue tubadilike vipi? Vinginevyo tuendelee kutegemea kazi za deiwaka.
Mkuu hapo umenena jambo, kwani ni lazima tukubali mapungufu tuliyonayo wa tz.
 
mkuu tembelea hapa arusha AICC ukutane na wanyarwanda,wasenegali,wacameroun e t c walivyojazana.hawajui kingereza!

Hao unaowataja walau wanajua lugha nyingine ya Umoja wa Mataifa (Maana huko kuna lugha zinazotambuliwa na kukubaliwa). Hapo sikubaliani na wewe kabisaaaa! Maana hao utakuta ni wazuri kwa Kifaransa, nenda uchunguze utatujuza!!

Maana kwenye UN system unaweza kupata kazi hata kama hujui kiingereza mradi tu unajua ama Kifaransa au Ki-Italiano n.k na siyo Kiswahili peke yake.
 
kifaransa wanakipata barabara lakini kingereza ni mambumbu ile mbaya.
Sasa huyu muanzisha thread anaona kingereza ndio ishu,angewauliza hao jamaa wako fluent kwa kiswahili au la.
Cha muhimu angalia uwezo wa mtu kufanya kazi,kwani alikuwa anaajiri walimu wa kingereza?

Na wewe acha uzezeta hapa!! Mbona unataka kumlazimisha jamaa aajiri watu wasioweza Kiingereza kwenye kazi inayodai kujua Lugha? Ni wa-TZ wanagapi hata kujieleza kwa Kiswahili kwenyewe ni ngoma? Tatizo hapa ni mfumo wetu wa elimu hatujajengewa mazingira ya kujieleza bwana!! Si Sekondari wala Chuo Kikuu, wote hoi!!
 
Kaama dakika ishirini zilizopita nilikuwa naendesha usahili kwa vijana ambao wamemeliza vyuo vikuu amini usiamini kati ya vijana hao kumi walishindwa kabisa kufanya conversation ya kingereza japo kwa dakika mbili.

Baba yangu ameishia la nne lakini anaongea kingereza standard na kinachoeleweka ila vijana hawa wana utasikia its likee..... its like..... yani ...... i mean......what am trying to say is?

Ika yaani anababaika mpaka anatia huruma, ni kwamba siku hizi hawafundishwi kingereza shuleni au ndo mkakati wa kufanya kiswahili lugha ya kimataifa umeanza?

Au basi elimu wanaiacha darasani wanatoka na vyeti?

Tatizo liko wapi jamani?

Au wizara ndo imekosa sera kiasi hiki?

haya sasa,wale wa udsm,sua na mzumbe mnaojiitaga bora.
 
huwezi kuwekwa pale hata kama una taaluma ya kitu fulani lakini eti Kiingereza huwezi! Sasa ukitembelewa na wageni kutoka nje tuende kuazima tena makarimani? Wewe vipi wewe!!!
hopeless kabisa kwa hiyo ulitaka pasiwepo na wakalimani?kwa hiyo ukitembelewa na wachina utalazimisha kuongea kingereza hata kama hamuelewani.
 
Back
Top Bottom