Elpaul
JF-Expert Member
- Jan 19, 2018
- 742
- 470
Mfua vyuma katika ubora wako........Nakuombea na binafsi sina kinyongo nawe kwakuwa tumeishi kwa kuheshimiana mno na kupeana sitara pale palipokuwa na mitazamo tofauti..!
Kila jambo huanzia rohoni bila kujali asili yake.. Tokeo lolote la kimwili asili yake ni rohoni..! Hili jambo utakalo kama una asili nalo BASI LITAKUWA .. Lakini kama ni 'passive' kutokana na jinsi ulivyoeleza hapo basi kuna shida kidogo.. Nachelea kusema unaweza kuangua pua
Natambua unatambua kwa hakika kwa kipindi cha 2015 mpaka sasa ama kwa kujua au kwa kutojua ulijijengea nguvu hasi kubwa sana...lakini haya si sehemu yake sasa kwakuwa umejinyenyekesha, kujishusha kabisa na kuomba radhi... Ambaye hatakusamehe ajitambulishe na kutuonesha ukamilifu wake! Kwenye hili huna mawaa tena ila kuna hiki kitu kinaitwa KARMA!
Sala na maombezi yetu vitakuwa nawe lakini vinaweza kukosa nguvu chanya ya uchaji wa kiroho kulingana na muktadha wake! Kwamba kama ni nafasi ya kisiasa basi baraka nyingi hukumbana na nguvu za kiza
Very interested!!