BwanaSamaki012
Member
- Jan 13, 2023
- 92
- 99
Habari zenu wadau wa JF
nimekuja kwenu na jambo langu naomba kuwashirikisha natumaini kupitia nyie natapa solution. Direct to the point, nimejenga nyumba moja kubwa yenye pande mbili zinazojitegemea upande mmoja ni kwa ajili yangu na upande wa pili nilijenga kwa ajili ya kuweka mpangaji.
Naomba nijikite kwenye upande huu wa kupangisha, upande wa mpangaji unavyumba viwili vyakulala, sebule, dinning, stoo na jiko. Nyumba imefikia 80% ya ujenzi hadi sasa, bado vigae, vioo na rangi. Nimeshindwa kuikamilisha kwa 100% kutokana na changamoto za kiuchumi zinazonikabili kwa kipindi hiki, kiukweli sioni kama naweza kuimaliza kwa vijisenti nilivyobaki navyo kama akiba yangu.
Lengo la andiko hili ni kuomba/kutafuta mtu ambaye anaweza kunisaidia kumalizia kazi hii ya ujenzi kwa makubaliano ya malipo ya baadaye. Kwa mfano, mtu anaweza kunikopesha hela ya kumalizia ujenzi kwa makubaliano ya maandishi, yakuwa anachukua kodi ya nyumba deni hadi pale deni lake litakapomalizika. Au kama kuna mtu anahitaji nyumba ya kuishi tuingie makubaliano anilipe kodi ya mwaka mzima mapema kabla hajaamia nitumie hela (kodi) hiyo kufanya finishing.
Kwa makadilio aliyofanya fundi hela inayohitajika ili kamilisha ujenzi wa nyumba upande wa kupangisha ni Tsh 3,000,000 na makadilio ya kodi ni Tsh 250,000 kwa mwezi. Baadhi ya vitu kama vile cemment, gypsum body, wallput mikada ya maua ya gypsum body ipo na pia umeme na maji pia vipo
Location ni Mwanza, Ilemela jirani na Malaika Beach, sehemu ni nzuri, usalama wakutosha na panafikika kwa urahisi, kiufupi ni rahisi kupata mpangaji kama ikikamilika 100%.
Maoni na ushauli wenu ni muhimu ili niweze kupata njia ya kutoka hapa nilipokwama, pia unaweza kunipigia nikakutumia picha au nikakuelekeza ukaja directly kwenye nyumba tukafanya majadiliano na kufikia makubaliano
+255758779170
nimekuja kwenu na jambo langu naomba kuwashirikisha natumaini kupitia nyie natapa solution. Direct to the point, nimejenga nyumba moja kubwa yenye pande mbili zinazojitegemea upande mmoja ni kwa ajili yangu na upande wa pili nilijenga kwa ajili ya kuweka mpangaji.
Naomba nijikite kwenye upande huu wa kupangisha, upande wa mpangaji unavyumba viwili vyakulala, sebule, dinning, stoo na jiko. Nyumba imefikia 80% ya ujenzi hadi sasa, bado vigae, vioo na rangi. Nimeshindwa kuikamilisha kwa 100% kutokana na changamoto za kiuchumi zinazonikabili kwa kipindi hiki, kiukweli sioni kama naweza kuimaliza kwa vijisenti nilivyobaki navyo kama akiba yangu.
Lengo la andiko hili ni kuomba/kutafuta mtu ambaye anaweza kunisaidia kumalizia kazi hii ya ujenzi kwa makubaliano ya malipo ya baadaye. Kwa mfano, mtu anaweza kunikopesha hela ya kumalizia ujenzi kwa makubaliano ya maandishi, yakuwa anachukua kodi ya nyumba deni hadi pale deni lake litakapomalizika. Au kama kuna mtu anahitaji nyumba ya kuishi tuingie makubaliano anilipe kodi ya mwaka mzima mapema kabla hajaamia nitumie hela (kodi) hiyo kufanya finishing.
Kwa makadilio aliyofanya fundi hela inayohitajika ili kamilisha ujenzi wa nyumba upande wa kupangisha ni Tsh 3,000,000 na makadilio ya kodi ni Tsh 250,000 kwa mwezi. Baadhi ya vitu kama vile cemment, gypsum body, wallput mikada ya maua ya gypsum body ipo na pia umeme na maji pia vipo
Location ni Mwanza, Ilemela jirani na Malaika Beach, sehemu ni nzuri, usalama wakutosha na panafikika kwa urahisi, kiufupi ni rahisi kupata mpangaji kama ikikamilika 100%.
Maoni na ushauli wenu ni muhimu ili niweze kupata njia ya kutoka hapa nilipokwama, pia unaweza kunipigia nikakutumia picha au nikakuelekeza ukaja directly kwenye nyumba tukafanya majadiliano na kufikia makubaliano
+255758779170