Waliotimuliwa UDOM waibuka, watoa ya moyoni

Waliotimuliwa UDOM waibuka, watoa ya moyoni

Wasiwasi wangu ni kwamba inawezekana hili jambo halikujadiliwa hata kwenye Baraza la mawaziri...kama lingepita basi wasingepishana kauli,ndalichako na msemaji wa UDOM wana kauli moja,rais ana kauli nyingine, lingepita kwenye Baraza la mawaziri lazima wangeitisha ufaulu/matokea ya hao vijana,hii ingeuwa hoja kwamba hao vijana ni vilaza,hukohuko kwenye vikao vyao vya ndani, Pili lingefuata suala la milioni 800 wanazodai walimu,hili nalo si kubwa kwa serikali inayojigamba kuwa na makusanyo makubwa,wangebana huku na kule walipe waalim vijana wamalize shule,hizo hela walizobana kwenye semina na safari za nje wanapeleka wapi? Mbona Huduma za afya ziko vilevile?tunachoona ni ukosefu wa uongozi wa pamoja kati ya mawaziri na mwenyekiti wao rais..
Kuna mmoja anawavuruga

Litajadiliwaje na Baraza la Mawaziri! Wakati lilipoletwa Bungeni tu Wabunge ambao wawakilishi wetu lilitupwa nje ya Uwanja na Mbunge mteule wa Rais?

Unategemea Waziri gani mwenye ubavu ataka ethubutu kuanzish a hiyo hoja barazani kwao, hajitaki.
 
Kama serikali iliyipita ilipitisha tena bungeni ukavunja tena bila kupitisha bungeni mtu mzima amekurupuka
Hawataji tena....kila kitu siri,mpaka bunge nalo ni siri kama vile kinachojadiliwa ni ushirikina
 
Nyie watu hamuelewi raisi aliwashangaa wale wanafunzi 400+ waliokuwa wanasoma kwenye vyuo vingine na walikuwa na dv four nakuwaita vilaza. Wale 7000 raisi alisema serikali itapitia upya kujiridhisha na sifa zao ili ione namna ya kuhandle ishu yao.
 
Iparamasa, iko hivi: Washauri wa Rais kwa wakati huu wanamshauri au kumweleza kile anachokihitaji yeye mwenyewe. Kwamba, Rais anakuwa tayari ameshajishauri mwenyewe, kwa hiyo washauri wanapomfuata wanampa kile ambacho amejishauri mwenyewe!
Akili za kuambiwa changanya na zako... Wabongo sio watu wazuri wanaweza kukupeleka chaka mbaya.
 
Kama inawezekana watuwekee majina yote na alama zao ili tuone uongo wa serikali uko wapi au nani yuko sahihi! Ukute walidanganya JPM!
 
Gazeti la Mzalendo la Leo.
Wanavyogeuzageuza maandishi ni dhahiri wanamponya bosi wao ambaye ame likoroga.
JK ndio mjanja, maana yeye kaamua kumruka kuwa haoni tatizo pale Dodoma
 
[QUOTE"delusions, post: 16402963, member: 118909"]Huyo mtoto alireseat akaendelea acheni ushambenga matokeo ya kureseat hamna mnaongea kishiranga kishambenga kikunanku kishombondokoloko kitawaponza[/QUOTE]
WEKa hayo aliorudia
 
Jeska alipelekwa udom kupewa digrii ya rasilimali watu ili akitoka hapo aajiri vilaza, wenye elimu zao waendelee kusota mtaani.
 
K
Nakumbuka Magufuli alisema

'wachina ndio marafiki wa kweli wengine ni wanafiki'

huku tz ikitegemea na kupokea misaada toka US na UK na Kikwete akasema misaada kwa sasa ni muhimu
'wanaopita mwendokasi chomoeni matairi muuze'

alisema hivyo kwa tone ya kusisitiza wala sio ya utani kwenye tv ya taifa na mbele ya balozi wa China

'wanaficha sukari ndio maana inapanda bei, na tutakamata sukari yao tutagawa bure, serikali ya magufuli haishindwi'

mpaka leo hii nyie wote ni mashahidi juu ya hili swala la sukari lilivyo


'sukari inayoagizwa nje ni ya bei nafuu kwa kuwa inakuwa imekwisha expire na haifai kwa matumizi ya binadamu'

huyu mkulu hii kauli hana uhakika nayo, na ni ya kukurupuka pia

'tulishindwa kesi ya samaki kwa kuwa DPP alikuwa amewapunguzia mashitaka'

huku akiwa hana uelewa mzuri juu ya sheria na hakuwa na uhakika walishindwa kwa sababu gani.


' migomo mingine inamalizwa kwa kufukuza tu, nilikuwa nasubiria na wanafunzi wengine wa Dodoma wagome, wangeondoka wote!!'

list ya kauli tata ni nyingi hapa ni chache tu.......

gazeti la Economist liliandika Huyu rais ni mzuri lakini ni mkurupukaji, ikulu ikatoa taarifa rasmi ya kupinga......
Kauli za magu zitatupeleka pabaya
 
Litajadiliwaje na Baraza la Mawaziri! Wakati lilipoletwa Bungeni tu Wabunge ambao wawakilishi wetu lilitupwa nje ya Uwanja na Mbunge mteule wa Rais?

Unategemea Waziri gani mwenye ubavu ataka ethubutu kuanzish a hiyo hoja barazani kwao, hajitaki.
Bashe alisema mawaziri wanamwogopa rais......wanaufyata wanamwacha apate aibu kama hizi labda ataelewa maana ya kuongoza kwa pamoja
 
Huyo mtoto alireseat akaendelea acheni ushambenga matokeo ya kureseat hamna mnaongea kishiranga kishambenga kikunanku kishombondokoloko kitawaponza
Ok kama ali reseat kwa ss alitakiwa kuwa mwaka wa ngap?
 
Nani kawatuma kujitetea??? Je hawajui rais anavyombo vya uchunguzi (TISS) na kuwa hawezi kuongea kitu bila facts?? Nadhani kwa dharau yao hii itabidi wasirudishwe UDOM, na watasambazwa kwenye vyuo vya ualimu, asiyetaka aache. Serikali haiwezi kutumia njia ya mkato.
 
Sasa kipi sahihi hapa ,Alichosema Ndalichako na huyu Afisa wa Udom ama alichosema baba Jesca ???
 
Back
Top Bottom