Majestic wolf
JF-Expert Member
- Feb 10, 2015
- 1,248
- 1,854
Hivi mbona hamuoni probability ya huyo dada kusoma a level kwa mwaka mmoja??
Chengachenga network haikamati vizuri. Nchi nyingine bunge lingemuhoji utendaji wake au hata kumuondoa.Unahitaji saikolojia ya juu kugundua tatizo la ugonjwa wa akili alionao mtu mzima. Kuna mambo yanaendelea naona kabisa huyu mtu hayuko sawa!
Kufeli, ku-reseat, kubadili fani, elimu za kuungaunga, na kozi fupifupi ni changamoto za maendeleo ya kiuchumi, kijamii, kisiasa nchini.Huyo mtoto alireseat akaendelea acheni ushambenga matokeo ya kureseat hamna mnaongea kishiranga kishambenga kikunanku kishombondokoloko kitawaponza
Kwa akili gani aliyonayo mbona o-level miaka minne katoka patupu?Hivi mbona hamuoni probability ya huyo dada kusoma a level kwa mwaka mmoja??
Aliandaa mada ya dakika tano siku tano naona imepigwa na makombora ya Masada marefu -intercontinental ballistic missile,sasa hivi atakuwa anajifuta vumbi na kujikusanyakusanya
![]()
Mwakilishi wa wanafunzi, Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), waliofukuzwa Gibson Johnson akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana. Picha na Beatrice Moses
By Waandishi wetu, Mwananchi mwananchipapers@mwananchi.co.tz
IN SUMMARY
Jana wawakilishi wa wanafunzi hao ambao waliambatana na viongozi wa
Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), walisema wanapinga pia hatua ya kutimuliwa chuoni.
Dar/Dodoma. Sakata Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) limezidi kupanuka baada ya wanafunzi waliorudishwa nyumbani kupinga kuitwa vilaza.
Jana wawakilishi wa wanafunzi hao ambao waliambatana na viongozi wa
Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), walisema wanapinga pia hatua ya kutimuliwa chuoni.
Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake, Gibson Johnson alisema wanasikitika kuona wanavyozushiwa tuhuma mbalimbali kuhusiana na wao kujiunga na chuo hicho.
Alisema wamekuwa wakijiuliza sababu za Serikali zinazotaka kuhalalisha kutimuliwa kwao chuoni kuwa hawakuwa na sifa, jambo ambalo si la kweli.
“Siyo kweli kwamba sisi ni vilaza (wanafunzi wasiofanya vizuri darasani) na waliofeli na kupata daraja sifuri.
“Sisi ni wanafunzi tuliofaulu kwa viwango vilivyohitajika kwa daraja la kwanza hadi la tatu na tulipangiwa shule za kuendelea na masomo ya kidato cha tano na sita, lakini tulibadili na kuamua kujiunga Udom, hivyo tunaomba Serikali itumie busara zake.
“Hatuwezi kwenda kusoma kidato cha tano na sita kwa kuwa tumepoteza muda wetu.”
Alisema wanamshauri Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako na Rais John Magufuli kutumia busara kuwarudisha chuoni kumalizia masomo yao.
Katibu Mkuu wa TSNP, Alphonce Lusako aliitaka Serikali ichukukue hatua kwa waliohusika kudahili wanafunzi wasio na vigezo na kuwawajibisha.
“Lakini pia wanafunzi wafidiwe fedha na muda waliopoteza kwa wakati wote waliokuwa chuoni, kama hawatapewa haki zao, sisi tutashirikiana na wadau wa elimu zikiwamo asasi za utetezi wa kisheria kutafuta haki mahakama,” alisema Lusako.
Udom yazungumza
Ofisa uhusiano wa Udom, Beatrice Baltazali alisema wanafunzi hao wote walifaulu vizuri wakiwa na daraja la kwanza, pili na wachache daraja la tatu.
“Wanafunzi wote walikuwa na nafasi ya kwenda kidato cha tano, lakini kwa kuwa waliahidiwa ajira, waliona wapitie huku kwa kuwa watapata ajira ya moja kwa moja,” alisema.
Beatrice alisema walimu wa Udom walikuwa wanalipwa fedha za ziada kuwafundisha wanafunzi wa programu hiyo kwa kuwa walikuwa wanatumia muda mwingi zaidi ya kiwango walichokuwa wamepangiwa.
“Kutokana na madai ya malipo hayo, mkaguzi wa ndani aligundua kuna tatizo, ndiyo walimu nao wakaamua kugoma, wanafunzi wakawa hawafundishwi Serikali ikaamua warudishwe nyumbani,” alisema Beatrice.
My take; mh raisi tuelewe lipi na aliangalia wapi mpaka ukajilizisha hawa wanafunzi kufukuzwa ndani ya masaa 24?
Wameanza kufulia madeni ya nyuma yameisha.Siku hizi unasikia wakitaja makusanyo ya ndani kwa mbwembwe kama walivyoanza?
![]()
Mwakilishi wa wanafunzi, Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), waliofukuzwa Gibson Johnson akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana. Picha na Beatrice Moses
By Waandishi wetu, Mwananchi mwananchipapers@mwananchi.co.tz
IN SUMMARY
Jana wawakilishi wa wanafunzi hao ambao waliambatana na viongozi wa
Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), walisema wanapinga pia hatua ya kutimuliwa chuoni.
Dar/Dodoma. Sakata Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) limezidi kupanuka baada ya wanafunzi waliorudishwa nyumbani kupinga kuitwa vilaza.
Jana wawakilishi wa wanafunzi hao ambao waliambatana na viongozi wa
Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), walisema wanapinga pia hatua ya kutimuliwa chuoni.
Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake, Gibson Johnson alisema wanasikitika kuona wanavyozushiwa tuhuma mbalimbali kuhusiana na wao kujiunga na chuo hicho.
Alisema wamekuwa wakijiuliza sababu za Serikali zinazotaka kuhalalisha kutimuliwa kwao chuoni kuwa hawakuwa na sifa, jambo ambalo si la kweli.
“Siyo kweli kwamba sisi ni vilaza (wanafunzi wasiofanya vizuri darasani) na waliofeli na kupata daraja sifuri.
“Sisi ni wanafunzi tuliofaulu kwa viwango vilivyohitajika kwa daraja la kwanza hadi la tatu na tulipangiwa shule za kuendelea na masomo ya kidato cha tano na sita, lakini tulibadili na kuamua kujiunga Udom, hivyo tunaomba Serikali itumie busara zake.
“Hatuwezi kwenda kusoma kidato cha tano na sita kwa kuwa tumepoteza muda wetu.”
Alisema wanamshauri Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako na Rais John Magufuli kutumia busara kuwarudisha chuoni kumalizia masomo yao.
Katibu Mkuu wa TSNP, Alphonce Lusako aliitaka Serikali ichukukue hatua kwa waliohusika kudahili wanafunzi wasio na vigezo na kuwawajibisha.
“Lakini pia wanafunzi wafidiwe fedha na muda waliopoteza kwa wakati wote waliokuwa chuoni, kama hawatapewa haki zao, sisi tutashirikiana na wadau wa elimu zikiwamo asasi za utetezi wa kisheria kutafuta haki mahakama,” alisema Lusako.
Udom yazungumza
Ofisa uhusiano wa Udom, Beatrice Baltazali alisema wanafunzi hao wote walifaulu vizuri wakiwa na daraja la kwanza, pili na wachache daraja la tatu.
“Wanafunzi wote walikuwa na nafasi ya kwenda kidato cha tano, lakini kwa kuwa waliahidiwa ajira, waliona wapitie huku kwa kuwa watapata ajira ya moja kwa moja,” alisema.
Beatrice alisema walimu wa Udom walikuwa wanalipwa fedha za ziada kuwafundisha wanafunzi wa programu hiyo kwa kuwa walikuwa wanatumia muda mwingi zaidi ya kiwango walichokuwa wamepangiwa.
“Kutokana na madai ya malipo hayo, mkaguzi wa ndani aligundua kuna tatizo, ndiyo walimu nao wakaamua kugoma, wanafunzi wakawa hawafundishwi Serikali ikaamua warudishwe nyumbani,” alisema Beatrice.
My take; mh raisi tuelewe lipi na aliangalia wapi mpaka ukajilizisha hawa wanafunzi kufukuzwa ndani ya masaa 24?
Iparamasa, iko hivi: Washauri wa Rais kwa wakati huu wanamshauri au kumweleza kile anachokihitaji yeye mwenyewe. Kwamba, Rais anakuwa tayari ameshajishauri mwenyewe, kwa hiyo washauri wanapomfuata wanampa kile ambacho amejishauri mwenyewe!Sasa kama msemaji wa UDOM anasema hao walioitwa vilaza walikuwa na ufaulu wa division one,two,na wachache three,mh rais atawaambia nini watanzania anapodai walikuwa na division four? Hii si ushahidi kwamba rais hapati taarifa sahihi na mwisho wa siku anafanya maamuzi ya kuumiza watu? Ni nani alimpelekea rais taarifa hizo? Mbona UDOM kupitia msemaji wao na bi ndalichako kauli zao zinafanana? Za rais zinatoka wapi na ni naani mpasha habari wake? Wangapi wameshaumia kwa staili hii tangu aingie madarakani? Hawa watoto wakienda mahakamani watashinda kwa hakika,serikali itachukua kodi za nani kuwalipa fidia? Hiyo fidia na kuwaacha waendelee kusoma kipi cha busara?
Ndio ninyi mnaoongozwa na methali/misemo ya samaki moja akioza, Wote wameoza. Badala ya kukaa chini ukafanya uchunguzi wa yupi kaoza na yupi hajaoza. Mwisho wa siku unaona ni bora uingie hasara isiyo na tija kwa ufinyu wa fikra. Haya mawazo ungempa mapema waziri husika/ Rais wake kabla ya maamuzi yao, na si kumpa msemaji wa chuo muda huu tayari "samaki wameisha mwangwa" woteHuyo msemaji wa udom nae anatuchanganya.anawezaje kusema kuwa wanafunzi walofukuzwa wana ufaulu mzuri wa grade 1,2and 3.!!! inamaana hajui kama jesca John yupo UDOM?
km jesca amedahiliwa UDOM,uwezekano wa kwepo kwa wanafunzi wa aina yake upo.cha msingi UDOM waweke file zima la wanafunzi hao tuone matokeo yao.
Huyu naye......Tatizo mnaongea sanaaaaa ila maamuzi ya Magufuli hayarudi nyuma
Haiwezekani serikali ibebe mzigo wakati wangeweza enda soka A level
Wewe na jesca hamna utofauti na wote vilazaHuyo mtoto alireseat akaendelea acheni ushambenga matokeo ya kureseat hamna mnaongea kishiranga kishambenga kikunanku kishombondokoloko kitawaponza
Sasa kama msemaji wa UDOM anasema hao walioitwa vilaza walikuwa na ufaulu wa division one,two,na wachache three,mh rais atawaambia nini watanzania anapodai walikuwa na division four? Hii si ushahidi kwamba rais hapati taarifa sahihi na mwisho wa siku anafanya maamuzi ya kuumiza watu? Ni nani alimpelekea rais taarifa hizo? Mbona UDOM kupitia msemaji wao na bi ndalichako kauli zao zinafanana? Za rais zinatoka wapi na ni naani mpasha habari wake? Wangapi wameshaumia kwa staili hii tangu aingie madarakani? Hawa watoto wakienda mahakamani watashinda kwa hakika,serikali itachukua kodi za nani kuwalipa fidia? Hiyo fidia na kuwaacha waendelee kusoma kipi cha busara?
Mkuu jamaa huwa hana tofauti na "boss wake". Amebaki "tishu" siku hizi.