Waliotimuliwa UDOM waibuka, watoa ya moyoni

Waliotimuliwa UDOM waibuka, watoa ya moyoni

Wasiwasi wangu ni kwamba inawezekana hili jambo halikujadiliwa hata kwenye Baraza la mawaziri...kama lingepita basi wasingepishana kauli,ndalichako na msemaji wa UDOM wana kauli moja,rais ana kauli nyingine, lingepita kwenye Baraza la mawaziri lazima wangeitisha ufaulu/matokea ya hao vijana,hii ingeuwa hoja kwamba hao vijana ni vilaza,hukohuko kwenye vikao vyao vya ndani, Pili lingefuata suala la milioni 800 wanazodai walimu,hili nalo si kubwa kwa serikali inayojigamba kuwa na makusanyo makubwa,wangebana huku na kule walipe waalim vijana wamalize shule,hizo hela walizobana kwenye semina na safari za nje wanapeleka wapi? Mbona Huduma za afya ziko vilevile?tunachoona ni ukosefu wa uongozi wa pamoja kati ya mawaziri na mwenyekiti wao rais..
Kuna mmoja anawavuruga
Siku hizi unasikia wakitaja makusanyo ya ndani kwa mbwembwe kama walivyoanza?
 
Huyo mtoto alireseat akaendelea acheni ushambenga matokeo ya kureseat hamna mnaongea kishiranga kishambenga kikunanku kishombondokoloko kitawaponza
Mbona umeandika utumbo? ali reset wapi? na kwanini alidahiliwa na NACTE na sio TCU kama alireset?
 
Tatizo mnaongea sanaaaaa ila maamuzi ya Magufuli hayarudi nyuma
Haiwezekani serikali ibebe mzigo wakati wangeweza enda soka A level
 
Tanzania Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wangu wote.... Nadhani tutaingia kwenye kitabu cha kumbu kumbu cha Dunia. Wasi Wasi wangu kuna siku jamaa atadanganywa kuwa Ziwa Tanganyika limeibwa na yeye atakurupuka na kuagiza lirudishwe kwa nguvu zote Hahahaha
 
Kama hii kauli ya mtu wa ndani wa UDOM ni kweli basi hii serikali imetokota. Na utakuwa ni ukurupukaji wa hali ya juu!
 
JPM wangu weeee kalishwa kasa! Kama kweli hakuna Kilaza.....ni hatari kwa nchi kumdanganya President! Isije kutokea kumbe Kilaza ni Jesca pekee alieko UDOM! Naendelea kula pop corn movie ikiendelea!! Aje aombe radhi kwa lugha ya kuudhi!
Picha linaendelea, season 1, episode 8
 
Wale watoto wa watu wanapakaziwa kwamba waligoma wakati waliogoma ni waalimu wao. Baba Jesca alitaka kufukuza Wanafunzi wa UDOM anajisahaulisha kwamba pale pale alipokuwa kuna wanafunzi walikuwa wamegoma na hakupenda kukemea wala kuchukua hatua yeyote yeye pamoja na Joyce wake, mbona wanakuwa na "Double Standards"!?.
Kama baba Jesca kashindwa kutofautisha Division one two three na four na kuzichanganya na kuziita vilaza,pia kashindwa kutofautisha diploma na degree kisha kuwatimua Udom na kusahau kuwa wakati huo huo mwanae Jesca Division 4.30 yupo pale anasoma degree huku nae ni Kilaza, Je ataweza kweli kulielewa hili neno "Double Standard"? Si unamchanganya tu mkuu.
 
Siku hizi unasikia wakitaja makusanyo ya ndani kwa mbwembwe kama walivyoanza?

Kwa hizo kontena kumi zinazokuja kwa mwezi!!!!!! Tena siku hizi ndani ya siku tatu unapata kontena lako maana kazi Hakuna.

Usisahau kuwa roba za mbao zitaongezeka hasa ukichukulia namna ya wamiliki wa malori wanavyohamisha malori yao kutoka "NNJII HII" hivyo madereva wa hayo malori wameanza kukosa ajira
 
Kwenye hili sakata la Dart mfalme yuko uchi!
Wana propaganda magogoni inabidi wabuni propaganda ya kuhamisha upepo huku hili jambo likishughulikiwa fasta.
 
Tatizo mnaongea sanaaaaa ila maamuzi ya Magufuli hayarudi nyuma
Haiwezekani serikali ibebe mzigo wakati wangeweza enda soka A level
Serikali ndio ilianzisha hiyo kozi....ikawapa ufadhili mia kwa mia....na hili lilianzia kwenye Baraza la mawaziri la kikwete ambako magufuli naye ,akiwa waziri alikuwa ni mjumbe wa Baraza la mawaziri,wakalipitisha wakijua hizo shule za A-level zipo,kwa nini asingejiuzuru kama alikuwa anapingana?
Wao wanafunzi wakienda mahakamani wakashinda utamsikia analalamika mahakama zinamuonea na kwamba waendesha mashitaka wanashirikiana na upande wa Pili...kesi kama hii mwanasheria wa serikali Mwenye akili anawaambia mabosi wake wakae chini wajadili kumaliza kesi nje ya mahakama-fidia
 
Huyo msemaji wa udom nae anatuchanganya.anawezaje kusema kuwa wanafunzi walofukuzwa wana ufaulu mzuri wa grade 1,2and 3.!!! inamaana hajui kama jesca John yupo UDOM?
km jesca amedahiliwa UDOM,uwezekano wa kwepo kwa wanafunzi wa aina yake upo.cha msingi UDOM waweke file zima la wanafunzi hao tuone matokeo yao.
 
Back
Top Bottom