Waliokufa wamekwenda wapi??

Waliokufa wamekwenda wapi??

Yes!!! huyu ndiye aliye kufa na kufufuka, na sasa kila anayemwamini HATAKUFA bali ataishi milele!!!
Asante nimekuelewa ila mimi nilikuwa namaanisha kuwa hakuna Binadamu mwenzetu aliyefariki akafufuka akaja kutuelezea kinachoendela baada ya kifo.
 
Ukilala ndiyo kufa kwenyewe.Ukiamka ndiyo uhai.Kwa kifupi kufa ni kulala usingizi fofofo milele,ni pumziko la milele,ndiyo maana kuna watu wakichoka wanajipumzisha kwa kujinyonga au kunywa sumu.
 
Unaponunua tv na kuitoa ndani ya box huwa tv inaenda wapi?.
 
Kuna waliofukiwa ardhini, waliotupwa majini, walio.liwa na wanyama, waliochomwa moto, waliosagwa kwa tindikali, hivyo yaani
 
Kisayansi, tunajua mwili hufa na shughuli za ubongo hukoma, lakini hatuna ushahidi wa kuthibitisha fahamu huenda wapi baada ya hapo. Dini zina majibu yao kama Pepo, Moto au ulimwengu wa baada ya kifo lakini hayo ni masuala ya imani, si jambo lililothibitishwa kisayansi.

Kwa hiyo ukiuliza “kwa uhakika wamekwenda wapi?” hakuna mwanadamu anayejua.
 
Hakuna walipokwenda, the moment wanakufa ndo inakuwa mwisho wao, hakuna kinachoendelea, utambuzi wao, maarifa yao, na Kila kitu kinaishia hapo, kinachofuata ni kuzikwa and then decomposition inachukua nafasi na kinachofuata ni all element kurudi kwenye udongo na kurutubisha mengine, kiufupi hakuna tena maisha baada ya Kifo, inakuwa kama vile kipindi hujazaliwa, hukuwepo na Wala haikukuumiza Wala kukushughulisha, na ndiyo hivyo baada ya kufa, inakuwa ndo mwisho wa uwepo wako, hakuna mbingu Wala moto wa milele, it's just the end of you, the end of your existence
Agiza kitimoto kilo saba nakuja kulipa mkuu
 
Hakuna maisha baada ya kifo , ukifa umemaliza yote yakupasayo kwahiyo asitokee mtu akakudanganya etii kuna sehemu wanakwenda , hakuna bali wanaoza nakubakia mifupa mitupu.
Ukweli huu hapa ambao watu hawataki kuusikia
 
“Kwa sababu ya imani yenu ndogo. Ninawaambia kweli, mkiwa na imani ndogo kama punje ya haradali, mtauambia mlima huu, ‘Ondoka hapa uende pale,’ nao utaondoka”
Nani amewahi kubeba zege Kwa Imani? Au Dunia nzima hakuna mwenye Imani kiasi Cha kuhamisha mlima?
 
Hakuna walipokwenda, the moment wanakufa ndo inakuwa mwisho wao, hakuna kinachoendelea, utambuzi wao, maarifa yao, na Kila kitu kinaishia hapo, kinachofuata ni kuzikwa and then decomposition inachukua nafasi na kinachofuata ni all element kurudi kwenye udongo na kurutubisha mengine, kiufupi hakuna tena maisha baada ya Kifo, inakuwa kama vile kipindi hujazaliwa, hukuwepo na Wala haikukuumiza Wala kukushughulisha, na ndiyo hivyo baada ya kufa, inakuwa ndo mwisho wa uwepo wako, hakuna mbingu Wala moto wa milele, it's just the end of you, the end of your existence
Jibu sahihi utalipata siku ukifa.
 
Jambo likishakuwa la kiroho basi mpaka hapo ugaigai umeanza, hakuna Cha maana tena
Inakuwa ni ngumu kuthibitisha inakuwa tu ni faith, na kitu kikiwa kwenye angle ya faith ni ngumu kuwa proved inabaki kuwa assumption
 
Jibu sahihi utalipata siku ukifa.
Hakika. Ijapokuwa embu fikiria huu mfano mdogo ukiwa umelala in a dreamless night, assume umelala saa 4 usiku ukashtuka saa 11 alfajiri, unakuwa hujui what happens hapa katikati kuanzia saa 5 hadi saa 10, sasa usingizi ni kama nusu ya Kifo tu , so ina make sense kusema ukifa inakuwa ni eternal sleep without any thoughts, imagination or any feeling..

Just think about it
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom