You made my day.... Watu hawashangai watu wanakimbia site wanaacha magofu...kuna wale hawajawahi kununua hata mfuko wa cement ndio wanaosema ujenzi rahisi. Hata kama una kipato kizuri ujenzi ni gharama. Usione wenye nyumba wanatoa lugha ngumu mnapobamiza milango they know its price.
inatagemea na location na materials used, unaweza kujenga kwa tofali za kuchoma ukatumia mbao za bei nafuu kuezeka na madirisha ya bei nafuu pia. ila ujenzi ni finishing na hapo ndio kazi ilipomi nimejenga chumba na sebule kila kitu.. basic finishing.. no tiles.. kwa 5m tu... ila kuna uzi humu watu walikuwa wanasema milion 10.. nikakata tamaa..
nilivyokaza roho na kuanza ujenz hadi nimeamia
Achaneni na immitation, mm nilianza na kazi ya kawaida kabisa early 2005 nikanunua uwanja. Ujenzi unauma! Uchungu! Hela yote inaishia kwenye nyumba hasa pale mafundi wamefikia kwenye finishing uko radhi hata usinywe soda.! Ilifika kipindi nikataka kuuza baada ya kuona saving inakuwa ndogo kila mwezi.. All in all jitose! Never give up! Kadri unavyojitavidi the more the trouble knocking on to you! JikakamueNadhani sentensi yako ya mwisho ndo ushauri unaotufaa wote humu.
Wengi tunajenga kwa kuangalia Fulani kajenga vipi. Cha muhimu jipange mapema. Fanya utafiti wa kutosha. Omba ushauri wa kitaalam. NA tumia mali ghafi ambazo una uwezo nazo. Mwisho wa siku nyumba ni finishing. The quality of your finishing determines resources required.
Ukiwa na kiwanja, gharama ya nyumba ya vyumba vitatu, kwa basic finishing ni around 20M. With the same house some one will mention kuwa ametumia milioni mia! Utadhani kajengea mchanga wa makinikia.
mmmmh! hayo madirisha ya wavu ikija mvua ya upepo ni shughuli pevu. Ni bora hata kama ukashindwa yote lakini uweke vioo dirishani. Naamanisha hata chini uweke jamvi tu, hata ukose plasta/ripu, gipsam na mengineyo lakini madirisha kuwekewa vioo ni muhimu sanaKama basic finishing ni floor ya cement tu na madirisha ya wavu labda.
Mungu akutangulie ndoto yako na dhamira yako itimie, inshallah!!dahhh!! nikiona hayo mamilioni mnayosema eti ndo gharama ya chini navurugwa tumbo, ama hakika ujenzi noma, ila kufikia mwaka 2020 lazima niwe kwenye mjengo wangu mzuuuri!!
AmeenMungu akutangulie ndoto yako na dhamira yako itimie, inshallah!!
Hongera mkuu. Kapicha tafadhali.mi nimejenga chumba na sebule kila kitu.. basic finishing.. no tiles.. kwa 5m tu... ila kuna uzi humu watu walikuwa wanasema milion 10.. nikakata tamaa..
nilivyokaza roho na kuanza ujenz hadi nimeamia
Ujenzi rahisi kivipi? Fafanua.Ujenzi rahisi sana ..sema waliojenga hupenda kutisha watu
Hongera mkuu. Kapicha tafadhali.
Usihofu.kapicha kikitumwa naomba uni tagi, plisi spinderalla
Upo sahihi sana, ila ujenzi hauna ghalama maalum. Kwa mfano kuna mtu anaweza kujenga nyumba kwa Milioni 70 na mwingine akajenga nyumba hiyo hiyo na kwa ramani hiyo hiyo kwa M100. Tofauti kubwa hapo ni nyumba unaijenga wapi na unafanyia finnishing vifaa gani na vya bei ganiNimejaribu kufuatilia kauli za waliojenga nyumba. Huwa wanapenda kuwaogopesha waliopanga kuwa ujenzi ni gharama.
Huwezi kutana na mtu akakutia moyo hata kidogo. Lengo la wengi waliojenga ni ku play god. Yani wanapenda waheshimike na kujionesha kuwa wana mawe marefu.
Mimi ninapopiga gharama za ujenzi, napata gharama za chini kama ambavyo Magufuli alifanya kwenye ujenzi wa hostel za UD. Tukienda kwa stail yake, mbona kila mtu atakuwa na ka mjengo!
Safi mkuu umekuwa objective.Ndio nyie tunaowazungumzia.
Nyumba ya mabati sabini kwa elfu kumi na tano bati moja ni milioni moja hiyo.
Mbao za milioni na nusu zinatosha kupaua.
Matofali elfu mbili na mia tano ni milioni tatu hiyo, cement ya kujengea mifuko mia ni sh milioni moja hiyo.. Fundi wa kujenga na kupaua, milioni nne hiyo.. Hizo gharama unazozungumza, unajenga shule?