Bila kuwa na kibali cha ujenzi ni marufuku kufanya ukarabati wowote wa nyumba yako jiji la Ilala na viunga vyake

Wamuyaya

Member
Apr 4, 2021
72
68
Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni!

Sikuamini machoni mwangu pale nilipowaona mafundi waliokuwa wakiendelea na ukarabati (kupiga plaster) nyumba ya jirani yangu maeneo ya Tabata, wakiambiwa na mtendaji wa mtaa kuwa hawaruhusiwi kuendelea na kazi ya ujenzi huo hadi pale boss wao atakapoenda kuomba na kulipia kibali cha kufanya ukarabati wa nyumba yake.

Cha kushangaza ni kwamba huyo jirani yangu alihamia Kwenye hiyo nyumba zaidi ya miaka 5 iliyopita, na alihamia kigumu bila kupiga plaster. Na alipokuwa anajenga wala hakuombwa kibali cha ujenzi, lkn leo hii amepata vihela ili afanye finishing ya nyumba yake anaambiwa lazima akalipie kwanza kibali. Hivi hii imekaaje...yaani Tanzania ya Mama Samia imefikia hapo?

Alipojaribu kufuatilia Ofisi ya jiji aliambiwa hilo ni agizo kutoka kwa mkurugenzi wa jiji la Ilala...Ni sheria! Wakidai kwamba kila aina ya ujenzi na ukarabati wowote unaotumia materials kama cement, nondo, mchanga nk bila kujali ukubwa na aina ya jengo, ni lazima mhusika aombe na kulipia kibali cha ujenzi kabla ya kuendelea na ujenzi/ukarabati.

Hatari sana....Juzi kati tumetoka kwenye ongezeko la tozo za miamala ya simu, leo tena zimekuja tozo za LUKU. Huku JIJI nao wanataka tozo za vibali vya kukarabati vibandavyetu. Hii nchi sasa naona kila mahali ni pa MOTO...hapashikiki! NIMECHOKA!
 
Ni utaratibu wa kawaida sema huwa haufatiliwi sana toka zamani. Ila kwa wanaojenga ama kukarabati city centre na kariakoo wanajua hili vizuri.
 
Hivi kupiga plasta nyumba ni ikarabati au stage ya ujenzi??ina maana ataoma kibali kupiga rangi,tiles,ceiling board nk???
 
Huyo mwenyekiti unamvuta chemba unampa elfu kumi ya kubrashia viatu vyake naye apendeze aonekane kama mwenyekiti , anaangalia pembeni unakarabati nyumba yako hata wakimuuliza anawaambia ni yeye anakarabati nyumba yake, wanaachana naye ni mwenzao huyo. Hujui kula na viongozi wa chama kile

Sent from my Infinix X572 using JamiiForums mobile app
 
ili upate kibali unatoboka hela ndefu... Mimi nilimtoa mjumbe buku 2 ya shimwa... sikuzinguliwa na yeyote.

viongozi Wa ccm bila kuwapoza utalipa kubwa zaidi
 
Hawana lolote wanashindwa hata kupendezesha jiji hata kwa kumaintain garden za barabarani...wamachinga wamejaa kila kona. Wao wanajua uzuri wa jiji ni mijengo tu. Wakajifunze Nairobi na kigali
 
Ni utaratibu wa kawaida sema huwa haufatiliwi sana toka zamani. Ila kwa wanaojenga ama kukarabati city centre na kariakoo wanajua hili vizuri.

Nakubaliana na wewe ,ukitaka kujenga au renovation ya jengo ni lazima uombe kibali ,hata kujenga fensi inatakiwa uwe na kibali.
 
Kuna sheria kwenye sheria za mipango miji inamtaka mtu anayejenga awe na Kibali cha ujenzi atatakiwa kupeleka ramani ya jengo kwenye mamlaka,Engineer,tanesco na shirika la simu lazima wafanye survey kwenye hilo eneo ili wajiridhishe.
 
Kuna sheria kwenye sheria za mipango miji inamtaka mtu anayejenga awe na Kibali cha ujenzi atatakiwa kupeleka ramani ya jengo kwenye mamlaka,Engineer,tanesco na shirika la simu lazima wafanye survey kwenye hilo eneo ili wajiridhishe.
Ila sio kupiga plasta
 
Kumradhi mleta uzi, ilala ni jiji tangu lini? Mi najua jiji ni Dar, na ramani ya jiji la Dar ni ramani nzima ya iliyokuwa wilaya ya Ilala. Nb: kwa kifupi ndani ya Tanzania hakuna jiji linaloitwa ilala, ila ilala ni jiji la Dar!
 
Kumradhi mleta uzi, ilala ni jiji tangu lini? Mi najua jiji ni Dar, na ramani ya jiji la Dar ni ramani nzima ya iliyokuwa wilaya ya Ilala. Nb: kwa kifupi ndani ya Tanzania hakuna jiji linaloitwa ilala, ila ilala ni jiji la Dar!
Hufuatiliagi vyombo vya habari ndio maana unabaki nyuma hivi
 
Back
Top Bottom