Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,395
- 13,266
Hakuna la kuhangaza hapa. Kama wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika wanachaguliwa kuingia sekondari unategemea nini? Hapa wanakwepa aibu ya kufaulisha wasiostshili ili wawe na takwimu kubwa. Wanchotafuta au kutaka wao ni takwimu kubwa na si ubora. Ni katika nchi ya ajabu kama Tanzania ndipo waziri anasimama hadharani na kutangaza kuwa wanafunzi zaidi ya 5200 wamefaulu kuingia kidato cha kwanza wakiwa hawahui kusoma. Sasa jiulize huko sekondari wanafanya nini? Hatua kama hii ni mwendelezo ule ule wa kufaulisha badala ya wanafunzi kufaulu wenyewe. Hawa si muda mrerefu utawakuta vyuo vikuu. Wamepitaje? Ni kwa njia hii kwakuwa viongozi wanacheza na idadi na si ubora. Mwakani wakati wa kampeni utawasikia wakitoa takwimu hizo za kuongezeka kwa ufaulu na idadi ya wanafunzi mashuleni na vyuoni. Na ndipo kwa mtindo huu tunawapata mawaziri kama Mulugo asiyejua hata historia ndogo ya nchi yake na kiongozi mkuu asiyejua kwanini nchi yake ni masikini licha ya kuwa na shahada ya uchumi! LONG LIVE "BIG RESULTS NOW!"