Mwizukulu wa Buganda
JF-Expert Member
- Nov 19, 2024
- 638
- 1,771
Serikali imeanza mpango wa kupanga upya walimu kulingana na viwango vyao vya elimu, ambapo walimu wenye stashahada watapangiwa kufundisha katika shule za msingi huku wale wenye shahada wakielekezwa kufundisha ngazi ya sekondari.
Hatua hiyo inalenga kuongeza ufanisi katika ufundishaji kwa kuzingatia utaalamu wa walimu pamoja na mahitaji ya kila ngazi ya elimu.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Daniel Mushi, amesema mpango huo ni sehemu ya maboresho ya mifumo na miundombinu ya elimu nchini.