Walimu kupiga watoto mpaka kuua! ipo siku atauliwa mtoto wa kiongozi ndipo tutaamka

Wazazi tupo humu kuponda walimu wakati malezi ya hovyo tunayo wapa watoto hatujioni.Mm sio nwalim ila kuna kaya ukienda unakuta kuna watoto hata adabu hayana kusalimia tu wakubwa hayawezi na kauli yanazo wajibu wazazi hapana kwa kweli mm ningekua mwalimu naona siku moja tu ningeua mtoto wa watu.Wazazi pia tuangalieni malezi yetu.... tunawapelekea walimu watoto washenz majeuri mpaka bas.
 
Tatizo la wazazi mnaficha magonjwa ya watoto wenu,akiguswa na mwalimu kidogo inakuwa tiketi ya kifo na malalamiko kuanzia hapo,hakuna mwalimu wa kuchapa mtoto wa miaka 6 kwa jinsi hiyo inavyoelezwa never
Acha ujinga wewe mwalimu,madeni yanawafanya muwe na hasira sana
 
Jirani yangu mtoto wake wa form 4,ashapoteza jicho moja, baada ya mwalimu kumuadhibu na kipande cha fimbo kupiga jichoni, walimtekeleza mtoto KCMC huku mzazi akifichwa, amekuja kuambiwa na matron muda mrefu ushapita, wamekuja kusaidiwa na mkuu wa Wilaya baada ya mama wa mtoto kwenda kwake kuomba msaada, Shule wakalazimishwa kughalimia matibabu India, huko wakaambiwa mtoto amecheleweshwa sana, kuna uwezekano lisione tena.
 
Kwa bahati nzuri watoto wa sisi viongozi awasomi shule wanazo piga🤣🤣🤣

Mlipo ambiwa elimu GHARAMA mlibeza na mkachekelea elimu ya bure 🤣🤣🤣

Mtaisoma namba​
 
Uyo dogo alikua mgonjwa kabla ila tu hakuonyesha dalili za wazi, Huyu BTP mjinga alichokosea ni kumchapa mtoto mdogo kwa uchungu kama mwizi hii ilidhoofisha hali yake ya mwanzo sasa.
Me naweza sema Mzazi wa Mtoto na Mwalim wote wameshirikiana kuua. Issue ya mtu kuvunja damu we unampa panadol huoni ni Utaahira huo?

Angalizo, Oeni wanawake wenye akili na Walimu wawe na angalau dvn 1 ya 4m4.
 
Inaonekana mtoto alikuwa mgonjwa na alicheleweshwa kupata huduma sahihi za kiafya ila ndiyo hivyo tena jumba bovu limemwangukia teacher.
Huyo mwalimu hakwepi kosa lake.
Amehamsha magonjwa mengine.
Kwanza amekiuka kanuni ya adhabu ya viboko iliyowekwa na wizara husika.
Unapigaje mtoto kichwani?
Unapigaje mtoto wakati hujui historia yake ya afya?
Huyo kichaa akapigwe mjebele jela atatia akili.
 
Imeniuma sana. Sana yaani....

Lazima kesi za wanafunzi kudhuriwa na waalimu zitakua nyingi, ila zinafichwa.

Huyo mtoto hata kama alikuwa anaumwa, asingepigwa hivyo angekufa?

Mnaosema watoto wanakosa adabu, kuchelewa kuchukua namba ni kosa la kupigwa hivyo?

Hao waalimu ni wauwaji.

Post moterm inafanyika leo, lakini post moterm hazi-fojiki kweli? mimi siamini.

Kuna haja ya kudhibiti utoaji adhabu mashuleni.

Watoto hawadhuriwi kimwili tu, hata kiakili wanaweza kupata trauma.
 
Hii tabia imekithiri sana ya kupiga watoto kwa mangumi, mateke, na mbaya zaidi kupiga watoto mgongoni ambako ndiko kuna uti wa mgongo! Tabia ya kuficha na kutoa taarifa za uongo kumkandamiza aliyeuliwa na kukosesha haki ndiko kunafanya walimu waendelee na tabia hii mbaya kabisa!

Halafu kuna hawa walimu wa vitendo ambao sio waalimu kamili wao wanawapigisha watoto mazoezi ya JKT mwishowe wanaua

Soma hii ya tukio la moshi kwa kweli nimesikitika sana

Mimi hii ikinitokea kwa mwanangu lazma ntalala mbele mwalimu husika sina msamaha

----
Jeshi la Polisi linawashikilia na kuwahoji walimu watano tarajali wa mafunzo ya ualimu (BTP) wanaofundisha katika Shule ya Msingi Mrupanga mkoani Kilimanjaro, kwa madai ya kuhusika na kifo cha mwanafunzi wa darasa la kwanza, Jonathan Makanyaga (6).

Mwanafunzi huyo, mkazi wa Kijiji cha Kimanganuni chini, Kata ya Uru Kusini wilayani Moshi, alifariki dunia Machi 10, mwaka huu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini, KCMC alikolazwa kwa matibabu, kwa kile kinachodaiwa alichapwa viboko na mmoja wa walimu hao baada ya kuchelewa shuleni.

Inadaiwa Februari 28, mwanafunzi huyo akiwa na wenzake wawili walichapwa na mwalimu huyo (jina halijatajwa) baada ya kuchelewa shuleni hapo na Jonathan alichapwa sehemu mbalimbali mwilini, kisha kuangushwa chini.

Inaelezwa wenzake wawili alikuwa nao wakati wanachapwa walijikinga na fimbo hizo kwa kutumia mabegi waliyokuwa wamebeba mgongoni na Jonathan alishindwa kujizuia na kuumizwa sehemu ya uti wa mgongo, mbavuni na sehemu ya mapajani na kisha kuangushwa chini.

Akizungumza na Mwananchi jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alisema mama na bibi wa Jonathan walikwenda shuleni kuhoji kwa nini mtoto wao amerudi nyumbani akiwa na hali hiyo na ndipo walimu waliwapoza na wakashirikiana nao kumpeleka hospitali bila kutoa taarifa polisi.

“Mtoto aliendelea na matibabu mpaka Machi 10 alipofariki. Tulichofanya, lilifunguliwa jalada la kifo cha mashaka kwa sababu hakuna taarifa iliyotolewa awali, ila tunawashikilia walimu wa mafunzo ya vitendo watano kwa mahojiano na kesho (leo) kutafanyika postmortem (uchunguzi wa kifo) ili kujua chanzo cha kifo chake,” alisema.


Mama afunguka

Janeth Shayo, mama wa mtoto huyo alieleza Februari 28 mwanaye alirudi nyumbani akiwa hana furaha na mdogo wa Jonathan alimweleza kuwa kaka yake anavuja damu mdomoni.

Alisema alipomwangalia alibaini ni kweli, mwanaye anavuja damu mdomoni na puani, na alipomuuliza alimweleza amechapwa viboko na mmoja wa walimu hao kwa sababu ya kuchelewa kushika namba saa moja kamili asubuhi.

“Jioni nilipakua chakula, nikamwambia baada ya kula apumzike kidogo kisha aende kulala, wakati nadeki mdogo wake akaniita akanambia Jonathan anatoka damu puani, nikimwangalia damu zinatoka bado nikamuuliza wapi panauma, akanambia kichwa kinamuuma, nilimpa dawa za maumivu (paracetamol) wakalala na mdogo wake,” alisema.

Alisema asubuhi ya siku iliyofuata aligundua mtoto huyo alikuwa na damu nyingi mdomoni, wakati anamuandaa ampeleke hospitali alibaini ana majeraha mgongoni.

“Nikamuuliza tena umejigonga wapi? Akasema hajajigonga, mgongo ulikuwa umevimba na eneo la chini ya uti wa mgongo kuna uvimbe umevilia damu na ni kweusi, pajani nako kuna alama ya fimbo na kumevilia damu, kwenye mguu nako kumevimba," alisema.

Alisema hali hiyo ilimfanya aende shule kujua sababu za mtoto wake kuadhibiwa kiasi hicho.

“Nilikutana na mwalimu mkuu msadizi ambaye baada ya kuona hali ya mtoto, akanipa Sh20,000 nikamtibu na itakavyokuwa niwaambie. Nilikwenda zahanati nikapewa dawa, daktari akanambia akizidiwa nimrudishe achomwe sindano, nilienda naye nyumbani lakini bado hali yake ilikuwa si nzuri,” alisema na kuongeza;

“Sikuweza kulala ilibidi nimrudshe zahanati, alipomwona na kumwangalia kwenye macho akanambia nimpeleke hospitali ya St Joseph.
"Nilipofika mapokezi walimwangalia mtoto hali yake ilivyo, nikaambiwa nikafungue faili, walivyomuona mtoto kadri siku zilivyokuwa zikienda, wakanishauri nimpeleke KCMC kwa vipimo vikubwa zaidi na Machi 8 tukawa tumeenda,"

Hata hivyo, alisema baadaye daktari aliyekuwa akimhudumia alimweleza kuwa mtoto ana changamoto ya seli sahani na kuna damu imevujia tumboni, hivyo atawekewa mirija.

“Kabla hilo halijafanyika mwanangu akawa amefariki tarehe 10," alisimulia mama huyo.

Alipotafutwa mwalimu mkuu wa shule, Florah Kahabi alisema hawezi kuzungumzia tukio hilo kwa kuwa lipo kwenye vyombo husika na kwamba yupo msemaji wa tukio hilo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Shedrack Mhagama alisema baadaye ya kupita taarifa ya mwanafunzi kufariki shuleni hapo walifuatilia kujua ukweli wake na kwamba taarifa walizonazo ni kuwa mwanafunzi huyo alikuwa anaumwa saratani ya damu.

“Nilipata hizi taarifa, nilifuatilia kule shuleni, mtoto alikuwa anaumwa saratani kwa muda mrefu na ndio maana amefariki," alisema mkurugenzi huyo.

Kwa upande wake, Ofisa Uhusiano wa Hospitali ya KCMC, Gabriel Chisseo alisema, “Baada ya kufanyiwa uchunguzi na madaktari wetu, waligundua alikuwa na upungufu mkubwa wa damu na baadaye vipimo vilionyesha alikuwa na saratani ya damu, kwa mfano chembe sahani pekee tu zikikutwa 11 kwa hiyo uwezekano wa kupata matatizo ni mkubwa zaidi".

Chanzo: Mwananchi
Hii inaskitisha sana,nikisoma habari za huyu mtoto na wengine kama yeye,waliokutwa na visa,hivi,machozi huwa yananitoka.Na pia ni muhimu,watu wanaopita karibu ya shule na wanaoishi jirani na shule,wakiona matukio kama haya,waende kuwatetea hawa watoto,mimi nikipita karibu ya shule,nikiona wanafunzi wanaadhibiwa na mwalimu au waalimu,lazima niingilie kati kuwatetea hawa wanafunzi.
Kwa nini kusianzishwe chama cha kuwatetea wanafunzi,na kiwe na matawi mpaka mashuleni na mpaka vyuoni?
 
Imeniuma sana. Sana yaani....

Lazima kesi za wanafunzi kudhuriwa na waalimu zitakua nyingi, ila zinafichwa.

Huyo mtoto hata kama alikuwa anaumwa, asingepigwa hivyo angekufa?

Mnaosema watoto wanakosa adabu, kuchelewa kuchukua namba ni kosa la kupigwa hivyo?

Hao waalimu ni wauwaji.

Post moterm inafanyika leo, lakini post moterm hazi-fojiki kweli? mimi siamini.

Kuna haja ya kudhibiti utoaji adhabu mashuleni.

Watoto hawadhuriwi kimwili tu, hata kiakili wanaweza kupata trauma.
Na hata kama hakudhurika sasa,huwenda atakapokuwa myu mzima,akapata madhara.Na nafikiri hii,ndio inapelekea mahospital kuwa na wagonjwa wengi,wamatatizo mbali mbali sugu,huwenda waliumizwa utotoni shule,kwa fimbo za kichwani,mgongoni,makalioni,mbavuni nk.
 
Hii tabia imekithiri sana ya kupiga watoto kwa mangumi, mateke, na mbaya zaidi kupiga watoto mgongoni ambako ndiko kuna uti wa mgongo! Tabia ya kuficha na kutoa taarifa za uongo kumkandamiza aliyeuliwa na kukosesha haki ndiko kunafanya walimu waendelee na tabia hii mbaya kabisa!

Halafu kuna hawa walimu wa vitendo ambao sio waalimu kamili wao wanawapigisha watoto mazoezi ya JKT mwishowe wanaua

Soma hii ya tukio la moshi kwa kweli nimesikitika sana

Mimi hii ikinitokea kwa mwanangu lazma ntalala mbele mwalimu husika sina msamaha

----
Jeshi la Polisi linawashikilia na kuwahoji walimu watano tarajali wa mafunzo ya ualimu (BTP) wanaofundisha katika Shule ya Msingi Mrupanga mkoani Kilimanjaro, kwa madai ya kuhusika na kifo cha mwanafunzi wa darasa la kwanza, Jonathan Makanyaga (6).

Mwanafunzi huyo, mkazi wa Kijiji cha Kimanganuni chini, Kata ya Uru Kusini wilayani Moshi, alifariki dunia Machi 10, mwaka huu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini, KCMC alikolazwa kwa matibabu, kwa kile kinachodaiwa alichapwa viboko na mmoja wa walimu hao baada ya kuchelewa shuleni.

Inadaiwa Februari 28, mwanafunzi huyo akiwa na wenzake wawili walichapwa na mwalimu huyo (jina halijatajwa) baada ya kuchelewa shuleni hapo na Jonathan alichapwa sehemu mbalimbali mwilini, kisha kuangushwa chini.

Inaelezwa wenzake wawili alikuwa nao wakati wanachapwa walijikinga na fimbo hizo kwa kutumia mabegi waliyokuwa wamebeba mgongoni na Jonathan alishindwa kujizuia na kuumizwa sehemu ya uti wa mgongo, mbavuni na sehemu ya mapajani na kisha kuangushwa chini.

Akizungumza na Mwananchi jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alisema mama na bibi wa Jonathan walikwenda shuleni kuhoji kwa nini mtoto wao amerudi nyumbani akiwa na hali hiyo na ndipo walimu waliwapoza na wakashirikiana nao kumpeleka hospitali bila kutoa taarifa polisi.

“Mtoto aliendelea na matibabu mpaka Machi 10 alipofariki. Tulichofanya, lilifunguliwa jalada la kifo cha mashaka kwa sababu hakuna taarifa iliyotolewa awali, ila tunawashikilia walimu wa mafunzo ya vitendo watano kwa mahojiano na kesho (leo) kutafanyika postmortem (uchunguzi wa kifo) ili kujua chanzo cha kifo chake,” alisema.


Mama afunguka

Janeth Shayo, mama wa mtoto huyo alieleza Februari 28 mwanaye alirudi nyumbani akiwa hana furaha na mdogo wa Jonathan alimweleza kuwa kaka yake anavuja damu mdomoni.

Alisema alipomwangalia alibaini ni kweli, mwanaye anavuja damu mdomoni na puani, na alipomuuliza alimweleza amechapwa viboko na mmoja wa walimu hao kwa sababu ya kuchelewa kushika namba saa moja kamili asubuhi.

“Jioni nilipakua chakula, nikamwambia baada ya kula apumzike kidogo kisha aende kulala, wakati nadeki mdogo wake akaniita akanambia Jonathan anatoka damu puani, nikimwangalia damu zinatoka bado nikamuuliza wapi panauma, akanambia kichwa kinamuuma, nilimpa dawa za maumivu (paracetamol) wakalala na mdogo wake,” alisema.

Alisema asubuhi ya siku iliyofuata aligundua mtoto huyo alikuwa na damu nyingi mdomoni, wakati anamuandaa ampeleke hospitali alibaini ana majeraha mgongoni.

“Nikamuuliza tena umejigonga wapi? Akasema hajajigonga, mgongo ulikuwa umevimba na eneo la chini ya uti wa mgongo kuna uvimbe umevilia damu na ni kweusi, pajani nako kuna alama ya fimbo na kumevilia damu, kwenye mguu nako kumevimba," alisema.

Alisema hali hiyo ilimfanya aende shule kujua sababu za mtoto wake kuadhibiwa kiasi hicho.

“Nilikutana na mwalimu mkuu msadizi ambaye baada ya kuona hali ya mtoto, akanipa Sh20,000 nikamtibu na itakavyokuwa niwaambie. Nilikwenda zahanati nikapewa dawa, daktari akanambia akizidiwa nimrudishe achomwe sindano, nilienda naye nyumbani lakini bado hali yake ilikuwa si nzuri,” alisema na kuongeza;

“Sikuweza kulala ilibidi nimrudshe zahanati, alipomwona na kumwangalia kwenye macho akanambia nimpeleke hospitali ya St Joseph.
"Nilipofika mapokezi walimwangalia mtoto hali yake ilivyo, nikaambiwa nikafungue faili, walivyomuona mtoto kadri siku zilivyokuwa zikienda, wakanishauri nimpeleke KCMC kwa vipimo vikubwa zaidi na Machi 8 tukawa tumeenda,"

Hata hivyo, alisema baadaye daktari aliyekuwa akimhudumia alimweleza kuwa mtoto ana changamoto ya seli sahani na kuna damu imevujia tumboni, hivyo atawekewa mirija.

“Kabla hilo halijafanyika mwanangu akawa amefariki tarehe 10," alisimulia mama huyo.

Alipotafutwa mwalimu mkuu wa shule, Florah Kahabi alisema hawezi kuzungumzia tukio hilo kwa kuwa lipo kwenye vyombo husika na kwamba yupo msemaji wa tukio hilo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Shedrack Mhagama alisema baadaye ya kupita taarifa ya mwanafunzi kufariki shuleni hapo walifuatilia kujua ukweli wake na kwamba taarifa walizonazo ni kuwa mwanafunzi huyo alikuwa anaumwa saratani ya damu.

“Nilipata hizi taarifa, nilifuatilia kule shuleni, mtoto alikuwa anaumwa saratani kwa muda mrefu na ndio maana amefariki," alisema mkurugenzi huyo.

Kwa upande wake, Ofisa Uhusiano wa Hospitali ya KCMC, Gabriel Chisseo alisema, “Baada ya kufanyiwa uchunguzi na madaktari wetu, waligundua alikuwa na upungufu mkubwa wa damu na baadaye vipimo vilionyesha alikuwa na saratani ya damu, kwa mfano chembe sahani pekee tu zikikutwa 11 kwa hiyo uwezekano wa kupata matatizo ni mkubwa zaidi".

Chanzo: Mwananchi
Actualy hakuna mtoto wa kingozi atauliwa, why hawasomi huko
 
Wewe kama mwalimu huwezi kufuata muongozo wa utoaji adhabu kwa wanafunzi?

Au kusoma hamjui vizuri ndiyo maana licha ya kupewa muongozo wa utoaji adhabu mashuleni lakini bado hukuelewa?

Fuateni sheria vinginevyo mtaishia jela na kupelekea kunyongwa hadi kufa kisa kuendekeza upuuzi.

Mimi kitaaluma ni lawyer huwa napita mashuleni kukutana na walimu kuwakumbusha juu ya umuhimu wa kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali ya elimu na adhabu.
Binafsi mimi siyo mwalimu , ila kuna namna waalimu wanachukuliwa poa. Hata hivo siungi mkono adhabu zilizo pitiliza.

Kwa miaka hivi karibuni wazazi kama wamekua wanawachagulia waalimu namna mtoto wake / wao aadhibiwe. Hii imepelekea walimu kutokua na time na shida zozote na wanafunzi . Saizi mwalimu anaangalia mambo yake tuu, mtoto aelewe ama asielewe , akosee ama asikosee hiyo haimuuhusu atajijua yeye na mzazi wake.
 
Watoto sikuizi kama wazazi wao tuu wanajidai wanajua kila kitu .
 
Back
Top Bottom