ladyfurahia
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 14,758
- 9,592
Muwazima wanamod wenzangu humu ndani? Mnaendeleaje
Ni siku ingine ya Blue Monday iliyojaa uchovu kwa wote waliokuwa katika pilikapilika za weekend,
na mihangaiko ya utafutaji wa shiilingi ktk kila kona ya mji.
Mwenzenu leo nimeonelea niwajie kwa jambo moja ambalo limekuwa na maswali mengi sana juu ya kichwa changu,
hasa hiyo mada hapo juu niliyotoa, nimeshindwa kuwaelewa wanadamu kwa vile walivyo, wengi wao wamekuwa
watu wa ajabu sana tena sana, Mtu anaamua tu kugombana na mwenzie ukiangalia wanachogombania ni kitu
cha kijinga sana hata ukitaka kuuliza watakwambia ameazima kiatu changu huu ni mwaka wa 3 na hataki kunipa
Sasa wewe ndugu yangu kiatu cha watu kwanini hutaki kumlejeshea unabaki nacho, atakwambia kuwa kiliharibika
au sina nishakitupa jalalani, kitu sio chako umekiazima kwanini usikirudishe kwa mwenyewe, unakaa nacho mpaka kinabaribika, kwanini jamani unakuwa una hata utu jamani?
Wengine humuhumu ndani ya JF CC wanaanza kugombana tu hovyo pasipo msingi wowote ukiuliza ni maandishi tu yaliteleza kidogo, mtu anawaka utafikiri gesi ya mtwara jamani. kwa hapa sitaki kueleza zaidi wenyewe mwafahamu
mpaka yapelekea kutokuwa na urafiki tena na mwananajf mwenzio. Jamani tuache tabia ya ugomvi humu ndani.tupendane na tuchukuliane na kujaliana huo ndio urafiki wa kweli.
Wengine hasa akina dada wenzangu walioko mahome utakuta mtu anagombana na mwenzio na kumporomoshea lugha zisizopendeza kisa eti kachukua mume wake, hii yote yatokana na nini jamani, kwanini tusipendane na kwanini tunachukiana kiasi hicho. Tabia ya ugomvi sio njema. Na makaka nao wanaugomvi wa kichinichini tena hao hata
kuuana wanauana ovyo utafikiri wamekazwa. Acheni jamani tabia hiyo haimpendezi Mungu kabisa.
Katika Nchi na Mataifa mengi yameingia katika ugomvi ambao unakuwa mkubwa na kuleta mapigano ya wenyewe kwa wenyewe (civil war) ambayo yanapelekea mauaji ya kutisha, unyama usioelezeka, njaa isiyoneneka, uharibifu wa maliasili, magonjwa, na hata kuleta chuki isiyoweza pimika.
Hivi kwanini jamani wanadamu tunakuwa hivi kwanini tusipendane jamani, mfano halisi ni nchi ya jirani hapo Kenya na hata hapa nchi kwetu napo hasa nyanda za juu kaskazini, Mwanza geita, na pwani pia tunakwenda wapi jamani kwanini tunagombana na kupigana hata kuuana? NINI KIPO NYUMA YA PAZIA LETU HAPA TANZANIA?
na kwanini viongozi wanashindwa kufuatilia majanga yanapotokea? Kwanini tunakuwa watu tusiopendana
na kufurahiana?
Kwa kweli waungwana nimeshindwa kueleza kwani hapa machozi yananitoka hususani kwa Taifa letu TZ tunakwenda wapi jamani? furaha ya kujiita mm mtanzania sasa imetoweka, kutokana na vita hivi vya wenyewe kwa wenyewe, kwani wandugu marafiki zangu nyie hamuoni hili? Najua mnaliona basi ni vyema tumuombe Mungu atuepushe na mambo haya, tuwe watu wenye kujaliana, kupendana, kutakiana heri, na hata kuhurumiana kwani wale wagombanao ndio wapatanao.
Hebu tujifunze kumpenda / kuwapenda mwenzio / wenzio na sio kumchukia kwa kisa kidogo tu, hata kama amekukosea usimlipize kisasi, kwani kisasi ni cha Bwana muumba wako.
siku njema marafiki.
copy to: Erickb52, Mamndenyi, Filipo, Arushaone, my cousin charminglady, Ruttashobolwa, Madame B, watu8, passion lady, Bakulutu, Mentor, Jiwe Linaloishi, gfsonwin, na mpiganaji mwenzangu Smile
hebu angalia hapa:
Ni siku ingine ya Blue Monday iliyojaa uchovu kwa wote waliokuwa katika pilikapilika za weekend,
na mihangaiko ya utafutaji wa shiilingi ktk kila kona ya mji.
Mwenzenu leo nimeonelea niwajie kwa jambo moja ambalo limekuwa na maswali mengi sana juu ya kichwa changu,
hasa hiyo mada hapo juu niliyotoa, nimeshindwa kuwaelewa wanadamu kwa vile walivyo, wengi wao wamekuwa
watu wa ajabu sana tena sana, Mtu anaamua tu kugombana na mwenzie ukiangalia wanachogombania ni kitu
cha kijinga sana hata ukitaka kuuliza watakwambia ameazima kiatu changu huu ni mwaka wa 3 na hataki kunipa
Sasa wewe ndugu yangu kiatu cha watu kwanini hutaki kumlejeshea unabaki nacho, atakwambia kuwa kiliharibika
au sina nishakitupa jalalani, kitu sio chako umekiazima kwanini usikirudishe kwa mwenyewe, unakaa nacho mpaka kinabaribika, kwanini jamani unakuwa una hata utu jamani?
Wengine humuhumu ndani ya JF CC wanaanza kugombana tu hovyo pasipo msingi wowote ukiuliza ni maandishi tu yaliteleza kidogo, mtu anawaka utafikiri gesi ya mtwara jamani. kwa hapa sitaki kueleza zaidi wenyewe mwafahamu
mpaka yapelekea kutokuwa na urafiki tena na mwananajf mwenzio. Jamani tuache tabia ya ugomvi humu ndani.tupendane na tuchukuliane na kujaliana huo ndio urafiki wa kweli.
Wengine hasa akina dada wenzangu walioko mahome utakuta mtu anagombana na mwenzio na kumporomoshea lugha zisizopendeza kisa eti kachukua mume wake, hii yote yatokana na nini jamani, kwanini tusipendane na kwanini tunachukiana kiasi hicho. Tabia ya ugomvi sio njema. Na makaka nao wanaugomvi wa kichinichini tena hao hata
kuuana wanauana ovyo utafikiri wamekazwa. Acheni jamani tabia hiyo haimpendezi Mungu kabisa.
Katika Nchi na Mataifa mengi yameingia katika ugomvi ambao unakuwa mkubwa na kuleta mapigano ya wenyewe kwa wenyewe (civil war) ambayo yanapelekea mauaji ya kutisha, unyama usioelezeka, njaa isiyoneneka, uharibifu wa maliasili, magonjwa, na hata kuleta chuki isiyoweza pimika.
Hivi kwanini jamani wanadamu tunakuwa hivi kwanini tusipendane jamani, mfano halisi ni nchi ya jirani hapo Kenya na hata hapa nchi kwetu napo hasa nyanda za juu kaskazini, Mwanza geita, na pwani pia tunakwenda wapi jamani kwanini tunagombana na kupigana hata kuuana? NINI KIPO NYUMA YA PAZIA LETU HAPA TANZANIA?
na kwanini viongozi wanashindwa kufuatilia majanga yanapotokea? Kwanini tunakuwa watu tusiopendana
na kufurahiana?
Kwa kweli waungwana nimeshindwa kueleza kwani hapa machozi yananitoka hususani kwa Taifa letu TZ tunakwenda wapi jamani? furaha ya kujiita mm mtanzania sasa imetoweka, kutokana na vita hivi vya wenyewe kwa wenyewe, kwani wandugu marafiki zangu nyie hamuoni hili? Najua mnaliona basi ni vyema tumuombe Mungu atuepushe na mambo haya, tuwe watu wenye kujaliana, kupendana, kutakiana heri, na hata kuhurumiana kwani wale wagombanao ndio wapatanao.
Hebu tujifunze kumpenda / kuwapenda mwenzio / wenzio na sio kumchukia kwa kisa kidogo tu, hata kama amekukosea usimlipize kisasi, kwani kisasi ni cha Bwana muumba wako.
siku njema marafiki.
copy to: Erickb52, Mamndenyi, Filipo, Arushaone, my cousin charminglady, Ruttashobolwa, Madame B, watu8, passion lady, Bakulutu, Mentor, Jiwe Linaloishi, gfsonwin, na mpiganaji mwenzangu Smile
hebu angalia hapa:
Last edited by a moderator: