Nimekuwa nikijiuliza mara nyingi hivi hawa vijana wanaoshika nafasi za juu kwenye matokeo ya kidato cha Nne na Sita ambao kimsingi huwa na ufaulu wa Division 1.7 kwa Form Four na 1.3 kwa Form 6 huwa wanaishia wapi? Kwasababu najua kuna wengine huwa wanasoma Sheria, kwanini wasingekuwa wanapelekwa kwenye kesi kma hizi za usuluhusi na makampuni ya wazungu ambayo kila siku tunashindwa kesi.
Wenzetu kwenye kesi kama hizo huwa wanapeleka vichwa hasa ile cream yenyewe iliyofaulu vizuri kuanzia sekondari mpaka chuo kikuu.
Vinginevyo labda elimu yetu ina mapungufu au kukariri sana kiasi kwamba hatuwezi kuona impact ya wale vipanga wetu.
Wenzetu kwenye kesi kama hizo huwa wanapeleka vichwa hasa ile cream yenyewe iliyofaulu vizuri kuanzia sekondari mpaka chuo kikuu.
Vinginevyo labda elimu yetu ina mapungufu au kukariri sana kiasi kwamba hatuwezi kuona impact ya wale vipanga wetu.