Wale mliooa wanawake wanaofanya kazi

Wale mliooa wanawake wanaofanya kazi

Mrejesho.........Badala ya kwenda mbele ndo narudi nyuma!

Huyu mwenzangu ye kaajiriwa na serikali na mwisho wa mwezi sio haba. Tunakaa mikoa tofauti, Usiku wa kuamkia leo nikampa maneno matamtam sana ili nianze kuandaa mazingira ya kumuomba aniongezee laki na 10 ili niagizie vifaranga vipya kwenye mradi wangu maana bado haujaanza kutoa matunda. Nilipomwambia tu akaanza kuniambia ooh hela sina na wakati najua juzi kapokea mshahara.
Akiwa katikati ya mwezi hali mbaya huwa nafanya kila niwezalo nimtumie hata 50 ya matumizi kwa wiki ila yeye laki tu karuka viunzi.
Hapa najiona kama nimeruka stage kwenye maisha yangu, kutokana na kuoana na yeye now nashindwa hata kujilipua kwenda mbali kutafuta maisha, nakaa karibu nae ili niwajibike kama mwanaume kwake na kwa mtoto wetu lakini mwenzangu akipata hela anajiangalia sana yeye tu.
Sioni faida ya hii ndoa soon naongeza idadi ya single mothers mtaani.
Pole mkuu, kaa nae chini muelewane
 
Mwanamke alioajiliwa na hana makuzi na malezi bora, ni mzigo na kero kubwa pesa yao ionekani nyumbani, ni muendo wa vikomba, michango ya sherehe, safari za kwao, nk sioni maana yoyote yaye kufanya kazi, nimesha surrender......kaa nyumbani kama hutaki changua moja mimi au Kazi..
Pole mkuu [emoji3]
 
Ni mwaka wa nne huu na bado sijutii. Tunasaidiana kwa mengi, kuanzia matumizi ya nyumbani mpaka kwenye investments. Na hata bahati mbaya nikitangulia mbele za haki, Niko na confidence of more than 60% kwamba mtoto (watoto) wangu are in good hands.
Usijali ukitangulia atakuja jamaa mwenye caliber kama yako kumpa support na kula mzigo. Yah kuomba mungu akuwekee mpaka mzeeke.
 
Bora wewe, kiasi kikubwa cha matumizi yake anajitegemea mwenyewe. Kuna jamaa yangu, mke anachukua 20,000 daily kwa ajili ya kula na mafuta ya gari. Saloon anaomba hela na mshahara wake huwa haujulikani unafanya kitu gani. Akiulizwa ugomvi wa kufa mtu
Sio wewe mkuu [emoji3]
 
Mrejesho.........Badala ya kwenda mbele ndo narudi nyuma!

Huyu mwenzangu ye kaajiriwa na serikali na mwisho wa mwezi sio haba. Tunakaa mikoa tofauti, Usiku wa kuamkia leo nikampa maneno matamtam sana ili nianze kuandaa mazingira ya kumuomba aniongezee laki na 10 ili niagizie vifaranga vipya kwenye mradi wangu maana bado haujaanza kutoa matunda. Nilipomwambia tu akaanza kuniambia ooh hela sina na wakati najua juzi kapokea mshahara.
Akiwa katikati ya mwezi hali mbaya huwa nafanya kila niwezalo nimtumie hata 50 ya matumizi kwa wiki ila yeye laki tu karuka viunzi.
Hapa najiona kama nimeruka stage kwenye maisha yangu, kutokana na kuoana na yeye now nashindwa hata kujilipua kwenda mbali kutafuta maisha, nakaa karibu nae ili niwajibike kama mwanaume kwake na kwa mtoto wetu lakini mwenzangu akipata hela anajiangalia sana yeye tu.
Sioni faida ya hii ndoa soon naongeza idadi ya single mothers mtaani.
Pole sana
Kaa nae myaongee kwamba ni wajibu wetu wote kutunza familia na kusaidiana ili mfikie malengo na muwe familia yenye mafanikio. Mafanikio kwny ndoa hayaletwi na mume tu bali wote wawili hasa kama nae ana kipato
 
Bora wewe, kiasi kikubwa cha matumizi yake anajitegemea mwenyewe. Kuna jamaa yangu, mke anachukua 20,000 daily kwa ajili ya kula na mafuta ya gari. Saloon anaomba hela na mshahara wake huwa haujulikani unafanya kitu gani. Akiulizwa ugomvi wa kufa mtu
Pole sana mkuu, mtoto umleavyo ndivyo akuavyo...mi nilishamnyoosha mapema kama hela yangu tunaitumia wote jua kuna siku na yako tutaitumia wote 😂😂😂!!!

Ule upuuzi wa changu changu chako chakwetu sijawahi kuunga mkono. So far hakuna longolongo...Ni kuweka misingi mapema tu maana maisha yanabadilika siku unachapa itakubidi uanze kuwa kijakazi wa mkeo ili akusaidie huku ukishuhudia dharau za kila rangi.
 
Utasikia mengi mazuri na mabaya lakini ukweli una pande mbili
1. Kuna idadi ndogo wanaochanga kinachopatikana na maisha yanaenda vizuri kabisa
2. Kuna idadi kubwa ambayo hela ya upande wa mwanamke haionekani na ikitokea ikanunua kitu kitakachofuata ni maneno maneno mengi ili kuonyesha tu alinunua yeye.

Jambo la msingi ni kuwa oa bila kutegemea kwamba kazi yake itakuwa na msaada kwenye mipango yako.
Kama akikubali kuchangia basi epuka kumwachia afanye jambo fulani peke yake, mfano kumwachia kulipa Ada ya shule ya mtoto au kulipa kodi kama umepanga. Mara zote zichanganyeni fedha zenu kwanza ndipo muanze matumizi maana wake zetu hawachelewi kutangaza "Mimi ndio nalipa ada ya mtoto mle ndani"

Nina bahati mmoja huyu mwanamke niliye naye ni mtiifu na anachopata anakileta kama kilivyo na ana kauli yake "tufanye maendeleo kwa ajili ya watoto wetu". Aina hii ya mwanamke atakumsaliti unajisikia vibaya. Sina maana kwamba ni mkamilifu ila kwenye eneo hili yupo vizuri.
Mi nadhani kusaidiana sio jambo baya hasa kama mmekubaliana..

Unaweza kuta mnakubaliana vzr as wife ata cover expenses za nyumbani, chakula, umeme, maji na vingine alafu mume afanye maendeleo as ujenzi ada za watoto ( hii ni kama mume ana kipato kikubwa kumshinda mama)

Tatizo linakuja pale mume anaishia kunywa pombe na marafiki na kuhonga michepuko, maendeleo hayaonekani, hela yake haionekani, yuko radhi kupangia mchepuko full furnitured lkn mwanae anadaiwa ada shuleni, na mke anahangaika peke yake na familia. Hii inaumiza sana na wanawake wengi wapo kwny kundi hili.
 
Bora wewe, kiasi kikubwa cha matumizi yake anajitegemea mwenyewe. Kuna jamaa yangu, mke anachukua 20,000 daily kwa ajili ya kula na mafuta ya gari. Saloon anaomba hela na mshahara wake huwa haujulikani unafanya kitu gani. Akiulizwa ugomvi wa kufa mtu
Na kwanini uulize pesa ya mwanamke inaenda wapi? Kutoa pesa yangu katika mchango wa familia ni mapenzi yangu sio kitu Cha lazima.
 
Back
Top Bottom