Pasco,
Nimeangalia kwa haraka haraka nimeona wana tasnia ya habari wako kama watano hivi, nikiongeza na wale walioteuliwa awamu iliyopita, ninapata mashaka kwamba kuna political corruption ndani ya sekta ya habari na hasa kwenye awamu hii ya JK. Huu ni mfumo mpya wa bahasha za khaki.
Jina lako nasubiri kuliona after 2015, japo nayo ni subjet to certain factors. Hata kama utagoma na kuleta za masikini jeuri, tutakulazimisha!
Mkuu Keil,
Wanahabari nimeona wakilamba UD wa shukrani. Kwanye ule uzi wangu wa mazuri ya JK nilimsifia JK kuwa ni mtu wa shukrani na anakumbuka fadhila, hivyo kamwe hawezi kuwatupa jumla wowote waliomsaidia!.
Muhingo ndie aliyeratibu waandishi wa habari wakati wa kampeni za JK mwenyewe anajiona alistahili kuwa msadizizi wa Salva, usaidizi kapewa Michuzi hivyo angalau amekumbukwa!.
Liana ndiye mhariri wa gazeti la Uhuru ambapo kila negative ya CDM ni front page!.
Kipozi ni mtangazaji mwenye sauti ya mvuto wa dhahabu, ndiye alitangaza zile documentaries za kampeni za CCM, Tido akagoma kuzitangaza TBC, ITV, Star TV na Channel Ten kwa njaa zao wakazikumbatia.
Makunga ni kada wa CCM aliomba kuteuliwa ubunge kura hazikutosha ila ndiye ripota wa kambi ya CCM kwa ITV wakati Ufoo ni kambi ya CDM.
Yule mwandishi dada wa mwisho ni chakula ya wakubwa kama walivyo ma DC kadhaa!.
Kwa upande wangu let me be honest, kama nilikuwa Political Advisor wa ubalozi fulani na package ilikuwa nono, nilikataa kuendelea for reasons, kwenye U-DC ndio ningepewa nini?.
Amini usiamini ningekuwa CCM jina langu lingepelekwa, niwe DC alafu so what?.
Nawaona ma DC kama maboya fulani hivi, hawana lolote la maana la kufanya zaidi ya ku chair hizo kamati za ulinzi na usalama za wilaya!.
Kiukweli mimi binafsi yangu naboreka na kazi yoyote ambayo sio interesting kwangu, nahisi hata ma DC wengi ambao ni action oriented, wanaboreka na kuvumilia tuu wakisubiria labda watapewa u RC!.
Hilo la kusubiria kuliona jina langu 2015, ni kweli subiria na utaliona tuu ila sio kwenye nafasi za shukrani kwa kufagilia au kujikomba komba, ukiwa mkweli daima, utachukiwa tuu na mimi CCM huwa nawaambia ukweli hivyo sitegemei shukrani yoyote toka kwao kama ninavyowaambia CDM ukweli humu jf!.