Wakulima wa vanilla Kagera kutapeliwa na kampuni ya SOSAKA

Mkulima wa vanilla

New Member
Oct 14, 2023
1
0
Sisi Wakulima wa Zao la Vanilla Kagera tulimuuzia Kampuni ya Sosaka Limited iliyopewa vibali na Ofisi ya Mkoa wa Kagera, vanilla zetu mnamo tarehe 19-23 July 2023 lakini mpaka sasa hatujalipwa hela zetu. Sosaka alikua ananunua vanilla kwa bei ya 15,000 Tsh na alikusanya takribani kilo 80,000.

Tunaomba msaada wetu kwani ni kilio kikubwa sana kwetu kwani wakulima kila siku tunasafiri kutoka vijijini kwenda mjini kufuata hela na hakuna msaada.

Tumejitahidi kuwasiliana na ofisi ya mkuu wa mkoa lakini hatujapata msaada wowote mpaka sasa.

Ufafanuzi wa Serikali huu hapa - Serikali yatoa ufafanuzi madai ya Wakulima wa Vanilla kutolipwa zaidi Tsh. Bilioni 1 na Kampuni ya Sosaka Limited
 
Huenda nao wamepata changamoto, process za kusafirisha Vanilla mpaka ifikie kwa final buyer ni very complicated. Hii kitu ni kama dhahabu na hata huiwezi kuihandle bila escort, kama hawawapi ushirikiano ripotini mamlaka husika, wawakilishi wenu wakae mezani mjue nini kinaendelea.
 
Tanzania Mazao Yote Ya Kisiasa Yaepuke Sana Kama Ukoma
Unapoona Siasa Inapenyezwa Ujue Mwisho Wake Ni Kibudu
Vanilla
Korosho
Mbaazi

Dengu
na Mengine Kaa Nayo Mbali
 
Back
Top Bottom