Wajumbe Kamati Kuu CHADEMA wamuonya Zitto.

Wajumbe Kamati Kuu CHADEMA wamuonya Zitto.

tulia utaelewa tu kinachozungumziwa hapa ni kuhusu utaratibu na kanuni idadi ya wajumbe na waliongelea wapi cyo msingi.mikutano yote ya chama nje ya jimbo la mbunge husika huandaliwa na chama.swala la zitto kuongea na wapiga kura wake wa kigoma kas cyo dhambi ila kasulu na kwingineko nje ya utaratibu wa chama ni kosa
Kwani ye kasema yupo kwenye ziara ya kichama? Yupo kwenye ziara Kama za lowassa, hivyo hahitaji ruhusa kutoka CC
 
Namshangaa Zitto kufanya mikutano nje ya jimbo lake la Kigoma Kaskazini kama ambavyo nisingemwelewa Dr. Kitila angeenda Singida

Zitto ameenda Kasulu kama nani?si naibu k/mkuu na kama ni umaarufu wake angeshirikisha CDM makao makuu
mkuu huo ndo ukweli, angalia ziara yake huko kasulu, watu wanatukana viongozi na chama mbele yake, halafu yeye anafurahi, je huko ni kukipenda chama? Hapana zitto ana agenda binafsi, tuweke ushabiki pembeni!
 
Amekwenda Kwa Kuwa Anamashabiki Nanyi Mmewaona, Amekwenda Kuwataka Wananchi Wake Wasiwe Na Mgogolo Na Kamati Kuu Ya Chama. Sikia, Mimi Miaka Ijayo Nitavunja Utawala Mkongwe Wa Magamba Katika Jimbo La Mufindi Kusini, Sasa Nikiwa Mbunge Pale Mnamaanisha Hamta Niruhusu Kuzungumza Na Wana Mufindi Kaskazini Hadi Kibali Kitoke Makao Makuu! Ona Sitakuwa Huru Kuzungumza Na Wanairinga Na Hata Tanzania Kwa Ujumla, It Means Mmenifunga! Huu Ukuritimba Wa Hali Ya Juu Hata Magamba Hawana! Na Kwahili Natafakari Uanachama Wangu Chadema, Nienelee Ama Nitafute Chama Huru?

Nakushauri Tafuta chama kingine kama una tabia za Umimi.
 
ni kipengele kipi cha chadema kina kataza mtu kuongea na wananchi wake?

Chadema huu unyanyasaji mnaomfanyia zitto utawaangamiza.
je mkutano wa kasulu ndo kuongea na wananchi wake? Mkuu weka ushabiki pembeni, angalia kwa macho manne jambo hili utajua kilichojificha nyuma ya pazia!
 
Binafsi nadhani kuna tatizo, siku 14 zimeisha kamati kuu malizeni habari hii. Eidha awe mbunge wa mahakama kama ambavyo imekuwa kwa yule wa CUF au mumsamehe tujue kawashinda kuliko mashindano ya kipuuzi namna hii. Tumechoka na yatosha sasa. "jicho lako likikukosesha ling'oe bora kuingia ukiwa chongo kuliko kuwa nayo yote katika upotevu.
 
zito anajua fika kuwa watamfukuza so anaandaa groundwork ya kitakachofuata baada ya akina slaa kumfuta uanachama..kina slaa nao wanafanya timing hawana uhakika kuwa athari kwa cdm zitakua kubwa kiasi gani ,ndo maana bado wanamlia timing that is why siku 14 zimepita bado kimya..ila telltale sign kuwa watamfukuza inapatikana kwa wapambe akina yerico,ben hawa ni kama mouthpieces za akina slaa na mbowe ,ukiwasoma wanayoyasema ni wazi kuwa watamvua uanachama zito.

Zito nae anajua so nae analainisha maneno huku akiwaotea,that is why hajafanya maamuzi magumu,ila jana kaahidi kurudi kwao pindi wamkimfukuza for more consultation.
mwanzoni sikupenda zitto afukuzwe au kuvuliwa uanachama na chama chake, kwa haya yanayoendelea huko kasulu zitto anajiharibia, huwezi kusema kuwa unakipenda chama huku ukipokelewa na mabango yanayokashifu viongozi wa chama chako na chama na wewe unaangalia tu, zitto anapenda chama kinafiki na sio kimatendo!
 
Humjui zzk unaandika ujinga zzk hata aende hai au karatu atapadua kuliko anavyo pasua kasulu na ujiji.

Mkuu Tatizo Nyinyi Wa Mjini, Ungeishi Kijijini Kidogo Tu Ungejionea, Zitto Anaushawishi Kuliko Mtu Yeyote Unae Mjua Kwa Mikoani. Haujui Chochote Kuhusu Zitto, Kizibo Wewe Rudi Iringa Ebony Wanakuhitaji!
 
Dogo anajipima nguvu na kamati kuu ya chama chake
 
Samaki mjanja majini tu, mtoe nje uone. Mwache awadanganye waha wenzake ila linalokuja laja tu!!!
 
Mkuu Pasco.. mtumzima hatishiwi nyau.. Zitto hata akusanye maelfu.tunacho angalia je taratibu anazifuata??
 
Zitto ana mawazo kama ya Sultani Makenga au ya Koffie Olomide anavaa suti nzuri chini anavaa raba na kofia ya jua .Zitto ana pambana kuonyesha CCM kwamba bado ana kubalika Chadema .Chadema mkateni na kumtosa aende CCM .
 
Hatakiwi kwenda nje ya jimbo lake mpaks awe ameombwa kwa utaratibu maalum

Kama Unacho Andika Kimetoka Katika Katiba Ya Chadema. Basi Mbunge Wa Chadema Ni Zaidi Ya Mfungwa, Kama Kimetoka Katika Akili Yako, Tutarajie Mazito Zaidi Kutoka DEVISION 5!
 
Back
Top Bottom