Elections 2010 Waimbaji wa makundi ya dini kushiriki kampeni

Anfaal

JF-Expert Member
Jan 19, 2010
1,154
113
Hivi karibuni kwenye hutuba ya kuvunja Bunge Rais Kikwete aliwatahadharisha wananchi juu ya kuwatumia dini wakati wa kampeni. Lakini cha kustaabisha makundi ya dini yamekuwa yakiripotiwa kushiriki kikamilifu katika kampeni hizo.

Hoja ni kwamba, hivi Chama fulani cha upinzani, kikitumia hivi vikundi vya dini kwenye kampeni tafsiri yake itakuwa ipi? Ni kwanini basi CCM yenye kujinadi kutenganisha siasa na dini isionyeshe hilo kwenye kampeni? Kwanini watu wanajifanya hawalioni hili?

Na hawa jamaa walivyostrategic vikundi hivi vya dini hutumiwa katika baadhi ya maeneo ya nchi, ni kwanini wasitumie mikoa yoote mpaka Zenji? Tuanzie hapo...
 
Mzee unatania, yaani vikundi vya kwaya vinashiriki katika kampeni ? Hapana, hii ni chini ya mkanda. NEC wako wapi ? Tusipokuwa makini hawa walafi wa madaraka watatugawa. Kusema ukweli hili jambo limeniudhi mpaka ngozi yangu imesisimka.
 
Kumbe huwa kuna wakati macho yako yanaona eeh? Mimi nilifikiri na wewe ni wale binded CCM followers, otherwise good point bro!!!!!
 
Mimi wala hainibabaishi, watz wacha Mungu wale wanaofuata dini kwa vitendo hawazidi asilimia 1. Wangine tunatumia dini kama kisingizio tunapoguswa kwene maslahi yetu. nukta.
 
Bila bongoflava,Komba,Taarab na hizi kwaya CCM kamwe haitopata wasikilizaji.............watu wanajaa kusikiliza burudani.........na wengi wanaletwa kwa mabasi hawaji wenyewe....
 
Mzee unatania, yaani vikundi vya kwaya vinashiriki katika kampeni ? Hapana, hii ni chini ya mkanda. NEC wako wapi ? Tusipokuwa makini hawa walafi wa madaraka watatugawa. Kusema ukweli hili jambo limeniudhi mpaka ngozi yangu imesisimka.

Niogezee tu, kuna gazeti moja limeonyesha viongozi wa dini wakiwa wamejipanga mwanza kumpokea mwenyekiti wa CCM na mgombea urais JK. Wamepewa kipaumbele mstari wa mbele na viongozi wa CCM. Viongozi wa dini wana haki ya kushiriki shughuli za kijamii kama raia wengine, lakini kwanini wasiachwe kujichanganya na wananchi wengine hadi inafikia wanapewa kipaumbele!!!!!!!!!!.
Tumeambiwa tusichanganye dini na siasa, sijui ni haki kuchanganya siasa na dini. Tume ya uchaguzi haya hamyaoni hadi mtakaposikia watu wameanza kuvurugana?
Hivi Dr Slaa akikusanya kwaya za kanisani na kaswida za misikitini na kuanza kuzunguka nazo katika helikopta atakuwa na tofauti gani na JK aliyelakiwa na Maaskofu na mashehe pale Mwanza.
NEC Mnajua hatari za mambo haya au mumekaa kimya kwavile aliyewapa ugali ndiye anayepalilia wa kwake? mnaipeleka wapi nchi!
 
Niogezee tu, kuna gazeti moja limeonyesha viongozi wa dini wakiwa wamejipanga mwanza kumpokea mwenyekiti wa CCM na mgombea urais JK. Wamepewa kipaumbele mstari wa mbele na viongozi wa CCM. Viongozi wa dini wana haki ya kushiriki shughuli za kijamii kama raia wengine, lakini kwanini wasiachwe kujichanganya na wananchi wengine hadi inafikia wanapewa kipaumbele!!!!!!!!!!.
Tumeambiwa tusichanganye dini na siasa, sijui ni haki kuchanganya siasa na dini. Tume ya uchaguzi haya hamyaoni hadi mtakaposikia watu wameanza kuvurugana?
Hivi Dr Slaa akikusanya kwaya za kanisani na kaswida za misikitini na kuanza kuzunguka nazo katika helikopta atakuwa na tofauti gani na JK aliyelakiwa na Maaskofu na mashehe pale Mwanza.
NEC Mnajua hatari za mambo haya au mumekaa kimya kwavile aliyewapa ugali ndiye anayepalilia wa kwake? mnaipeleka wapi nchi!

Tatizo kubwa ni kwamba Rais aliye madarakani sasa hivi ni mgombea wa CCM, hivyo si raisi kutenganisha mambo haya. Nionavyo mimi hao viongozi wa dini walifika hapo kumlaki kama Rais na si mgombea wa urais!
 
Hivi vikundi vya kwaya za dini kama wanaimba nyimbo za dini basi ni tatizo lakini kama wametunga nyimbo za kisiasa za CCM sioni shida. Shida kama wataanza kuimba nyimbo za dini na kumwiingiza JK, hapo ni issue kubwa tu! Mfano, "Yesu tunakushukuru kwa kutuletea Rais kijana na handsome, Dr. JK, kuwa kiongozi wetu bora, Mungu twa kushukuru, Mungu twakuomba umpe afya njema, na kwa maombezi ya Bikira Maria mama wa Mungu..." La! Kama ni wimbo aina hii basi Advocate Tendwa, Jaji Lewis na wengine lazima waindoe CCM kwenye kinyang'aniro hiki mara moja!!!!!!!!!
 
CCM hata wangevunja sheria vipi hakuna wa kuwagusa, NEC ni maliyao, Msajili wa vyama ni kada wao, majeshi yote ya ulinzi na usalama yanapokea amri toka Lumumba. Ila kwa upande wa hao waimbaji wa nyimbo za Injili kwenda kuikampenia CCM ni kuanguka kiroho, kwani Injili ni habari njema iletayo wokovu, sasa wao kujiunga na mafisadi hiyo tena si habari njema, kwani hata hizo hela wanazolipwa hela chafu.
 
Hiyo ni misuse ya kipaji ambacho wamepewa na Mungu ili kumtumikia sasa kama wao wanaitumikia CCM kwa nyimbo na mapambio,hiyo sio njia ya kushiriki katika siasa.Labda kuna mungu kawafunulia katika maono wamfanyie hiyo kazi...,lakini sidhani kwani kuna maono mengi waliofunuliwa na hawakutenda labda kuna kitu kidogo kutoka kwa "mungu" wakishiriki kuimba ktk kampeni
 
Kama kuna sehemu iliniudhi sana, basi ni kuona viongozi wa dini wamejipanga mstari mbele kabisa kumlaki mgombea urais kwa tikiti ya CCM. Sina hakika kama waliingizwa mkenge au walikuwa wanajua wanachokifanya. Hawa ni viongozi ambao waumini wao ni wanachama wa vyama mbali mbali tofauti tofauti. Sasa hawa waumini wachukue uamuzi gani kama tayari viongozi wao wameamua kuegemea upande mmoja. Labda niambiwe kuwa watajipanga hivyo hivyo kuwapokea kina Mutamwega, Prof Lipumba, Dr. Slaa na wagombea wengine wote.

Niogezee tu, kuna gazeti moja limeonyesha viongozi wa dini wakiwa wamejipanga mwanza kumpokea mwenyekiti wa CCM na mgombea urais JK. Wamepewa kipaumbele mstari wa mbele na viongozi wa CCM. Viongozi wa dini wana haki ya kushiriki shughuli za kijamii kama raia wengine, lakini kwanini wasiachwe kujichanganya na wananchi wengine hadi inafikia wanapewa kipaumbele!!!!!!!!!!.
Tumeambiwa tusichanganye dini na siasa, sijui ni haki kuchanganya siasa na dini. Tume ya uchaguzi haya hamyaoni hadi mtakaposikia watu wameanza kuvurugana?
Hivi Dr Slaa akikusanya kwaya za kanisani na kaswida za misikitini na kuanza kuzunguka nazo katika helikopta atakuwa na tofauti gani na JK aliyelakiwa na Maaskofu na mashehe pale Mwanza.
NEC Mnajua hatari za mambo haya au mumekaa kimya kwavile aliyewapa ugali ndiye anayepalilia wa kwake? mnaipeleka wapi nchi!
 
Ni kikundi gani hicho cha kwaya kimetumika kwenye kampeni?? Itabidi niongee na Rozi Mhando awe anaambatana na Dr Slaa kutoa burudani wakati wa kampeni kama hii maneno inaruhusiwa. Malaria Sugu a.k.a Jeykey uko wapi kutoa comments zako katika hili??? Kama ingetokea kwa CHADEMA ungehukumu haraka kuwa CHADEMA ina udini.
 
Hivi karibuni kwenye hutuba ya kuvunja Bunge Rais Kikwete aliwatahadharisha wananchi juu ya kuwatumia dini wakati wa kampeni. Lakini cha kustaabisha makundi ya dini yamekuwa yakiripotiwa kushiriki kikamilifu katika kampeni hizo. Hoja ni kwamba, hivi Chama fulani cha upinzani, kikitumia hivi vikundi vya dini kwenye kampeni tafsiri yake itakuwa ipi? Ni kwanini basi CCM yenye kujinadi kutenganisha siasa na dini isionyeshe hilo kwenye kampeni? Kwanini watu wanajifanya hawalioni hili? Na hawa jamaa walivyostrategic vikundi hivi vya dini hutumiwa katika baadhi ya maeneo ya nchi, ni kwanini wasitumie mikoa yoote mpaka Zenji? Tuanzie hapo...
Ni kweli FLORA Mbasha na kundi lake walishiriki kampeni za Mwanza. Angalia kwenye blog ya michuzi.
Hata hawa vijana wa Bongo Flavour badala ya kuwa kioo cha jamii nao wanaambatana na Kikwete kwenye kampeni. Ilitakiwa katika miziki yao walenge jamii nzima na siyo mgombea au chama fulani. Nao sasa wamekuwa TOT (wanamilikiwa na CCM?) Je Sheria za kampeni zinafuatwa kwa hili?
 
Ni kikundi gani hicho cha kwaya kimetumika kwenye kampeni?? Itabidi niongee na Rozi Mhando awe anaambatana na Dr Slaa kutoa burudani wakati wa kampeni kama hii maneno inaruhusiwa. Malaria Sugu a.k.a Jeykey uko wapi kutoa comments zako katika hili??? Kama ingetokea kwa CHADEMA ungehukumu haraka kuwa CHADEMA ina udini.

MALARIA SUGU yuko lupango na akiwa huku alizirai saa 9.32 siku ya jumamosi
 
Mimi wala hainibabaishi, watz wacha Mungu wale wanaofuata dini kwa vitendo hawazidi asilimia 1. Wangine tunatumia dini kama kisingizio tunapoguswa kwene maslahi yetu. nukta.

uko sahihi mkuu,laiti Mungu angetupa japo jicho la roho kidogo hata hao waliotumika na ccm kukampeni si wana dini
bali watafuta vya ufalme wa dunia tu, hawana lolote, nyimbo hizo siyo mahali pake huu ni uhuni wazi wazi
 
Hivi karibuni kwenye hutuba ya kuvunja Bunge Rais Kikwete aliwatahadharisha wananchi juu ya kuwatumia dini wakati wa kampeni. Lakini cha kustaabisha makundi ya dini yamekuwa yakiripotiwa kushiriki kikamilifu katika kampeni hizo. Hoja ni kwamba, hivi Chama fulani cha upinzani, kikitumia hivi vikundi vya dini kwenye kampeni tafsiri yake itakuwa ipi? Ni kwanini basi CCM yenye kujinadi kutenganisha siasa na dini isionyeshe hilo kwenye kampeni? Kwanini watu wanajifanya hawalioni hili? Na hawa jamaa walivyostrategic vikundi hivi vya dini hutumiwa katika baadhi ya maeneo ya nchi, ni kwanini wasitumie mikoa yoote mpaka Zenji? Tuanzie hapo...

mjomba ck hizi sio zile za kale watu walipokuwa wanamwimbia Mungu kwa ajili ya utukufu wake....
ck hizi wapo kimaslahi zaidi kwani Gospel zimeonekana zinalipa kuliko miziki mingine. Hivyo hao hawana wito wa kumtumikia Mungu
 
Hao ndio CCM, wazee wa double standard..kujisaidia ajisaidie kuku akijisaidia bata kahara. Hapo hujagusa matumizi ya rasilimali za serikali kwa ajili ya chama. Hapo hujagusa utekaji nyara wa ziara za kiserikali kuguezwa kuwa za chama! Safari ni ndefu lakini tutafika tu!
 
Dada mbasha mimi nikiwa kama mmoja kati ya fan wako nimesikitishwa sana na kitendo cha wewe kukubali kuchanganya siasa na dini wakati hata yesu mwenyewe hakupenda vitu ivyo vichanganywe. nakumbuka alisema vya kaisari mpe kaisari na mungu mpe mungu.

how can submerge urself like that sisiter, u have disapointed alot of ur fans and beginning to wonder what will happen next. are u goint to be Pastor Chrispher Mtikila. manake hatima ya kuchanganya mambo haya mawili siku zote inaishiaga kubaya.

CHONDECHONDE





MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Dada mbasha mimi nikiwa kama mmoja kati ya fan wako nimesikitishwa sana na kitendo cha wewe kukubali kuchanganya siasa na dini wakati hata yesu mwenyewe hakupenda vitu ivyo vichanganywe. nakumbuka alisema vya kaisari mpe kaisari na mungu mpe mungu.

how can submerge urself like that sisiter, u have disapointed alot of ur fans and beginning to wonder what will happen next. are u goint to be Pastor Chrispher Mtikila. manake hatima ya kuchanganya mambo haya mawili siku zote inaishiaga kubaya.

CHONDECHONDE

MUNGU IBARIKI TANZANIA

1. Njaa si imani, ni siasa
2. Angeimbia vyama vingine ni udini
 
Back
Top Bottom