Tatizo kubwa ni kwamba Rais aliye madarakani sasa hivi ni mgombea wa CCM, hivyo si raisi kutenganisha mambo haya. Nionavyo mimi hao viongozi wa dini walifika hapo kumlaki kama Rais na si mgombea wa urais!
Hivi vikundi vya kwaya za dini kama wanaimba nyimbo za dini basi ni tatizo lakini kama wametunga nyimbo za kisiasa za CCM sioni shida. Shida kama wataanza kuimba nyimbo za dini na kumwiingiza JK, hapo ni issue kubwa tu! Mfano, "Yesu tunakushukuru kwa kutuletea Rais kijana na handsome, Dr. JK, kuwa kiongozi wetu bora, Mungu twa kushukuru, Mungu twakuomba umpe afya njema, na kwa maombezi ya Bikira Maria mama wa Mungu..." La! Kama ni wimbo aina hii basi Advocate Tendwa, Jaji Lewis na wengine lazima waindoe CCM kwenye kinyang'aniro hiki mara moja!!!!!!!!!
kwa Dr. Slaa sawa ila kwa Mbasha hapana, wanafiki wa kubwa nyie
........Huyu mbona yupo kibiashara zaidi!!! Usione watu wanakimbilia kuimba nyimbo za injili wengine ni kazi hizo jamani.
Yeye na mumewe kuimba hiyo ndio kazi yao inayowaweka mjini......hivyo msione ajabu kuamua kujiingiza kuimba hadi kwenye siasa hiyo yote ni kutafuta pesa.
Ni mjukuu wa Nchungaji Mozes Kulola wa Tanzania Assemblies of GOD muulizeni askofu wake mkuu Dr Barnabas Mtokambali ameridhia hali hiyo?
Nimempigia simu Dakta Slaa hajapokea lakini nilitaka nimshauri aende ZANZIBERI akakodi kundi la KASWIDA lije limwimbie jumapili jangwani kuleta burudani na kukifanya chama kikubalike na waislam
Na alivyojichubua sasa utafikiri anataka kuwa mtasha!!
Ndio matatizo yenu. Lkini lazima muelezwe ukweli. Udini Upo kwa Dakta slaa lakini Kikwete akiimbiwa mapambio na wainjilishaji, sio mdini, MAPEPO WAKUBWA NYIE! Mshindwe na mlegee!
Hayo ya CUF sina muda nayo na wala hayanihusu. Kwakuwa wewe ni mwanachama wa CUF nashukuru kwa kuuweka ukweli hadharani.
.........Tena kaupitisha haswa mkorogo hilo halijifichi........kipindi anatoa ile single yake ya kwanza ya jipe moyo hakuwa na light skin kama alivyo sasa. Tena kipindi hicho nilimuona live pale mikocheni B Assemblies of God alikuwa na rangi ya kawaida tu maji ya kunde.Kazi kweli kweli sijui hawaoni aibu wanavyojikoboa.
Labda wameona ili mkuu asianguke tena basi watafute mwimbaji wa kilokole aimbe kwanza kabla mkuu wa kaya hajahutubia.
All in all it is disappointing kuona mwimbaji wa nyimbo za injili anashabikia kwa uwazi mgombea mmoja. Mwimbaji wa injili ni kama mhubiri na ukiona mhubiri anapanda jukwaani kumpigia kampeni mtu basi ujue hapo injili inaanza kuchakachuliwa. Huenda binti ameahidiwa viti maalumu na akaamua kumsaliti Bwana kama Yuda Iskariote