Wahitimu wengi wa Vyuo Vikuu vya Kitanzania hawawezi kufanya mjadala kama huu wa watoto wa shule

Mambo hubadilika kila nyakati....saiv kuna internet ambayo imepunguza kwa kiasi kikubwa mambo ya mijadala ya face to face lakin pia internet imesababisha vijana wa sasa tuache kujieleza Sana tunavohitaji kitu fulan mfano; mtu unaweza kuhtaji kitabu flan badala ya kwenda library au kwa teacher saiv unaweza kudownload, lakn pia hata kukaa na watu mtaani(wazee, masela n.k ) kumepungua sababu ya internet. Hii inasababisha kijana akose public speaking skills na kukosa uwezo wa kujieleza mbele ya kadamnasi....turudi nyuma kwa hao vijana wa zaman, hakuna simu hakuna internet ,ukitaka kitu chochote ni lazma ufanye physical contact na mhusika, hii iliwajengea public speaking skills na uwezo mzuri wa kujieleza mbele za watu.
Hivyo Basi, vijana wa sasa hiv tujitahidi kucontact na watu face to face tupate walau confidence ya kueleweka mbele ya umati wa watu.practice make perfect.
 
Shule bora huwa zinatilia sana mkazo uwezo wa kudebate, sana. Bahati mbaya shule zetu zinazalisha waoga na wafyata mkia. Wasioweza kuhoji, wanaosubiria labda mambo yatakuwa mazuri yenyewe.
 
Siasa imevamiwa na watu wasio na uwezo kichwani..siasa imegeuzwa kuwa ajira badala ya tanuru la kuibua hoja zilizoshiba...
 
Usisahau kitu kinaitwa personality, kuna watu kulingana na walivyoumbwa, kuongea huwa ni tatizo hata kama wana hoja.

Jamii ya wasomi nchi yoyote ni mchanganyiko wa wazungungumzaji wazuri, waadishi wazuri au wenye sifa zote mbili.

Kwa maoni yangu ni vizuri tukawapima wasomi wetu kwa kuzingatia ujuzi wa walichosomea maana kuna fani nyingine hazimhitaji mtu kuwa mzungumzaji mzuri ili kuleta matokeo.
 
Tena walikuwa wanataka wapikiwe mayai kutoka ulaya,ya bongo hawakuyataka,
Alisimulia Mzee samwel sita alipokuwa mwanafunzi pale UDSM,kulinganisha 1957 na leo,huwatendei haki vijana wetu,
Mi Mzee wangu,siku anamaliza shule,Gari ya Serikali ipo nje inamsubili aende akaanze kazi,hata matokeo hayajatoka,leo hii una masters na kazi huna.
Mama yangu kasoma middle skuli,kipindi hicho,Waalimu wazungu,leo hii anaongea kimombo hata Profesa wa chuo kikuu hafikii hiyo fluence,may be Mkapa tu.
Unasoma kwa tabu,ukikosa mkopo,mpaka wazazi wajipige pige
 
Wewe kama mwalimu wa chuo ulichukua hatua gani kutatua hii changamoto? Hatua ulizochukua zilifanikiwa kiasi gani?
Tatizo kama hili halitatuliwi na mtu mmoja ndugu RRONDO, ni kubwa na lina mizizi mirefu. Kama mtoto hataandaliwa vizuri chini (Elementary, Primary & Secondary levels) usitegemee kama atafanya makubwa chuo kikuu. Atafaulu na kupata madaraja ya juu lakini uwezo wa kukabiliana na mazingira yake utakuwa hafifu sana...
 
Nakubaliana na wewe, uwezo wa kuzungumza na kuandika hutofautiana. Lakini hii haimaanishi kwamba mtu aliyesoma ashindwe kabisa kuwasilisha mawazo yake kwa kupitia hoja. Lakini pia mtu asipokuwa mzungumzaji mzuri basi hata utendaji wake huzungumza, kitu ambacho Tanzania ya leo kinapotea sana. Kinachoshanganza, hata ukizungumza na mtu (One to One) unakuta anapata shida....
 
Unazungumzia hawa wanaomaliza TEKU na St. John?
Wahitimu wengi wa vyuo vikuu vya kitanzania hawawezi kufanya mijadala mizuri. Kama wakifanya basi itakuwa ni mijadala ya kisiasa ambayo ni ya ndani ya nchi, lakini ukiwachukua leo hii ukawaweka vijana wa UDSM (Top Brass ya nchi) wafanye mjadala na vijana wa Pretoria, Zimbabwe, Abuja au Accra ni wachache sana watakaofanya vizuri. Hili nimeliona kwa macho yangu na kulithibitisha.........
 
Wanafunzi wa UDSM wao wanaona sifa kuongea broken English ila kudebate hawawezi kabisa maana uelewa wao ni mdogo mno. Utakuta mtu kajuwa Kiingerza miaka 6 iliyopita akiwa chuoni, leo hii hajuwi Kiswahili. Kwa kweli wanachekesha mno.
 
Wanafunzi wa UDSM wao wanaona sifa kuongea broken English ila kudebate hawawezi kabisa maana uelewa wao ni mdogo mno. Utakuta mtu kajuwa Kiingerza miaka 6 iliyopita akiwa chuoni, leo hii hajuwi Kiswahili. Kwa kweli wanachekesha mno.
Kimtazamo wangu hapa kuna mawili: Kuna vijana wengi wanajitahidi sana, wanakuwa na uelewa mzuri wa vitu lakini utaalamu (Skills) wa kujieleza hawakujengewa tokea wanasoma shuleni. Siyo rahisi kuwa na mzungumzaji mzuri kama hukujengewa msingi mzuri. Hoja hii ameitoa Mkaruka hapo juu.

Kuna Debates, Morning Speeches, Poetry, Play and Drama na mambo mengnei sana ambayo yanapuuzwa leo lakini yanamsaidia sana mtoto katika kumjengea ujasiri (Confidence) na kumfundisha taaluma ya uzungumzaji mzuri. Mimi wakati nasoma tumefanya Play and Drama, Debates, tumeandika Poetry na kufanya mengineyo ambayo kiukweli yalinisaidia sana,....

Lakini pili, mjadala unaweza ukakushinda kama una uelewa mdogo. Kuna watoto unaweza kutana nao, wanaongea kiingereza hicho hadi utakimbia lakini uelewa wao wa mambo uko finyu hivyo humzuia kujenga hoja ipasavyo au mara nyingine ujasiri. Japo huyu yuko kwenye nafasi nzuri endapo atafanya jitihada.

Mwisho kabisa naamini ili wasomi tuweze kufanya vizuri mijadala yenye tija kitaifa, tunahitaji tufahamu vizuri jinsi ya kuwasilisha hoja, lakini pia tuwe na uelewa mpana wa mambo ambayo tunataka kuyajadili.....
 
Wapo watu wanajua kujenga hoja hata kwa sasa, tatizo ni kwamba 'hakuna wanunuzi wa hoja'.

Maana yangu ni kwamba, asilimia kubwa ya watanzania wa sasa hawapo tayari hata kusikiliza hoja, wengi wao amasa zao zipo kwenyr habari za kutekenya na mlipuko

Kwa mazingira kama hayo usitegemee kupata ile taste ya hoja za kisomi. Hapa enyewe jamii forum unaweza kutoa hoja lakini ukaishia kutukanwa pasipo sababu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…