Wahitimu wa vyuo waokolewe

Wahitimu wa vyuo waokolewe

Ndio hicho kitu nilikuwa namuelekeza yeye anafikiri labda kwenye chuo cha udaktari kuna kozi inaitwa udaktari bingwa.
Hajui kwamba lazima upitie MD then badae unajiendeleza halafu unaspecialize kwenye kieneo kimoja unaweza kuspecialize kwenye mifupa,sikio(meno),ngozi na maeneo mengine.
eti course ya udaktari ya bingwa khaaaa
 
Tulikuwa na mradi wa kusaidia vijana waliohitimu kozi fulanifulani kupata ajira. Tulituma tangazo, na vijana kadhaa wakajitokeza. Baada ya mchujo, tukapata vijana kadhaa kwenda kujitolea.

Katika wale waliochaguliwa, ilibidi kurudi kwenye taasisi tulizoomba nafasi kwa wahitimu, kwani baadhi walikuwa wakikataa nafasi hizo, walizoziomba wenyewe!

Sehemu ya kazi ilikuwa ni mjini kwenye viyoyozi na porini pa hapa kazi tu. Wazoefu wa sekta waliwashauri vijana wajitose kwenda maporini.

Tunashukuru wale vijana walioenda kujitolea, hawakutuangusha. Walichapa kazi. Wengi miongoni mwao waliishia kupata ajira walipokuwa wakifanyia kazi, na wengine taasisi jirani. Wengine walikataa ajira kwa sababu zao binafsi. Na wengine waliutumia uzoefu walioupata huko kufanya shughuli nyingine. Kwa ujumla zoezi lilikuwa na mafaniko makubwa.

Pengine ipo haja kuendeleza zoezi hilo kwa sekta ile, na hata kwa sekta nyinginezo.
 
Mkuu laiti kama ungejua situation za vijana hao usingekua unaongea hvyo...na kibongo bongo skuhiz ukijifanya unapenda ku voluntere utabak unatumikishwa weeeee had akili ikukae sawa na kaz hupat..
Siku hizi ukienda kujitolea ndio basi tena hawaajiri mtu wanakutumia miaka yote bila mshahara.
 
Ona sasa akili za wabongo hizi
Ndiyo maana wazungu wanatudharau
wazungu ndo wana akili zaid? wao wana utamadun wao na wabongo tuna wetu, yan niuwe watoto kisa cna kazi? hyo akil kwel?
 
Tatizo tunang'ang'ania mijini, ukinunua kile kifaa cha kupimia na ukaweka kiti hapo nje....wagonjwa watajileta wenyewe; fani za afya kwa asilimia kubwa kwa mtu makini ni rahisi kujiajiri,na wanahitajika sana.
Hivi huyu jamaa anaandika nini 👆👆
 
Kuna misemo mikuu ukiangalia sana taarifa ya habari hasa zikitokea ku delay kwa vitu.

1.Watumishi hawatoshi ndio maana tunakwama.

Sijawahi kuelewa mapaka leo hii huwa wanaamanisha nini tukiona vijana wanahangaika huku mitaani.

Tupunguze roho mbaya na ubinafsi sisi tulio makazini.

Nakumbuka 2006 na sita kuna HR mmoja alikuwa anaita vijana kusaidia kupanga panga files kwa ofisi na ndiko huku wengi tulijua connections za kazi.Sasa watu kama hawa ni wa kuhesabu sana.

Hizi recruitments agencies pia kuna baadhi zinaharibu sana ndoto za vijana wetu..zimejaa dharau?na kila aina ya maudhi.


Kijana usibague kazi hata kama umesoma kitu gani..muda unakwenda na unahitaji kujikwamua kiuchumi.Tumia fursa zilizopo kwa uwezo wako na umakini wako.

Nafahamu kuna watu wanapitia mazingira magumu hata ya kukosa nauli.Ukisaidiwa saidia wengine kwa kadri unavyoweza.
 
Kuna misemo mikuu ukiangalia sana taarifa ya habari hasa zikitokea ku delay kwa vitu.

1.Watumishi hawatoshi ndio maana tunakwama.

Sijawahi kuelewa mapaka leo hii huwa wanaamanisha nini tukiona vijana wanahangaika huku mitaani.

Tupunguze roho mbaya na ubinafsi sisi tulio makazini.

Nakumbuka 2006 na sita kuna HR mmoja alikuwa anaita vijana kusaidia kupanga panga files kwa ofisi na ndiko huku wengi tulijua connections za kazi.Sasa watu kama hawa ni wa kuhesabu sana.

Hizi recruitments agencies pia kuna baadhi zinaharibu sana ndoto za vijana wetu..zimejaa dharau?na kila aina ya maudhi.


Kijana usibague kazi hata kama umesoma kitu gani..muda unakwenda na unahitaji kujikwamua kiuchumi.Tumia fursa zilizopo kwa uwezo wako na umakini wako.

Nafahamu kuna watu wanapitia mazingira magumu hata ya kukosa nauli.Ukisaidiwa saidia wengine kwa kadri unavyoweza.
Kuna kazi za kutumia akili nyingi sana
Kuna kazi za kutumia akili nyingi nguvu kidogo
Kuna kazi za kutumia akili kidogo nguvu nyingi
Kuna kazi za kutumia nguvu nyingi

Sasa hapo,kijana anatakiwa aangalie ni ipi itakayomfaa kwa muda husika
 
Kuna kazi za kutumia akili nyingi sana
Kuna kazi za kutumia akili nyingi nguvu kidogo
Kuna kazi za kutumia akili kidogo nguvu nyingi
Kuna kazi za kutumia nguvu nyingi

Sasa hapo,kijana anatakiwa aangalie ni ipi itakayomfaa kwa muda husika
Ni kweli kabisa mkuu.Tuwe na moyo wa kuto dharau kazi kabisa.

Kuna kipindi niliangalia juzi kinaitwa POINTLESS ni maswali maswali kwa huko mbele.

Jamaa aliulizwa unafanya nini ukiachana na Mechanics unayosoma.Jibu lake ni Bartender na anasema inampa hela ya kujiendeleza na kukidhi hali za maisha kwa mujibu wa ENGLAND.

Niliwahi pia kutana na IRISH mmoja alikuwa mwalimu wangu kwangu kwa 1Month.

MSc in Computer Science and BSc in Doctor of Medicine.
Nje ya shughuli hizo zote bado pia anachora sana na kutembelea familia za watu wanaotumia dawa za kulevya kwa kila week.

Wenzetu wana shughuli nyingi sana ambazo ki africa nyingi tunaziita za kipuuzi.Lakini hayo yote hutokana na dharau na kutothamini umuhimu wa kila jambo hata kama ni dogo kwa kiasi gani.

Ukiweza kufanya jambo fanya..maana malengo ya kusoma ni kujikomboa kiuchumi,afya,malazi na mavazi.
Sasa kama unaona unao uwezo wa kufanya kazi katika makundi kama uliyo sema hapo juu mkuu.Kikubwa heshima na nidhamu kwa kila unachofanya.

Weka uaminifu wa kazi zako na utulivu.Hakuna pesa nyepesi hela haimfuati mtu anayelala ana asiyetaka kuitumia akili yake..
 
Ni kweli kabisa mkuu.Tuwe na moyo wa kuto dharau kazi kabisa.

Kuna kipindi niliangalia juzi kinaitwa POINTLESS ni maswali maswali kwa huko mbele.

Jamaa aliulizwa unafanya nini ukiachana na Mechanics unayosoma.Jibu lake ni Bartender na anasema inampa hela ya kujiendeleza na kukidhi hali za maisha kwa mujibu wa ENGLAND.

Niliwahi pia kutana na IRISH mmoja alikuwa mwalimu wangu kwangu kwa 1Month.

MSc in Computer Science and BSc in Doctor of Medicine.
Nje ya shughuli hizo zote bado pia anachora sana na kutembelea familia za watu wanaotumia dawa za kulevya kwa kila week.

Wenzetu wana shughuli nyingi sana ambazo ki africa nyingi tunaziita za kipuuzi.Lakini hayo yote hutokana na dharau na kutothamini umuhimu wa kila jambo hata kama ni dogo kwa kiasi gani.

Ukiweza kufanya jambo fanya..maana malengo ya kusoma ni kujikomboa kiuchumi,afya,malazi na mavazi.
Sasa kama unaona unao uwezo wa kufanya kazi katika makundi kama uliyo sema hapo juu mkuu.Kikubwa heshima na nidhamu kwa kila unachofanya.

Weka uaminifu wa kazi zako na utulivu.Hakuna pesa nyepesi hela haimfuati mtu anayelala ana asiyetaka kuitumia akili yake..
Cha kujifunza hapa, hatima ya maisha yako, yako mikononi mwako; ni kujaribu kutumia elimu ya darasani, kama imeshindwa kufanya kazi tumia kipaji ulichonacho, vinginevyo tutakuwa tunalaumu mpaka tunazeeka hakuna cha maana tulichofanya.
 
Back
Top Bottom