Tulikuwa na mradi wa kusaidia vijana waliohitimu kozi fulanifulani kupata ajira. Tulituma tangazo, na vijana kadhaa wakajitokeza. Baada ya mchujo, tukapata vijana kadhaa kwenda kujitolea.
Katika wale waliochaguliwa, ilibidi kurudi kwenye taasisi tulizoomba nafasi kwa wahitimu, kwani baadhi walikuwa wakikataa nafasi hizo, walizoziomba wenyewe!
Sehemu ya kazi ilikuwa ni mjini kwenye viyoyozi na porini pa hapa kazi tu. Wazoefu wa sekta waliwashauri vijana wajitose kwenda maporini.
Tunashukuru wale vijana walioenda kujitolea, hawakutuangusha. Walichapa kazi. Wengi miongoni mwao waliishia kupata ajira walipokuwa wakifanyia kazi, na wengine taasisi jirani. Wengine walikataa ajira kwa sababu zao binafsi. Na wengine waliutumia uzoefu walioupata huko kufanya shughuli nyingine. Kwa ujumla zoezi lilikuwa na mafaniko makubwa.
Pengine ipo haja kuendeleza zoezi hilo kwa sekta ile, na hata kwa sekta nyinginezo.