Wafanyabiashara wote Moshi wamegoma

Wafanyabiashara wote Moshi wamegoma

Magesi

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2012
Posts
2,587
Reaction score
578
Wakuu ule Mwendelezo wa Wafanyabiashara Nchini kugomea Mashine za utoaji risiti EFD,Leo Unafanyika katika Mji wa Moshi.Pia wanataka Kesi iliyofunguliwa dhidi ya Mwenyekiti wao Taifa ifutwe.

Tokea Asubuhi Maduka hayajafunguliwa Mpaka Muda Huu Tofauti na siku Nyingine.

Kuna Taarifa Za Mikoa Mingine nako Wafanyabiashara wamegoma.
 
Wakuu ule Mwendelezo wa Wafanyabiashara Nchini kugomea Mashine za utoaji risiti EFD,Leo Unafanyika katika Mji wa Moshi.

Tokea Asubuhi Maduka hayajafunguliwa Mpaka Muda Huu Tofauti na siku Nyingine.
Bado asubuh sana
 
Wakuu ule Mwendelezo wa Wafanyabiashara Nchini kugomea Mashine za utoaji risiti EFD,Leo Unafanyika katika Mji wa Moshi.

Tokea Asubuhi Maduka hayajafunguliwa Mpaka Muda Huu Tofauti na siku Nyingine.

Hata dar leo kuna mgomo
 
Moshi maduka hufunguliwa kuanzia saa 2:30 mpaka saa 3 ..... sasa wewe saa 1:42 hii inakuwaje kuna mgomo
 
Chalii angu huo mgomo ni nchi nzima na kisa ni kesi waliyofungua serekali dhidi ya mwenyekiti wa wafanyabiashara na mgomo utakuwa kila siku ya kesi hadi siku wafute kesi au ifike mwisho
 
wafunge tu tutatumia vyakula vya mashambani mwetu.
 
Chalii angu huo mgomo ni nchi nzima na kisa ni kesi waliyofungua serekali dhidi ya mwenyekiti wa wafanyabiashara na mgomo utakuwa kila siku ya kesi hadi siku wafute kesi au ifike mwisho

mimi nashauri serikali wamfunge huyu jamaa tuone kama watafunga biashara kila siku.
 
Moshi maduka hufunguliwa kuanzia saa 2:30 mpaka saa 3 ..... sasa wewe saa 1:42 hii inakuwaje kuna mgomo

Achana na huyo mwehu. Ni huyo huyo mfanyabiashara mwenye kesi kila ikifika siku yake ya kwenda mahakamani huwa anajipostia vitu humu.Anajitekenya na kujichekesha mwenyewe.
 
Mwanza nako ni mwendo huo huo kuna mgomo mkubwa sana kuna hatari hata daladala nazo zikagoma kuanzia saa nne asubuhi.
 
mimi nashauri serikali wamfunge huyu jamaa tuone kama watafunga biashara kila siku.
Tangu Mwigulu aingie wizara ya fedha amesababisha migogoro na wafanyabiashara,nashauri aondolewe wizarani na huyu Mkiti aachiwe guru. Halafu eti Mwigulu anataka urais! Pambaf.
 
wakuu ule mwendelezo wa wafanyabiashara nchini kugomea mashine za utoaji risiti efd,leo unafanyika katika mji wa moshi.

Tokea asubuhi maduka hayajafunguliwa mpaka muda huu tofauti na siku nyingine.

wachaga moshi wagome KUFANYA BIASHARA? Wakigoma najiondoa jamii forums naapa.Migomo ya kufunga biashara ni kwa ajili ya vikabila visivyojitambua vya mikoa mingine visivyojua maana ya biashara ni nini.Moshi wagome chezea wachaga wewe huwajui.

Ulishawahi sikia hata maandamano ya fujo moshi? Hawataki kuharibu biashara maandamano yote ya fujo ni kwa makabila mengine.Mwanza kwa wasukuma,dar kwa wazaramo,Arusha kwa wamasai na wameru,KIGOMA kwa waha,mbeya kwa wanyakyusa,Iringa kwa wahehe n.k sio moshi.
 
hakuna mgomo mi ndo sasa nafungua duka apa nchi ya porojo tu hi
 
Wakuu ule Mwendelezo wa Wafanyabiashara Nchini kugomea Mashine za utoaji risiti EFD,Leo Unafanyika katika Mji wa Moshi.

Tokea Asubuhi Maduka hayajafunguliwa Mpaka Muda Huu Tofauti na siku Nyingine.

Serikali hii imezidi ulegevu.Hawa watu wanatakiwa kutandikwa viboko na si kuwalealea kijinga.Hawana hoja ya mşingi na wamezoea kukwepo kodi huku wakituumiza walajı kwa bei kubwa za bidhaa na huduma zao.Nchi wafanyabiashara wengi wanakwepa kulipa kodi stahiki na sasa inaonekana kuzoeleka na kujiona hawapaswi.Wafanyakazi wanabanwa kodi na wananchi tunauziwa bıdhaa na huduma kwa bei kubwa ikıamınika kuwa sehemu itakuwa kodi.Hawa jamaa ni wahunı na majambazi sawa na mafisadi wa kısıasa, tusiwaunge mkono kabisa.
 
Wakuu ule Mwendelezo wa Wafanyabiashara Nchini kugomea Mashine za utoaji risiti EFD,Leo Unafanyika katika Mji wa Moshi.

Tokea Asubuhi Maduka hayajafunguliwa Mpaka Muda Huu Tofauti na siku Nyingine.

Serikali ifanye maamuzi magumu; futa leseni zote wanaotaka kufanya biashara na kulipa kodi za serikali waombe leseni upya
 
Moshi maduka hufunguliwa kuanzia saa 2:30 mpaka saa 3 ..... sasa wewe saa 1:42 hii inakuwaje kuna mgomo

Amestuka usingizini ngoja akaoge aswaki mpk anywe na chai usingizi utakuwa imeisha.
 
Ujinga mtupu,na wagome tu watakula jeuri yao.wangegoma wa sokoni sawa,lakini hao wa maduka? Tena wagome mwezi mzima.
 
Serikali hii imezidi ulegevu.Hawa watu wanatakiwa kutandikwa viboko na si kuwalealea kijinga.Hawana hoja ya mşingi na wamezoea kukwepo kodi huku wakituumiza walajı kwa bei kubwa za bidhaa na huduma zao.Nchi wafanyabiashara wengi wanakwepa kulipa kodi stahiki na sasa inaonekana kuzoeleka na kujiona hawapaswi.Wafanyakazi wanabanwa kodi na wananchi tunauziwa bıdhaa na huduma kwa bei kubwa ikıamınika kuwa sehemu itakuwa kodi.Hawa jamaa ni wahunı na majambazi sawa na mafisadi wa kısıasa, tusiwaunge mkono kabisa.

Well said.
 
Back
Top Bottom