Wafanyabiashara wote Moshi wamegoma

Wafanyabiashara wote Moshi wamegoma

Hayo hayo unayojiuliza ndiyo yanayosababisha watu wanagoma ,wafanyabiashara wanatofautiana kuna Mzee Azam,Mengi,na wengine wakubwa wakubwa,hao machine kwao si issue.sasa mtu Ana mtaji wa sh milioni Sita unamwambia anunue machine,wapi na wapi.

Mfanyakazi mwenye mshahara wa ml 3.6 kwa mwaka analipa kodi, iweje mtu mwenye mtaji wa mil 7 aone ni shida?Mtaji wa milioni 7 unatengeneza faida ya laki3 kwa mwezi km ulivyo mshahara wa mfanyakazi huyo mlipa kodi?Milion 7 ina uwezo wa kuzaa kwa uchache mil 2 kıla mwezi.Lıpa kodi bwana, hela ya kununulia mashne si mnarudishıwa?Swala hapa sio gharama za mashne, ni kwamba sasa mnaona kubanwa ili mlipe kodi stahki.Mlizoea kuhonga maafisa wa TRA na kuongopa mauzo.Kazia hapohapo bwn RISHED.
 
Wakuu ule Mwendelezo wa Wafanyabiashara Nchini kugomea Mashine za utoaji risiti EFD,Leo Unafanyika katika Mji wa Moshi.Pia wanataka Kesi iliyofunguliwa dhidi ya Mwenyekiti wao Taifa ifutwe.

Tokea Asubuhi Maduka hayajafunguliwa Mpaka Muda Huu Tofauti na siku Nyingine.

Kuna Taarifa Za Mikoa Mingine nako Wafanyabiashara wamegoma.

kaka sema wafanyabiashara ndogondogo na wakati wagoma maana wale wakubwa wanaoongoza kukwepa kodi bado maduka yako wazi kama nakumat,kilimanjaro supermaket,panone a.ka ngiloi n.k. sisi wenye mitaji ya mikopo midogo tunaokatwa kodi kubwa ndo tumegoma na tamko toka halmashauri kupitia ofisi ya biashara wamesema tunafutiwa leseni zzetu za biashara.... Tanzania shikamoo
 
Samahani nilitaka kumjibu mwingine aliyesema wafanyabiashara elimu ndio inawasumbua ,wakati wenye elimu kibao wameajiriwa na wasio na elimu.samahani tena mkuu

Ndio tafsirı nyepesi.Ukıona umeajirı maana yake huna elimu ya kukuwezesha kumudu majukumu ya biashara ufanyayo.
 
Faida inayopatikana kwenye mashirıka ya umma ni kwa manufaa ya serikali hyohyo tofauti na mtu binafsi.

lakini kuendelea kutumia risit za karatasi badala ya EFD ni mwanya wa upotevu. ni vigumu serikali kujua kiasi kilichokushanywa. Wakitumia EFD taarifa zitapatikana kwa urahisi
 
Watu walipe kodi. Walimu wao na mshahara mdogo wanalipa iweje wao wasilipe??? Kukataa mashine za efd ni janja yao ya kukwepa kulipa malipo stahiki
 
Back
Top Bottom