Wabongo acheni kukariri maisha

Kwahyo sisi wenye familia hatuna majukumu, kisa tuu hakuna NDOA, akili yako ndio ilipoishia Kwa kua una minyororo Kwa kua mtumwa wa dini sikulaumu
 
Haijalishi nmeandikaje, kikubwa umeelewa ndio lengo langu
 
Kwahyo sisi wenye familia hatuna majukumu, kisa tuu hakuna NDOA, akili yako ndio ilipoishia Kwa kua una minyororo Kwa kua mtumwa wa dini sikulaumu
Kama unaishi na mwenza wako na hutaki ndoa unaogopa majukumu.

Hapo ulipo unauwezo wa kumfukuza huyo mtoto wa watu muda wowote.,na hakuna wa kukuuliza sababu huna ndoa nae.
Lakini ukishapiga pingu ya maisha huwezi kufukuza mke kiholela.

Sheria zitakubana..

Pia hapo ulipo hutambuliki ukweni zaidi ya watu wawili watatu wanaokutambuwa.
Hata baba mkwe na mama mkwe kuja kwako pia haiwezekani...

Kama kidume oa basi,,uone cha mtema kuni.

Hapo ndy vijana wa hovyo mnapaogopa..
 
Kufunga ndoa mara nyingi ni kutafuta kutawaliwa na nguvu za nje kama makanisa, misikiti na serikali.

Sio Lazima kufunga Ndoa lakini kwenye ulimwengu wa kitapeli ndoa ni muhimu.

Sisi Watibeli hatufungishwi Ndoa.
Hakuna mwenye mamlaka Duniani wa kutufungisha ndoa wala kuivunja ndoa yetu.

Ila hatuingilii wale wanaofungishwa
 
Namimi SIFUNGI NDOA, maana SITAKI KUONA CHA MTEMA KUNI MAANA NDOA NI UTAPELI, hivi tunavyoishi ndio poa akileta za kuleta Kila mtu anashika njia yake.

Kwa kua umethibitisha mwenyewe kua Ukifunga NDOA nitaona cha MTEMA KUNI namimi sitaki stress siwezi kufunga ndoa, wewe umeshaingizwa mkenge endelea kukiona cha MTEMA KUNI
 
Shida Hawa waliofungishwa ndoa wanatupangia sana
 
Kwasababu wewe ndio mamayake na babayake sawa, sitambuliki ukweli kutokana na maneno yako wewe baba yake
 

Hakuna sheria inayokulazimisha kubaki ndoani hata moja.
Ukiamua kuvunja ndoa unavunja muda wowote na hakuna yeyote atafanya chochote zaidi ya kujaribu kukushauri tuu.

Hakuna kitu kinachoitwa pingu za maisha. Ni maneno ya uongo. Watu wanavunja ndoa hata mwezi haujaisha tangu wafanye harusi.

Ndoa ni makubaliano ya Hiyari ya Watu Wawili. Na inahusisha Majukumu ya wanandoa tuu bila kuhusisha Watu wa nje. Wengi wanaotaka ndoa zifungwe ni kutaka kujiingiza kwenye familia za Watu kwa kuomba misaada.


N
 
Vijana wa hovyo mnaogopa
--commitment
--majukumu.

Hakuna cha utapeli wala chochote..
 
Akili za Hawa jamaa zinanichekeshaga sana, dini inawaendesha sana hawajui watu walishaishi, na familia zilishakuepo hata kabla ya dini kuwepo

Muda ndio utakaoamua. Mambo yote ya uongo yatazidi kuondoka na kupitwa na wakati na dunia itabaki kwenye Ukweli kama Zamani.

Mwanadamu ni mnyama anayejikosha tuu.

Wanaotaka kufunga ndoa wafanye hivyo ili waende sawasawa na mila, desturi na imani zao na kuwafurahisha wazazi na wazee wao ikiwa ndio hivyo. Lakini ujinga wao unajitokeza pale ambapo wanawapigia kelele wale wasiofanya kama wao ilhali ya kwao yenyewe yalishawashinda.

Angalia wengi wanaosema ndoa ndoano asilimia 90% wamefuata hizo taratibu. Afu angalia wanaoenjoy maisha ya ndoa asilimia 90% hawajafunga ndoa (hawajafuta taratibu).

Ambao hawajafunga ndoa kuachana ni dakika sifuri kwa sababu hawapo chini ya yeyote, na hakuna unafiki.
Lakini waliofunga ndoa ni kama watoto wadogo ambao kila kitu ni mpaka waombe ruhusa na mpaka wapewe ruhusa
 
Usimtishe,huyu anajitambia. Apongezwe[emoji122][emoji817][emoji3581]
 
Kufunga Ndoa ni hatari sana lakini kufungishwa Ndoa tena na Mungu mwenyewe ndio kuna usalama!. Ana hoja asikilizwe!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…