92 jerrie
JF-Expert Member
- Feb 28, 2022
- 7,425
- 17,063
Ni kawaida kabisa pale palipoonekana pasafi huwa pamefichwa uchafu mwingi sana na watu hutumia miavuli ya dini kujisafisha machoni pa watu.Hivi kwa nini makanisani watu wanafuatilia sana mambo ya watu, halafu ndio wanaongoza kusengenya wenzao, yani shida tupu, hata mkeo unakwenda nae kanisani mwambie akae mbali na wapendwa.
Nikupe ushuhuda..... Muinjilisti na mchungaji walionifundisha mafundisho ya NDOA wote hawajielewi mchungaji ndio shetani mdogo fikiri mtu anakufundisha mambo mazuri ila yeye hatekelezi anadiriki kusema mbele ya usharika acheni mizigo yenu acheni dhambi acheni kutembea nje ya ndo ila yeye anachepuka na katibu wake hebu fikiri huo ukaribu hapo yaani humo humo kanisani unahubiri na humo humo unaanguka.
Muinjilisti nae anatufundisha ukaribu kwenye ndoa kuheshimiana anajiifia yeye na mumewe walivyo wafusi sahihi wa imani na yesu kristo ila nikaja kujua mumewe ni mlevi mavi akilewa anapaki mitaroni sasa mume wa muijilisti kweli akawe kwenye njia ya upotevuni inamaana hakuna imani hapo ni kujikinga kwenye mwamvuli wa dini