Waarabu hawakuwa Wakoloni Afrika?

Kwani watumwa walikuwa wanapelekwa Uarabuni au Ulaya na America?
Tukitaka kujadili ni nini kiliwatokea watumwa waliopelekwa Uarabuni najua tutaachana njia. Wale waliopelekwa Uarabuni hawakuwa na bahati kama wenzao waliokwenda Ulaya na Amerika. Leo waliokwenda Amerika na ulaya masalia yao tunayaona lakini wale waliopelekwa Uarabuni imebaki hadithi!!
 
sasa kipindi warabu wanatawala misri na libya watawaliwa walikua kina nani

Mkuu umeuliza swali zuri sana, watu wakwanza kutawaliwa hapo misri na charthage(libya-tripol) walikuwa takribani walikuwa weusi ndoo maana wakaitwa kwanza sudan na watawala wa Roma na Ugiriki likaja neno Afrika sijui kama unajua watu gani walibatiza ili bara Afrika! kama unajua basi ongera.
Kitu gani kilifanya watu weusi wapungue huko?Ukifatilia historia zaidi nikuwa 1798 wakati Sultan mwanajeshi Mohamed Ali anaingia kutoka Uturuki na kumuonda Mfaransa Napoleon Bonaparte watu weusi walikuwa na nafasi kubwa lakini jamaa alipokuja watu weusi walipungua na nikivipi?Wengi walikimbia uislam kwani sultan alilazimisha watu kuwa waislam na wengi walirudi Sudan lakini jamaa hakuishia hapo kwani alivamia mpaka sudan na ikawepo vita kali.Tangia hapo waarabu wakawa wengi kwa kuzaliana na kulingana na mafundisho ya dini yao ya kuoa wanawake zaidi ya mmoja.
Pili ikumbukwe weusi wengi walikuwa wafuasi wa coptic church then walikuwa wakubariki kuoelea na mtu wa coptic alikuwa anapata shida kweli kama kupigwa,kuuwawa,kutozwa kodi kubwa etc.
Kuna tatizo kwenye kufundisha na kuandika historia ya Afrika,mfano wanafunzi wakitanzania awe O and A level historia ya N.Afrika hawaijui vizuri kuna mtu ameniambia kuwa ata chuo haifundishwi labda ufanye kama somo la ziada.Naombo mungu na washaishaji wa necta wanipendelee nifauru form 4 niende A level na niende chuo nisome hiyo course.
 
Vitabu vingi vya Historia na Fasihi viwe vimeandikwa na waafrika wenyewe au watu wa kutoka nje ya bara la Afrika, mara zote vinawataja Wareno,Waitaliano, Wajerumani, waingereza, Wadachi, na Wafaransa kama wakoloni, lakini mimi sijawahi kukutana na kitabu kinawataja waarabu kama wakoloni. Najiuliza kama waarabu hawakuwa wakoloni sifa yao ilikuwa ni nini hasa? Wavamizi, wafanyabiashara, waeneza dini au wao walikuwa pia wanatawaliwa na hao tunaowaita wakoloni?

mkuu umesoma vitabu au booklets za wakina Nyangwine haya soma hivi vitabu History of Africa by K.Shillinton 2ed,Africa since 1800 by Roland Oliver et al Batimire,IN THE BALANCE-WORLD HISTORY na Traditional and Encounters.
 
Mwarabu ni mwarabu. Mtu yeyote mwenye asili ya Bara arabu bila ya kujali kama katoka Yemen Emirate au Iran hao ndiyo waarabu. Naona kuna watu wanataka kusema hakuna waarabu duniani!! Sijui wanataka kukimbia nini??

I see na wazungu ni watu gani? na imekuwa kawaida dar watu wanasema fulani bana kama mzungu mambo yake naye ni mtu wa aina gani?
 
haya turudi darasa la 3 jamani,
MWALIMU: ukoloni nini nini?
WANAFUNZI(kwa pamoja): ukoloni ni kitendo cha nchi moja kuitawala nyengine kiuchumi kisiasa na kijamii.

Haya tuanze kisiasa sasa:
waarabu walikuja pwani ya africa mashariki je walitawala? Jibu hapana utawala ulikua chini ya machief wa kiafrica mfano mirambo
Kwa case ya znz ndio warabu walitawala mfano sultan seyid said

Tuje case ya kiuchumi:
Je ni kweli walitawala kiuchumi? Jibu hapana mfumo wa kiuchumi wa kiafrica ulikua vile vile mwarabu haku introduce capitalism wala socialism ila ye alikua middle men tu

Kisocial je?
Pia jibu litakuja hapana maana waarabu walikuja na culture ya kiisilamu lakini hawakuieneza kwa force ila kwa anaetaka.

Ukweli utabakia pale pale mwarabu si mkoloni na wala si mwenye biashara ya utumwa bali ni middle man ambaye alikua akitumika na nchi za kibepari za kizungu mfano hai subiri niwapeni

Now warabu wengi ni madereva mafuso. Kupitia mafuso yao wanatumika kununua mazao (kwa kuwanyonya wakulima). Then anenunua mazao ni tajiri wa mjini. Si haki kumnyonya mkulima ila fuso la mwarabu limetumika na anaenunua ni tajiri wa mjini.

Mfano huu kwa wenye akili ataelewa kama mwarabu alikua mkoloni au kibaraka

Naona mkuu umetujuza ingawa hapa kuna kitu umesema mwaarabu akuleta aina yoyote ya uchumi..mh sidhani kwani kati ya watu kutoka ulaya na yeye nani amekuwa wakwanza kufika east africa coast?Ref.Ibn Batuta and A Greek article tittle Peryplus of the Anthrenian sea kuna kitu kimetajwa kama media of exchange being coins,cowries,commodities etc.Alafu ustaarabu kama majengo,miskiti,madrasa,mavazi,utawala wa masheikh,mavazi,utumwa,biashara,mazao,makazi(miji) etc sasa inakuwaje unasema waarabu hawa kuleta mfumo mpya hapa Afrika na ujue kuwa hata wazungu hawakuleta mambo tofauti na waarabu mfano dini,elimu,mazao etc
 
Kwani watumwa walikuwa wanapelekwa Uarabuni au Ulaya na America?

kwani mafuta ya Arabuni soko lake kuu liko wapi? hujui? waarabu mpaka kesho ni wavivu hawapendi kazi za shuruti. ili kufanya biashara na wamagharibi ilipaswa kupata manapower. ndo hayo mambo ya mji-mkongwe. ngozi nyeusi imeteseka sana. inashangaza kuona kuna watu wanawatetea waarabu. usaliti huu.
 
Mwarabu ni mwarabu. Mtu yeyote mwenye asili ya Bara arabu bila ya kujali kama katoka Yemen Emirate au Iran hao ndiyo waarabu. Naona kuna watu wanataka kusema hakuna waarabu duniani!! Sijui wanataka kukimbia nini??

Hapo ndipo unapokwenda mrama. Yemen hakuna Emirate na Iran sio Waarabu si hata kwa lugha. Naona unataka kubisha vitu ambavyo hukuchukuwa muda hata wa kuvisoma japo kidogo, nakushauri nisome vizuri, utapata faida kubwa sana. Hili la historia ni somo nnalo lipenda sana.

Wa Iran ni wa "persia" na hao ndio wanaojulikana pwani ya Afrika Mashariki kama Mashirazi.
 
Hapo ndipo unapokwenda mrama. Yemen hakuna Emirate na Ira sio Waarabu si hata kwa lugha. Naona unataka kubisha vitu ambavyo hukuchukuwa muda hata wa kuvisoma japo kidogo, nakushauri nisome vizuri, utapata faida kubwa sana. Hili la historia ni somo nnalo lipenda sana.

Wa Iran ni wa "persia" na hao ndio wanaojulikana pwani ya Afrika Mashariki kama Mashirazi.

Hakuna anaesema hakuna Waarabu duniani lakininimekueleza huko juu Waarabu ni kina nani na kwanini wanaitwa Waarabu naona hukulipenda hilo. Sasa kijana unataka kupata elimu kwa kubishana? elimu huwa watu wanafanya mnakasha, na si kubishana, unalolijuwa unaonesha na kama sikubaliani nalo nakupa sababu zangu na wewe hali kadhalika. Usitake kubandika maneno yako vinywani mwa watu, elimu haipatikani hivyo.
 
Hakuna anaesema hakuna Waarabu duniani lakininimekueleza huko juu Waarabu ni kina nani na kwanini wanaitwa Waarabu naona hukulipenda hilo. Sasa kijana unataka kupata elimu kwa kubishana? elimu huwa watu wanafanya mnakasha, na si kubishana, unalolijuwa unaonesha na kama sikubaliani nalo nakupa sababu zangu na wewe hali kadhalika. Usitake kubandika maneno yako vinywani mwa watu, elimu haipatikani hivyo.

bibie wameguswa waarabu kimekukuna. pole.

una ndugu arabuni?

nimekuja kivengine.
 
teh teh teh! Waarabu wabaya sana coz walishiriki kuwauza Maniga huko ufaransa,uingereza,marekani{kwa mabwana zenu wazungu ambao mnawaona wema }lakini aliogopa kuwapeleka kule arabuni coz biashara hiyo ilikuwa haramu.. Lakini Waarabu ndo wakoloni pekee walo"zaa" na dada zenu weusi na kuish nao kama wake zao...
.
.
Namaliza kwa kusema kuwa waarabu walikuwa wakoloni "waungwana" walotuletea Uislam

kwa hyo kuzalisha dada zetu wa kiafrica ndo umewapa maksi?
Waarabu, wazungu yote mikoloni tu!
 
Tukitaka kujadili ni nini kiliwatokea watumwa waliopelekwa Uarabuni najua tutaachana njia. Wale waliopelekwa Uarabuni hawakuwa na bahati kama wenzao waliokwenda Ulaya na Amerika. Leo waliokwenda Amerika na ulaya masalia yao tunayaona lakini wale waliopelekwa Uarabuni imebaki hadithi!!

Nadhani biashara ya utumwa unaisoma kijujuu, utumwa ilikuwa ni biashara ya dunia nzima. Enzi hizo kulikuwa hakuna neno, "mfanya kazi", mfanya kazi ni Mtumwa tu au mtumishi siku hizo, na walikuwepo wa kila namna na kutoka kila Taifa. Walikuwa wanahitilafiana thamani zao zao kwa wayajuwayo.

Kuna Waafrika walikuwa na watumwa kutoka Uropa na hali kadhalika kulikuwa kuna Wa Uropa walikuwa na watumwa kutoka Afrika.

Somo la utumwa na historia yake ni ndefu kuliko unavyofikiria, samahani kwa kukuambia kuwa, kwa maandishi yako machache naweza kusema hujaingia ndani kuisoma historia kama hobby au somo na nnauhakika, hukufanya vizuri mitihani ya historia kama lilikuwa ni moja ya kati ya masomo uliyofundishwa.

Nakuomba tafadhali sana wacha kuchanganya mambo twende taratibu utafaidika sana, kama ulivyofaidika kule kwa Mohamed Said, unajuwa, mashule duniani huifundisha historia ya mwanzo mashuleni kutokana na wanavyotaka wao wanafunzi wawe na ufahamu upi. Ukiondoka stage hiyo ukifikia kutaka kuingia ndani kwa kina, kiila utavyo zama utakutana na pembe tofayti za historia zitazokufanya uwe na uelewa mpana zaidi.

Umeanza na ya Waarabu, hujayamaliza unarukia ya Utumwa. Tumalize ya ukoloni wa Waarabu kwanza, hilo pekee ni somo tosha na amabalo hulielewi na ndio maana ukaliuliza> Kaa tupeanae darsa, si lazima tukubaliane kwa yote lakini mwisho wa siku tutakuwa tumeondoka tumefaidika sote. Au unasemaje?
 
kidogo wao waliona dili ni kuwatia mimba bibi zetu wa kiafrika na kuwahasi wanaume wa kiafrika. Si unaona mbegu walizoacha zanzibar, hasa pemba. jamaa wao dili ni kut......ba wanawake tu. Na huo ugonjwa wakawarithisha watu wote wa pwani nao kwa akili zao finyu wanaendeleza hiyo kitu ya kuzaliana
 
Kwa mwarabu uislamu ni sehemu ya utamaduni wao. Ndio maana ukishaanza kujadili uarabu humu ndani lazima utaonekana una upinga uislamu-na huo ndiyo ukweli wenyewe. Asad akipigwa bomu moja tu, utasikia wanataka kuuangamiza uislamu. Hii kitu ni bora iachwe tu wakuu.

Kusema mwarabu hakuleta mfumo wa uzalishaji wa kiuchumi nayo ni kupotosha ukweli. Slavery ni moja ya mifumo ya uchumi ya uzalishaji. Kwa mwarabu kuwachukua watumwa toka bara kuwauza ughaibuni, ni mfumo pia wa uzalishaji-Slave Mode of Production.
 
Nadhani biashara ya utumwa unaisoma kijujuu, utumwa ilikuwa ni biashara ya dunia nzima. Enzi hizo kulikuwa hakuna neno, "mfanya kazi", mfanya kazi ni Mtumwa tu au mtumishi siku hizo, na walikuwepo wa kila namna na kutoka kila Taifa. Walikuwa wanahitilafiana thamani zao zao kwa wayajuwayo.

Kuna Waafrika walikuwa na watumwa kutoka Uropa na hali kadhalika kulikuwa kuna Wa Uropa walikuwa na watumwa kutoka Afrika.

Somo la utumwa na historia yake ni ndefu kuliko unavyofikiria, samahani kwa kukuambia kuwa, kwa maandishi yako machache naweza kusema hujaingia ndani kuisoma historia kama hobby au somo na nnauhakika, hukufanya vizuri mitihani ya historia kama lilikuwa ni moja ya kati ya masomo uliyofundishwa.

Nakuomba tafadhali sana wacha kuchanganya mambo twende taratibu utafaidika sana, kama ulivyofaidika kule kwa Mohamed Said, unajuwa, mashule duniani huifundisha historia ya mwanzo mashuleni kutokana na wanavyotaka wao wanafunzi wawe na ufahamu upi. Ukiondoka stage hiyo ukifikia kutaka kuingia ndani kwa kina, kiila utavyo zama utakutana na pembe tofayti za historia zitazokufanya uwe na uelewa mpana zaidi.

Umeanza na ya Waarabu, hujayamaliza unarukia ya Utumwa. Tumalize ya ukoloni wa Waarabu kwanza, hilo pekee ni somo tosha na amabalo hulielewi na ndio maana ukaliuliza> Kaa tupeanae darsa, si lazima tukubaliane kwa yote lakini mwisho wa siku tutakuwa tumeondoka tumefaidika sote. Au unasemaje?

Mimi sikuileta hoja ya Utumwa bali watu katika kujadili ukoloni ndiyo ikaja hoja ya Utumwa. Mimi huwa sikariri wengine wameandika nini na kugeuza hicho kuwa ndiyo maandiko matakatifu kwenye kutafakari kwangu. Kuna watu ni "Bookish" wao kila kitu wanauliza umewahi kusoma kitabu fulani. Kuna watu wanafikiri aliyeko kwenye jamvi hili ni wa rika lao ndiyo maana wanauliza "umesoma Papers za Nyangwine?"

Kwanza lazima nikiri mimi si msomi wa kiwango chochote kile unachokifahamu wewe, bali najitahidi kutumia uwezo wangu wote niliopewa na mwenyezimungu kutafakari mambo. Hebu jiulize kabla ya ugunduzi wa karatasi na uvamizi wa wakoloni Afrika kulikuwa hakuna waafrika walikokuwa wanafikiri zaidi ya wenzao. Walisoma wapi? Swali langu nataka kujua sisi kama waafrika tafsiri yetu kuhusu waarabu ni ipi? Unajua kama tafsiri yako kuhusu uarabu ni lazima iwe ni ile inayotokana na wazungu au waarabu wenyewe basi hapo kuna shida

Ukienda uswahilini kwetu kule Vingunguti Kiembembuzi, ukiuliza Mwarabu ni nani sijui kama tafsiri yako Bi. Mkubwa itafaa.

Halafu sikujua ya kule kwa Mohamed Said utayaleta huku. Na wewe!!
 
Mimi sikuileta hoja ya Utumwa bali watu katika kujadili ukoloni ndiyo ikaja hoja ya Utumwa. Mimi huwa sikariri wengine wameandika nini na kugeuza hicho kuwa ndiyo maandiko matakatifu kwenye kutafakari kwangu. Kuna watu ni "Bookish" wao kila kitu wanauliza umewahi kusoma kitabu fulani. Kuna watu wanafikiri aliyeko kwenye jamvi hili ni wa rika lao ndiyo maana wanauliza "umesoma Papers za Nyangwine?"

Kwanza lazima nikiri mimi si msomi wa kiwango chochote kile unachokifahamu wewe, bali najitahidi kutumia uwezo wangu wote niliopewa na mwenyezimungu kutafakari mambo. Hebu jiulize kabla ya ugunduzi wa karatasi na uvamizi wa wakoloni Afrika kulikuwa hakuna waafrika walikokuwa wanafikiri zaidi ya wenzao. Walisoma wapi? Swali langu nataka kujua sisi kama waafrika tafsiri yetu kuhusu waarabu ni ipi? Unajua kama tafsiri yako kuhusu uarabu ni lazima iwe ni ile inayotokana na wazungu au waarabu wenyewe basi hapo kuna shida

Ukienda uswahilini kwetu kule Vingunguti Kiembembuzi, ukiuliza Mwarabu ni nani sijui kama tafsiri yako Bi. Mkubwa itafaa.

Halafu sikujua ya kule kwa Mohamed Said utayaleta huku. Na wewe!!

Hiyo tafsiri yangu ndio hiyo nnaitolea ufafanuzi ya huko kiembembuzi na kwingine kokote, haina kukinzana. Wa kiembembuzi hawana tofauti na wewe hata kidogo, wamuonae wao humuita Mwaarabu, na ndivyo ilivyo hawajui huyu ni Mwaarabu wala si Mwaarabu, awe Muhindi awe Mshirazi. Hapo ndipo unapokuja mjadala, Muarabu ni nani? jibu nimelitoa huko juu na unalijua sina haja ya kulirudia.
 
[FONT=Times,Times New Roman]At the very beginning of the first Century CE, Zanzibar was part of the Kingdom of Saba (115 BC-525 CE), also known as Sheba. The Sabeans were a maritime people, with a large kingdom in Yemen and used the seasonal monsoon winds to travel regularly to and from Zanzibar. Their sailed south between November to February, during the Northeast Monsoon, carrying beads, the Chinese porcelain and clothes. Between March and September, they returned to north on the Southwest Monsoon, carrying food grains, mangroves poles for timber, spices, gold (from Sofala), ivory and ebony. These Arabs knew the East African coast as "Zinjibar" and thence the romantic name Zanzibar is derived.
source: [/FONT]http://victorian.fortunecity.com/portfolio/543/crusades.html[FONT=Times,Times New Roman]
[/FONT]
 
Namaliza kwa kusema kuwa waarabu walikuwa wakoloni "waungwana" walotuletea Uislam

Wale babu zako waliopelekwa uarabuni unajuwa walikfanyiwa kitu gani mpaka hawakuzaana huko kama Ulaya na Amerika? Ukikijua hicho ndo utajua ustaarabu wa mwarabu ukoje!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom