Pretty.. kwanza nadhani kuna majibu ya kisiasa na majibu ya kimkakati. La kisiasa ni kuwa CCM inafanya hivyo kwa sababu inaweza na kwa sababu Chama kinajijenga zaidi. Kwa upande wa mkakati ni kuwa kwa mtu yeyote ambaye anataka kufanikiwa huko mbeleni (kisiasa, kiuchumi na vinginevyo) ni muhimu kuchagua upande unaoshinda.
Wakati mwingine nafikiria hata yawezekana ni bora kurudisha chama kimoja tu ili kila mtu awe anaingia kwenye chama halafu tukijaza fomu za kuomba kazi, n.k tujaze kuwa "tulipitia UVCCM" au tumewahi kuwa viongozi wa chama mahali fulani. It comes na ujiko fulani.
Lakini upande mwingine inawezekana kabisa wananchi hawa wanamapenzi ya kweli ya CCM na wameshindwa kujizuia kutoyaonesha mapenzi hayo na wameamua kufanya hivyo. Kama hili ni kweli basi ni matatizo ya upinzani kutojitahidi kupata wanachama hadi nje ya nchi au matatizo ya mashabiki wa vyama vya upinzani na wenyewe kutojiunganisha na kuanzisha matawi yao huko waliko.
Tatizo litakuja pale ambapo vyama vya upinnzani navyo vitaanza kuanzisha amtawi kama hapo London n.k na matokeo yakawa ni mgawanyiko wa Watanzania. Ndio maana sisi wengine huku US tuko sensitive kweli na mambo haya ya kuanzisha matawi ya vyama hapa.
Mzee Mwanakijiji, Heshima mbele - Umechambua vyema sana mimi binafsi nakubaliana na wewe kwa yote uliyoandika hapo juu, Chukua Tano Mkuu
- Sometimes wa-Tanzania tunapenda sana kukuza ishus bils sababu, wananchi wana haki ya uhuru wa kuchagua wanayotaka kuyafanya na wasiyoyataka as long hawavunji sheria za Tanzania au za nchi walioko, binafsi sioni tatizo lolote na wananchi kujiamulia kuanzisha tawi la CCM au la Chadema hivi kwani wanalazimisha mtu kujiunga nao? Au wamemuharibia mtu kazi huko majuu?
- I mean please, waacheni jamani tunawaonea bure na hizi attacks bila hoja ya msingi, mwisho itaonekana tunawaonea wivu, wakianzisha matawi ya CCM, tuliobaki tuanzishe Jumuiya ya ki-Tanzania ili asiachwe mwananchi bila msimamo, waacheni wananchi wafurahie matunda ya uhuru na Demokrasia ya kujamulia mambo yao wenyewe bila kuamuliwa na serikali.
- So far hatuna hoja ya msingi ya kuwashambulia wananchi wanaoanzisha matawi ya CCM, sasa it about time tukawaacha kama walivyo na matawi yao!
Respect.
FMEs!
.........Siku hizi naona matawi mengi ya CCM yanafunguliwa huko ughaibuni, lakini mwenzenu sielewi malengo yake haswa ni nini? Je kama taifa linapata faida gani kutokana na hayo matawi ya chama cha siasa nje ya nchi?
Mwenzenu najiuliza hivi kwa sababu sijajua bado kama nchi nyingine hapa duniani nao wana utaratibu wa kufungua matawi ya vyama vyao tawala nje ya nchi zao?
Hapa Tanzania wapo raia wa nchi mbali mbali wanaishi hapa, lakini sijasikia kama wamefungua matawi ya vyama vyao vya siasa hapa nchini.
Lengo haswa ni nini hadi CCM inafungua matawi huko ughaibuni?Mie huwa najiuliza sababu ya ufunguzi wa hayo matawi sipati jibu...........hivyo nimeamua kuleta hapa labda nitapata majibu.
Mie nadhani hawajiamini na maisha yao, hivi mfano unakazi au unasoma utaweza kupata muda wa kuhudhuria upuuzi huu??? mhh asilimia kubwa ya hao watu ni chadirishani😀😀
Mie nadhani hawajiamini na maisha yao, hivi mfano unakazi au unasoma utaweza kupata muda wa kuhudhuria upuuzi huu??? mhh asilimia kubwa ya hao watu ni chadirishani😀😀
Mwenye macho haambiwi ona mkuu! Watayaona mbele ya safari baada ya kukusanya kila wanalotaka kukusanya hata kama ni mabomu ya kutegwaHata walioko Italy wamefungua !Lakini kama kuna mtu anajua mambo ya Italy,especially ya immigrant wa kiafrika walioko huko,tuliotembea tunajua .
CCM itakuja kuadhirika na watu hawa ,wengi wana history mbaya.
Kwa jukwaa hili, subiri matusi, lakini isikutishe, ni bora kupuuzwa na wajinga 1000mil. ila ukaungwa mkono na mwerevu mmoja!wakuu labda mnisaidie!kuna umuhimu gani wa chama pinzani kuanza kufungua matawi nje ya nchi wakati kuna baadhi ya maeneo ndani ya nchi hii hawajayafikia, ukizingatia watanzania wengi nje ya nchi hawaji kupiga kura wakati wa uchaguzi,na hatuna mfumo wa ON LINE VOTING?? inanitatiza sana hii