ni wazi kuwa hao wakaazi wa maeneo/vijiji ulivyovitaja nao wanatambua ugumu wa maisha na umasikini uliowajaa, hivyo basi wanapaswa kuwa na hasira na uchungu wa kuungana na harakati zozote za kupambana na aliyesababisha wao wawe hivyo ambaye ni ccm.
Wao wenyewe kwanza wanapaswa kuonesha nia ya kutaka kujiunga pamoja kupambana na adui ccm, kwa kuanzisha matawi na misingi ya cdm, kama wanaamini ndio chama sahihi kitakachoweza kuongoza harakati za ukombozi wa taifa lao.
Lakini kama bado wanaamini ccm ndio baba na mama yao, wataendelea kupeperusha bendera za ccm kwenye nyumba zao za tembe, wakisubiria msimu wa kupewa kanga, kofia na pilau.
Chadema sidhani kama ililazimisha london wafungue matawi ya chama , bali watanzania wenzetu waishio huko kwa kutambua umuhimu wa wao kushiriki kwenye harakati za kuikomboa nchi yetu kutoka kwa wakoloni weusi ,ccm,waliamua kujiunga pamoja na kuomba kutambuliwa na chama kama tawi.
Vivyo hivyo ninawaomba ndugu zangu wa huko kusini, kama tunatambua umuhimu wa harakati za kupambana na ufisadi,rushwa, umasikini mauaji holela ya raia, unyonyaji wa rasilimali zetu. Kama tunataka kuboreshwa kwa huduma za jamii, usawa katika mgawo wa keki ya taifa, maboresho ya kweli ktk sekta ya kilimo (sio hadithi za kilimo kwanza na powertillers), upatikanaji wa pembejeo za kilimo, soko la uhakika la mazao yetu, malipo stahiki kwa jasho tuvujalo.
Hatupaswi kuisubiri chadema ije ituambie haya, bali tujiunge pamoja, tuhamasishane (kama wenzetu wa huko ulikotaja) na kisha tuombe chadema itutambue kuwa na sisi ni sehemu yao, tunaiamini natunaongeza nguvu ya umma, katika kusukuma mbele harakati za kutafuta mabadiliko ya kweli.
Ninawaomba ndugu zangu popote pale mlipo, tusijiweke pembeni na kusubiri chama-cdm ,kije na kufanya kwa niaba yetu, tuamue kuwa sehemu ya harakati hizi pale pale tunakoishi ili hatimaye tuishinde vita hii!
Peoples...........