Vurugu kubwa kariakoo

Vurugu kubwa kariakoo

tuwekee japo picha moja. kama inawezekana.
 
sasa hivi ulinzi na usalama uko chini ya raia, coz askari wote wameshindwa kazi na wao wanapewa kisago kama kawa.
hii inanikumbusha wakati niko shule serikali poa unakuta viongozi wanapigwa na raia afu serikali ya wanafunzi inashinwa cha kufanya coz inawaogopa wababe.
ndo serikali ya JK imeshindwa kudhibiti mpaka raia wanajichukulia sheria mkononi, kwa sasa ni kawaida waziri na hata Rais mwenyewe kupopolewa mawe na kuzomea. haya yamemtokea JK mwenyewe na mawaziri kadhaa. hii nchi tunakoelekea kwa sasa naona giza nene badala ya nuru. Mungu atuepushe na hizi vurugu.
 
Tulia uandike kitu kieleweke ndo uturushie bhana, sasa hapa ndo umesema nini?
 
Kisa ni nini?

Habari nillizozipata jana kuna chinga mmoja alipigwa sana na wagambo wa jiji bila sababu. Akaenda kushitaki polisi msimbazi. Leo afisa mmoja wa polisi akiwa hajavaa uniform akamchukua huyo chinga ili amwonyeshe hao mgambo waliompiga. Badala yake wale mgambo wakamchapa sawa sawa yule afisa na kumnyanganya bunduki yake.
 
Habari nillizozipata jana kuna chinga mmoja alipigwa sana na wagambo wa jiji bila sababu. Akaenda kushitaki polisi msimbazi. Leo afisa mmoja wa polisi akiwa hajavaa uniform akamchukua huyo chinga ili amwonyeshe hao mgambo waliompiga. Badala yake wale mgambo wakamchapa sawa sawa yule afisa na kumnyanganya bunduki yake.

Hahahahahahaaaa......aseee.
Kwahiyo kilichobaki ni kukamata adui yako na kutembeza kichapo tu.
 
Taarifa zikamfikia mkuu wa kituo. Akawapa mamlaka wamachinga woote wa kariakoo kuwasaka mgambo wa city popote walipo na wampelekee kituoni, bila kujali wako katika hali gani.

Hapo Mgambo lazima miguuni wafunge motor, la sivyo wataumia.
 
Taarifa zikamfikia mkuu wa kituo. Akawapa mamlaka wamachinga woote wa kariakoo kuwasaka mgambo wa city popote walipo na wampelekee kituoni, bila kujali wako katika hali gani.
Post hii inaanza kunitia wasi wasi wa hii story yako
 
Kwa machinga hii imekuwa ni dream come true. Nimeshuhudia tangu saa saba mchana msako unaendela. Nimeona mgambo watatu wamezingirwa na machinga wakipewa kipigo. Tena wanatembezwa kwa amri, simama juu, kaa chini. Mpaka wakatokea askari kanzu kuingilia kuwaokoa.
 
Post hii inaanza kunitia wasi wasi wa hii story yako

Mkuu mambo xanafanyika peupe. Mpaka sasa makundi ya vijana yanazunguka kusaka wanamgambo yakipiga makelele kuwa wamezidi kutuonea hawa.
 
Jamani mgambo wanapitishwa kila baada ya muda mfupi wakipelekwa kituoni hata kama hamuamini!
 
Back
Top Bottom