Vumbi limetulia ukweli unatamalaki

Vumbi limetulia ukweli unatamalaki

Rudi shule ukasome,Mkuu Mshana ameeleza vizuri sana bila chenga,na kila kitu ameweka wazi kabisa,sasa wewe unakuja na upupu wako kuhusu vita kutokea na mji mkuu kutekwa?,au uko kilabuni unakunywa kangara,kaa kimya kuliko kutujazia kurasa.
Inatakiwa ujifunze namna ya kujiongeza kijana,
sio watoto wako hadi wafe kwa njaa ndio ujifunze namna ya kuweka akiba ya chakula nyumbani kwako.
Kosa alilofanya Mwalimu Nyerere la kuendelea kuitumia Dar kama makao makuu ya nchi baada ya uhuru alishaliona akakiri na akatoa wazo la kuamia Dodoma, maraisi waliopita kama Mwinyi, Mkapa, Kikwete walishindwa ila Magufuli kathubutu kwa miezi 8 tu aliyokaa madarakani, baada ya watanzania kumuunga mkono mnaanza kuleta ushabiki na maneno yasiyo na maana.
Pia fatilia nchi zingine kama Marekani, Uingereza, China, Afrika ya Kusini, Kenya n.k kama makao makuu ya nchi zao yapo Pwani au katikati ya nchi zao.
 
Inatakiwa ujifunze namna ya kujiongeza kijana,
sio watoto wako hadi wafe kwa njaa ndio ujifunze namna ya kuweka akiba ya chakula nyumbani kwako.
Kosa alilofanya Mwalimu Nyerere la kuendelea kuitumia Dar kama makao makuu ya nchi baada ya uhuru alishaliona akakiri na akatoa wazo la kuamia Dodoma, maraisi waliopita kama Mwinyi, Mkapa, Kikwete walishindwa ila Magufuli kathubutu kwa miezi 8 tu aliyokaa madarakani, baada ya watanzania kumuunga mkono mnaanza kuleta ushabiki na maneno yasiyo na maana.
Pia fatilia nchi zingine kama Marekani, Uingereza, China, Afrika ya Kusini, Kenya n.k kama makao makuu ya nchi zao yapo Pwani au katikati ya nchi zao.
Nchi yenyewe imeishauzwa,imebaki KAPUKU,nani anataka kuja kuteka au kufanya vita na MAKAPUKU?,hivi wewe hujui kwamba Tanzania kurudi kama mkoloni alivyoiacha itachukua si chini ya miaka 200?,kwa hiyo hifadhi nguvu zako ujitafutie uji na mihogo.
 
Asante wewe mwenye ubongo,lakini kumbuka Mshana kaandika kwa hekima sana,wewe umejitahidi ila ukaingiza vitu ambavyo havina umuhimu.
Mshana ajaandika kwa hekima, bali ameandika kwa itikadi na mtazamo wake,
kuandika kwa hekima maana yake lazima angekuwa neutral bila kuwa upande wowote.
Mtazamo wake umejaa kupinga juhudi za Magufuli tangu ametoa tamko la kuhamia dodoma ambapo ametoa mifano mingi yenye hoja nyepesi sana.
 
Nchi yenyewe imeishauzwa,imebaki KAPUKU,nani anataka kuja kuteka au kufanya vita na MAKAPUKU?,hivi wewe hujui kwamba Tanzania kurudi kama mkoloni alivyoiacha itachukua si chini ya miaka 200?,kwa hiyo hifadhi nguvu zako ujitafutie uji na mihogo.
Nasikitika kuona kijana hasa uliye JF kuongea maneno ya kukata tamaa kama hayo, ingekuwa FB ningekuacha ila kwa kuwa umo humu jamvini ngoja nikwambie kitu,
Hata kama hauna pesa nyumbani kwako jitahidi kila siku jifunze kuweka mazingira ya kuweza kupata pesa, ili siku Mwenyezi Mungu akikubariki ziweze kudumu.
Haya mambo ninayoandika ni madogo sana na nasikitika kuona unasema natumia nguvu kubwa, mana sijui wewe unatumia ubongo asilimia ngapi hadi unaona me natumia nguvu kubwa.
 
Mkuu nimekuelewa mzee.
Tatizo la serikali hii wao kazi yao ni kukurupuka na kutoa matamko tu.
Hawajui wala kutaka kupembua mambo kwa kutumia akili.

Akili ya Magufuli ni sawa na mtoto kaona nzi kwenye bakuli la uji. Badala ya kuchukua kijiko na kutoa yule nzi,atampiga nzi kibao na kumwaga uji wote,mwisho wake kumuunguza.

Yetu sisi macho. Anajifanya kucheza ba maisha ya watu na amani. Ubabe yeye,matamko yasio na tija ni yeye. Huyu mtu ana aakili timamu kweli?
Mkuu andaa mili7 na laki 2 fasta
 
Ina maana watendaji wake (JPM) hawakumuelewa ama ni nidhamu ya uoga au ni upungufu wa kufikiri?..

Bila shaka ni upungufu wa kufikiri uliofanywa mchanyato na nidhamu ya uoga. Nina uhakika ukimuuliza mama Jenista kwa nini anaharakisha kwenda Dodoma by September, jibu lake litakuwa ni "kutaka kumuwahi PM". Ukihamia kwa Majariwa na kumuuliza swali hilo hilo, usishangae kujibiwa anatimiza agizo la mkuu. Nothing more.

Na Wazabuni waendelee kuzibana korodani zao tu mpaka kiherehere cha kuhamia Dom kiishe.
 
Mimi nafikiri kabla ya kuanza kutoa lawama na shutuma kwa Rais JPM na safu yake ya uongozi juu ya uamuzi wake wa kuhamisha makao makuu ya nchi na serikali yakutoka jijini Dar hadi mkoani Dodoma ni vizur tukajiuliza haya maswali machache
1. Dhumuni hasa la muasisi wa nchi yetu Mwalimu JK Nyerere kuhamia Dodoma lilikuwa nini hasa?
2. Kwa nini mataifa makubwa duniani hayajaweka makao makuu ya nchi zao kwenye maeneo ambayo ni pembezoni mwa bahari mfano Marekani - washington DC, Uingereza - London, China - Beijing, South Afrika - Pretoria, Majirani zetu kenya nao wameweka Nairobi iliyopo katikati ya nchi na sio Mombasa iliyopo pwani mwa nchi yao?
3. Kiusalama ni vizuri makao makuu ya nchi yakae pwani au yakee katikati mwa nchi?
4. Kuleta maendeleo yenye usawa sawa katika nchi ni je vizur makao makuu ya nchi yabaki Dar au tuamie dodoma?
5. Ili kuweka karibu kuweka huduma za kiserikali karibu na wananchi ni vizur makao makuu ya nchi yaendelee kuwa dar au tuamie dodoma?

Mwenye majibu mujarabu wa haya maswali ndio anaweza kuendelea kukosoa uamuzi wa serikali kutoka Dar kwenda dodoma.
Note:
Kuna kosa ambalo alifanya mwalimu JK Nyerere la kuruhusu kutumia Dar kama makao makuu ya nchi, kwani ule uamuzi ndio ulipelekea mikoa mingine iendelee kudumaa nchini Tanzania hadi sasa, hivyo watanzania naomba tumuunge Rais JPM kwa dhumuni la kusahihisha makosa yaliyofanywa na mwalimu JK Nyerere, ambapo watangulizi wake kama Mwinyi, Mkapa, Kikwete walishindwa.
Pili watanzania inabidi tuvumilie maumivu tutakayopata kwa sasa baada ya zoezi la kuhama kutoka Dar kwenda dodoma litakapoanza, kwani badae hali itatengamaa na pia nchi yetu itakuwa katika nafasi nzuri ya kukua strategical.
Kumbe Washington ni katikati ya Marekani nilikuwa sijui!!!!!
 
Usihofu, yale ni matamko ya mwendokasi tu. Binafsi sioni faida kwa muda huu, labda kipindi cha Nyerere ndio palikuwa na tija. Kuhama ni gharama na si kipaumbele kwa sasa.

acha kungangania DAR WEW MAMA HATA KAMA UMEWEKEZA HUKO UMUHIMU UPO TENA MKUBWA TU
 
NISICHUKULIWE KAMA MKOSOAJI
Magufuli aliongea vizuri sana kuwa atahakikisha serikali yake inahamia/itahamia Dodoma kabla kipindi chake cha kuwa madarakani kwisha, amebakiza miaka minne na ushee
Baada ya hotuba ile tu ukatokea mlipuko wa matamko ya kuhamia Dodoma na mishemishe zikawa nyingi
-Aliaza Chizeba
-Akafuatia Jenista Mhagama
-Mambo ya ndani na wengineo
Hawa wote wakasema ni kabla ya mwezi wa tisa

ATHARI ZA MATAMKO HAYA
maandalizi lipulipu yakaanza Dodoma
Wapangaji wa CDA wakafukuzwa
harakati za kutafuta nyumba na viwanja zikawa nyingi
Wazabuni mbalimbali wanaoidai serikali wakafurika kwenye wizara walizofanyia kazi kudai chao
Shughuli nyingi za ki serikali zikavurugika mpaka mkuu wa mkoa wa Dodoma akasitisha matamko yote ya kuhamia Dodoma kwa wiki mbili

MITANDAO YA KIJAMII YANENA
Vumbi la kuhamia Dodoma lilikuwa kila mahali..mitandaoni kukawa na mijadala ya kila aina lakini wengi wakijikita kwenye haya
.uharaka wa kuhamia Dodoma bila maandalizi
.bajeti ya kuhamia huko
.miundombinu mbinu ya Dodoma
.maisha mapya huko nk
Hapa wengi tulitukanwa kuwa tunakurupuka na kukosoa kila kitu. tukawa wavumilivu kwakuwa tuliona wazi kuwa tuko sahihi

MAHITAJI YA NYAKATI
Ishu ya kuhamia Dodoma iliasisiwa na mwalimu Nyerere, aliona Dodoma kama iko katikati ya nchi hivyo kuwa rahisi kufikika kutoka pembe zote za nchi HII NDIO ILIKUWA SABABU PEKEE KUBWA ya kuhamishia makao makuu ya nchi kwenda Dodoma, kama zipo nyingine ni ndogo ndogo
Kwa dunia ya wakati ule mahitaji ya nyakati yalikuwa sahihi kabisa lakini si sasa na hata baadae , ulimwengu umekuwa kijiji, mambo yamerahisishwa mno maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia yanaifanya hoja ya kuhamia Dodoma kutokuwa VALID kwasasa, siku hizi hatuhitaji posta wala kusafiri masaa mengi kufuata huduma, siku hizi maendeleo yamesogezwa mikoani wilayani na hata sehemu ambazo mwanzoni hazikufikiriwa kabisa....Nyerere angekuwa hai bado angebatilisha huu uamuzi kwa hakika

BAJETI YA KUHAMIA DODOMA
Wakati wa Mkapa ulifanyika upembuzi yakinifu wa bajeti ya kuhamia Dodoma....ilikadiriwa kuwa zilihitajika kiasi cha shilingi za kitanzania TRILIOM MOJA NA BILIONI MIA MBILI...Ni pesa nyingi kwa nchi maskini kama yetu...Mkapa akashindwa
Leo hii tukitaka kwa hakika kuhamia Dodoma sijui bajeti yake itakuwa shilingi ngapi na hiyo pesa itapatikanaje
Lakini je kuhamia Dodoma kwasasa ndio kipaumbele? Faida zake ni zipi kiuchumi? Sio kwamba tunataka tu kuwatajirisha watu wachache?wengi wakiwa ni raia wa nje...kwakuwa miundombinu mingi watapewa wao kujenga
Je tumeshajitosheleza kwenye huduma zetu muhimu za kijamii? Elimu afya miundombinu nk?
Bandari zetu bado zinahitajika ukarabati mkubwa reli zetu pia nk ...tuwwkeze huku kwanza kunakotuingizia chochote

HITIMISHO
Mkuu wa nchi alisema atahakikisha serikali yake inahamia kabla muhula wake haujaisha na akasema AKIHAMA yeye wengine watafuata
Ina maana watendaji wake hawakumuelewa ama ni nidhamu ya uoga au ni upungufu wa kufikiri?
Hivi rais akisema ataenda Uganda kwa mfano mwezi ujao wewe mtendaji wake ukasema utaenda kabla yake atakuelewaje?
Tujifunze kusikiliza na kutafakari kabla ya kutenda...ishu ya Dodoma itupe somo na kutufumbua macho tusije tukaja kuchukua maamuzi ya kukurupuka yatakayoligharimu Taifa
Mungu ibariki Tanzania
Mkuu kuna Uzi ulianzisha mwanzoni kabisa mwa utawala wa Magu naona ulosema yanatimia!!

Kwamba mwanzo wa safari abiria na ndugu zao wanaowasindikiza huwa na furaha na matumaini mengi ya kufika, Dereva huaminiwa sana ila kadiri safari inavyoendelea ndivyo ugumu hujitokeza!!

Yetu macho!!
 
Bila shaka ni upungufu wa kufikiri uliofanywa mchanyato na nidhamu ya uoga. Nina uhakika ukimuuliza mama Jenista kwa nini anaharakisha kwenda Dodoma by September, jibu lake litakuwa ni "kutaka kumuwahi PM". Ukihamia kwa Majariwa na kumuuliza swali hilo hilo, usishangae kujibiwa anatimiza agizo la mkuu. Nothing more.

Na Wazabuni waendelee kuzibana korodani zao tu mpaka kiherehere cha kuhamia Dom kiishe.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] hapo kwenye korodoni nimewaza tu kama mlengwa ni mwanamke
 
Mkuu kuna Uzi ulianzisha mwanzoni kabisa mwa utawala wa Magu naona ulosema yanatimia!!

Kwamba mwanzo wa safari abiria na ndugu zao wanaowasindikiza huwa na furaha na matumaini mengi ya kufika, Dereva huaminiwa sana ila kadiri safari inavyoendelea ndivyo ugumu hujitokeza!!

Yetu macho!!
Ni kweli ila title nimeisahau please nipatie link kama hutajali
 
Dah... Hebu mwenyeakili na resources atupe takwimu serikali ikihamia Dodoma jiji la Dar litapoteza watu wangapi??? Tumechoka na hizi akadabradabra [emoji124] [emoji124] [emoji124] [emoji124]
 
Kuhamia Dodoma hakuna faida yoyote kwa Tanzania ya leo,labda kupata sifa za kijinga tu kuwa mtu fulani amefanikiwa kuhamisha makao makuu ya nchi Dodoma
 
Mijitu mingine buana taabu kwelikweli, kila kukicha yanaibua mapya, sijui yamekula maharage ya wapi
 
Rudia kusoma kwa makini nilichoandika tafadhali
Watu wa dizaini hio utawachoka tuu maana akili yao inelowekwa kwenye ile rangi ya kijani, na madhara yake hayafutiki hata kwa kifutio cha Nataraj ni tabu tupu mkuu Mshana Jr
 
Back
Top Bottom